Rafed English

Nafasi Ya Ahlulbayt (as)

Nafasi Ya Ahlulbayt (as) by : Allamah Syed Murtadha Askari

 

Kitabu kilichoko mikononi mwako, ni tarjuma ya kitabu cha Kiingereza, kwa jina la: "The role of Ahlul Bait (as) in Preserving the teaching of Islam" Tarjuma ya Mulla Asghaar M. M. Jaffer kutoka lugha ya Kiarabu. Sisi tumekiita: "Nafasi ya Ahlul Bayt katika kuhifadhi mafub- disho ya Kiislamu."

Mwandishi wa kitabu hiki amelishughulikia sana suala la ‘tawhid’. Suala hili limezua mjadala mkali sana miongoni mwa wanachuoni wa Kiislamu, wengine wakimhusisha Mwenyezi Mungu na viungo na makazi na wengine wakiwa wanaikataa dhana hiyo, kila upande ukitoa hoja na dalili zake. upande mmoja ni wa wanachuoni wa Madhehebu ya Sunni ambao wanaunga mkono dhana hii, na upande mwingine ni wa wanachuoni wa Kishia ambao wanapinga dhana hiyo.

Mwandishi wa kitabu hiki (Allamah Syed Murtadha Askari, mwanazuoni wa Kishia’h) amelishughulikia suala hili kwa kulinganisha hoja za pande zote mbili kwa kutumia vitabu vyao vya tawhid na vya hadith, na akahitimisha kwa kuonesha pasina shaka yoyote kwamba Mwenyezi Mungu yu mbali na hayo wanayo mhusisha nayo.

Sisi tunamuachia msomaji asome kwa makini na utulivu, na uwamuzi utakuwa ni wake; bali matumaini yetu ni kwamba ataelekea kule kwenye haki, bila ya kujali haki hiyo iko kwa nani.

Tumekiona kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote. Kutokana na ukweli huu, Taasisi yetu ya 'Al-Itrah Foundation' imeona ikitoe kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili, kwa madhumuni yake yale yale ya kuwahudumia

Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili.

Tunamshukuru ndugu yetu, Ramadhani Kanju Shemahimbo kwa kukubali jukumu hili la kukifanyia tarjuma kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwa kitabu hiki.

Mchapishaji:
Al-Itrah Foundation
S. L. P. 19071 Dar-es-Salaam

Marhum Mulla Asghar ameacha alama isiyosahaulika katika Jumuiya nzima ya Shi’a katika zama hizi. Mtu mwenye kipaji cha ubora huu, na athari kama hii, anachipukia mara moja tu katika maisha. Kama mubaligh adhimu, aliwasilisha kwa ufasaha kabisa mafundisho ya Ahlul Bayt (a.s.) kwa watu kwa jumla. Akithibitishwa na wanazuoni wa wakati wake, umaizi wake wa kina katika masuala ya Fiqh, theolojia, falsafa, teosofia (imani kwamba wanadamu wanaweza kumfahamu Mungu na kuwasiliana Naye kwa kutulia na elimu ya kina) na vile vile masuala ya nyakati hizi, yeye alikuwa maarufu. Kama muelimishaji kwa kiwango cha hali ya juu kabisa, uwezo wake wa kujulisha na kuelimisha wanafunzi wake juu ya fikra za Kiislamu kwa kweli ulikuwa unataalimisha sana. Kwa kupitia fikra zake, maandishi yenye kuchochea na hotuba zenye msukumo, vichwa au akili nyingi zimefanywa zianzishe tafakari, na maisha ya watu wengi yamebadilishwa. Athari zake juu ya jamii yetu ilikuwa kama ya ajabu sana na ambayo imekuwa ya kusaidia sana katika kubadilisha mifano (ya maisha).

Ninatumaini kwamba mfululiza huu wa vitabu wenye ukumbusho, vinavyozingatia maadhimisho ya miaka 25 ya Jumuiya yetu ya Kimataifa - World Federation – utaendelea kunururisha mafundisho ya Ahlul-Bayt (A.S.) kwa ulimwengu kwa jumla kupitia maneno ya mwanazuoni huyu mashuhuri. Kwa kuunga mkono Mfuko wa Kumbukumbu wa Mulla Asghar (Mulla Asghar Memorial Fund), ambao, miongoni mwa miradi ya kielimu, umefanya mfululizo huu wa machapisho kuwezekana, utasaidia kuhakikisha kwamba mapenzi yake juu ya kueneza mafundisho ya Ahlul- Bayt (A.S.) yanaendelea baada yake. Kwa pamoja, tunaweza kuleta ukweli kwenye zile ndoto nyingi alizokuwa nazo na kusaidia World Federation kuendelea katika njia ya huduma ambayo aliieneza chini ya uongozi wake wenye haiba kubwa. Ninawaombeni kumkumbuka Mulla Saheb kwa kumsomea Suratul-Fatihah

Hasanain Walji
Raisi, World Federation, KSI Muslim Communities.
Allamah Syed Murtadha Askari
Allamah Syed Murtadha Askari ni mwanazuoni wa Shia’h anayetambulika, ambaye vitabu vyake katika historia ya Kiislamu, masomo yanayowiana ya madhehebu mbalimbali ndani ya jamii ya Uislamu na falsafa, vimeacha alama isiyofutika.

Kwenye kutambulika heshima yake kuna vitabu vikubwa kama “Abdullah ibn Saba,” “Masahaba wa Mtume (s.a..w.w.) 150 wa bandia,” na kile “Sifa bainifu za kawaida za madhehebu mbili (za Kiislamu).” Baadhi ya uchambuzi wa awali na uchunguzi wa kisayansi katika nyanja ya historia ya Kiislamu umevunja zile fikra na mawazo yaliyokuwa yamekubalika hadi sasa, na kusababisha makelele yasiyo na kifani, ambayo hayajawahi kutokea miongoni mwa washikilia elimu ya vitabuni wasiobadilika na wenye imani kamili ya dunia ya Kiislamu.

Kama mwanaharakati wa kisiasa, Allamah anafahamika kwa maoni yake thabiti na mapambano juu ya kuhuisha Uislamu. Wengi wa marafiki zake na washirika wake wameuawa kishahidi na utawala katili wa Iraqi. Allamah yuko juu sana miongoni mwa wanazuoni wakubwa wanaoweza kusimama kutokana na makumbusho ya nyuma ya mapambano makali dhidi ya uasi wa kujitokeza kwa Wa-Ba’th. Yeye ni mzungumzaji mwenye mvuto na muongeaji mcheshi; na hata katika umri wa zaidi ya miaka themanini, haonyeshi dalili yoyote ya kudhoofika kwa raghba!

Mwenyezi Mungu amdumishe zaidi!
Imani za kikristo na kiyahudi, hususan utamaduni wa kiyahudi ulienea miongoni mwa Waislamu katika njia mbili: kwanza kabisa, kupitia juhudi za wakristo na wayahudi wenyewe, na pili kupitia kwa Waislamu fulani.

Hebu tuzichunguze njia hizi mbili kwa kinaganaga:

Kuenea kwa imani za Kikristo na Kiyahudi miongoni mwa Waislamu kupitia juhudi za makusudi kabisa za Wakristo na Wayahudi.

Huko nyuma, tumeelezea nafasi ya wanazuoni wa Kikristo na Kiyahudi katika kuzua hadithi. Tunajua kwamba pale Makhalifa walipokataa kuruhusu uenezaji wa hadithi za Mtume (s.a.w.w.), kwa hisani sana wao waliwaruhusu wanazuoni wa Kikristo na Wayahudi ambao walikuwa wameingia katika Uislamu ili kueneza fikra zao wenyewe miongoni mwa Waislamu. Mathalan, Tamim Darii, aliyekuwa mtawa wa Kikristo kabla ya kuukubali Uislamu, aliruhusiwa rasmi na Khalifa Umar kuhutubia Waislamu siku za Ijumaa, kabla ya hotuba ya Swala ya Jama’a, ndani hasa ya Msikiti mkuu wa Mtume (s.a.w.w.). Katika zama za Uthman, aliruhusiwa rasmi kufanya hivyo mara mbili kwa wiki.

Vivyo hivyo, Ka’b al-Ahbar (ambaye jina lake la kwanza lilikuwa ni Mati’) alikuwa ni kuhani aliyefahamika vizuri kabla yeye kuukubali Uislamu. Alijulikana kama Ka’b al-Habr au Ka’b al-Ahbar, kwani Habr kwa Kiarabu ina maana ya mtakatifu, mtu mwenye elimu. Katika siku za Khalifa Umar, Ka’b al-Ahbar alipandishwa kwenye cheo cha Msimamizi wa Baraza, na Uthman vile vile aliendelea kumlea yeye. Waislamu walimwendea katika mas’ala ya kanuni na ufafanuzi wa Qur’ani Tukufu.1

Ka’b alijaribu kiasi alivyoweza katika kueneza imani zilizochimbukia kutoka kwenye masimulizi yaliyopotoshwa ya Taurati, na dhana nyingine za Kiyahudi, miongoni mwa Waislamu. Baadhi ya watu wa wakati huo huo ambao waliwafuata Ahlul-Bayt (A.S.) walikuwa wanatambua juu ya mbinu zake za kichochezi, kama inavyoshuhudiwa katika kadhia ifuatayo:

Tabari katika kitabu chake cha historia anasimulia:

“Ibn Abbas aliambiwa: Ka’b anasema kwamba katika Siku ya Kiyama, jua na mwezi vitakuja kuletwa kama madume ya ng’ombe mawili yaliyochanganyikiwa na kutupwa ndani ya Jahannam.”

Alipoyasikia haya, Ibn Abbas alikasirika sana, na akajibu kwa ukali mara tatu:

“Ka’b ni muongo! Ka’b ni muongo! Ka’b ni muongo! Hii ni fikra ya Kiyahudi, na Ka’b anataka kuiingiza katika Uislamu. Mwenyezi Mungu yuko Huru kutokana na vitu wanavyomhusisha navyo. Yeye kamwe haviadhibu vile vinavyomtii. Hujamsikia Mwenyezi Mungu akisema ndani ya Qur’ani Tukufu kamba:
وَسَخَّرَ لَكُمُ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ دَائِبَيْنِ ۖ وَسَخَّرَ لَكُمُ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ {33}
“Naakakutiishienijuanamwezi,vifanyavyokazi(vikifuatanjiazao) mfululizo.’”(Ibrahim;14:33)
Ibn Abbas akasema: “Hii ‘Daibain’ iliyotumika katika Ayah hii inaonye- sha utii wa wakati wote kwa Mwenyezi Mungu.”

Kisha akaendelea:

“Yeye atawezaje kuyaadhibu haya maumbo mawili ya ki-mbinguni ambayo Yeye Mwenyewe anayasifia kwa utiifu wao? Mwenyezi Mungu Amlaani mwanazuoni huyu wa Kiyahudi na elimu yake! Ni ufidhuli usio na aibu kiasi gani huu wa kuhusisha uongo kwa Mwenyezi Mungu, na kutia hatia kwa viumbe viwili hivi vitiifu!”

Baada ya kuyasema haya, Ibn Abbas akarudia mara tatu kusema: “Sisi sote ni wa Allah, na Kwake Yeye tutarejea.”

Halafu Ibn Abbas akaendelea kusimulia kile ambacho Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) hasa alichokisema kuhusu jua na mwezi. Mtume alisema:

“Mwenyezi Mungu ameumba vyanzo viwili vya mwanga. Kile ambacho Yeye alikiita jua kilikuwa kama ardhi, baina ya sehemu za mawio na machweo. Na kwamba kile alichokiamuru kuwa bila mng’aro kwa nyakati fulani, Yeye alikiita mwezi na akakifanya kuwa kidogo zaidi kuliko lile jua. Na vyote huonekana kuwa kama vidogo kutokana na urefu wao katika anga na umbali wao kutoka ardhini.”2
Uchunguzi Ulioegemea Juu Ya Hadith Hizo Mbili
Kutoka kwenye Hadith hizi mbili, ambazo ni, ile moja kutoka kwa Ka’b na nyingine kutoka kwa Ibn Abbas, tunaona kwamba:

1. Ibn Abbas alikanusha na kukataa yale ambayo Ka’b aliyahusisha na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na akanukuu kutoka kwenye Qur’ani Tukufu:

“Na akakutiishieni jua na mwezi, vifanyavyo kazi (vikifuata njia zao) mfululizo……..”

Akitoa hoja kwamba juhudi yote hiyo ni sawa na utii kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu hakuwaadhibu wale au vile vinavyomtii Yeye.

2. Katika kukataa zaidi tabia ya Ka’b ya kufuata mkondo wa yaliyotangulia, Ibn Abbas alithibitisha kwamba jua na mwezi yalikuwa ni maumbo makubwa mawili ya kimbinguni kama ardhi, na alitafuta kuungwa mkono na Hadith ya Mtume (s.a.w.w.), ambayo imesema:

“Na vyote huonekana kuwa kama vidogo kutokana na urefu wao katika anga na umbali wao kutoka ardhini.”

Ni dhahiri, haya yalikuwa ndio maamuzi bora kabisa ambayo Ibn Abbas aliyoweza kuyafanya kutoka kwenye Hadith. Hata hivyo, katika zama hizi, tunao uwezo wa kupata mahitimisho zaidi kutoka kwenye Hadith, yaani:

i. Kutajwa kwa sehemu ya mawio na machweo kwa ajili ya jua kuhusiana na ardhi, kunatoa kidokezo kuhusu mizingo na mzunguko wa maumbo ya kimbinguni.

ii. Vile vile kunaashiria kwamba maumbile hayo yanapaswa kuwa ya mviringo (matufe) ili kuwa na sehemu mbalimbali za kutua na kuchomoza. Hili lisingewezekana kama yangekuwa ya ubapa.

iii. Ni wazi vile vile kutokana na namna Ibn Abbas alivyoijadili ile Hadithi iliyosimuliwa na Ka’b kwamba yeye hakuelekea kuukubali uwezo wa kisheria wa Ka’b.

Kwa hiyo, Hadith zote kama hizo, ambazo zina mwonjo wa imani za Kiyahudi na zinahusishwa bila matata kwa Ibn Abbas kwamba amezisikia kutoka kwa Ka’b, hazina msingi na sio za kweli. Hizi zilibuniwa katika wakati wa siku za utawala wa Bani Abbas kwa sababu Bani Abbas walimuamini sana mhenga wao Ibn Abbas. Watu walitengeneza hadithi kwa jina la Ibn Abbas ili kupata umaarufu katika mabaraza ya Bani Abbas. Ulikuja kuwa ni mtindo kuhusisha hadithi za uongo kwa Ibn Abbas, ambazo badala yake ziliunda sehemu kubwa sana ya propaganda ya Kiyahudi na Kikristo.

Ibn Abbas alikuwa na uwezo wa kupata maamuzi fulani kutoka kwenye Hadith za Mtume (s.a.w.w.). Tunao uwezo wa kufanya nyongeza kwenye maamuzi hayo, tukiegemeza uchunguzi wetu juu ya ukweli wa kielimu wa wakati huu. Inaelekea kabisa kwamba hapo baadaye, wakati elimu itakapokuwa imefanya uchunguzi wa ziada, wanazuoni wanaweza kufanya mahitimisho mapya na ya maana zaidi kutoka kwenye Hadith. Lakini simulizi ya Ka’b ni upuuzi wa Kiyahudi, na inazidi kuwa bure zaidi kadiri muda unavyosonga mbele.

Baadaye katika mjadala huu, tutaonyesha taswira ya nafasi kubwa ya Ka’b, kuthibitisha jinsi alivyofanikiwa katika majaribio yake ya hatari.

Kwa masikitiko makubwa, Hadith hii kutoka kwa Ka’b kuhusiana na jua na mwezi kutokea Siku ya Kiyama kama mafahari wawili waliochanganyikiwa, ilipata njia ya kuingia kwenye vitabu vya Kiislamu kupitia kwa masahaba kama Abu Huraira na wengineo.

Haya yametokea licha ya makanusho ya hasira ya Ibn Abbas. Katika Tafsiir ya Ibn Kathiir na katika Kanzul Ummal, imesimuliwa kutoka kwa Abu Hurair kwamba:

Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Katika Siku ya Kiyama, jua na mwezi vitakuwa katika moto wa Jahannam katika umbile la mafahari wa ng’ombe wawili waliochanganyikiwa.”

Mtu mmoja akamuuliza: “Lakini ni kwa dhambi gani walizofanya hadi kustahili adhabu hiyo?”

Abu Huraira akajibu vikali: “Mimi ninakusimulieni ambacho Mtume (s.a.w.w.) amekisema, na wewe unaniuliza mimi namna ya dhambi zao?”

Katika Hadith nyingine dhaifu kutoka kwa Anas, Ibn Kathiir anasimulia yafuatayo: “Jua na mwezi vitakuwa katika moto wa Jahannam kama madume ya ng’ombe mawili yaliyochanganyikiwa.”
Maoni Yetu Juu Ya Haya Yaliyopita
Hadith hizi kutoka kwa Abu Huraira na Anas kwa kweli zinafanana, ni hiyo hiyo moja ambayo ilibuniwa na Ka’b al-Ahbar. Zimehusishwa kwa uwongo kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).

Kama tukiichunguza Ayah hii ya Qur’ani Tukufu na Hadith sahihi kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), tunakuta kwamba haditi hii ya Ka’b ni uzushi wa mawazo yake mwenyewe, zilizoegemea kwenye fikra za Kiyahudi. Baada ya kuthibitisha kwamba hadithi hii kutoka kwa Ka’b imehusishwa kwa Mtume kwa visingizio vya uongo na kwa msaada wa Ibn Abbas aliyeishutumu kwamba ni utomaji maneno (yasiyokuwepo) wa Kiyahudi, hayabakii mashaka yoyote kwamba chanzo cha hadithi hii ni Ka’b al-Ahbar mwenyewe na wala sio hawa masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).

Hatari hii ilikuwa imetambuliwa na masahaba wa mwanzoni wa Mtume (s.a.w.w.). Ibn Abbas alikuwa miongoni mwa wale wa kwanza kusimama kidete dhidi ya mashambulio ya muingilio wa Kiyahudi, na Imam Ali (a.s.) vilevile alimuonya Khalifa Umar kuhusu jambo hili.

Kwa vile Ka’b hakuwa miongoni mwa masahaba wa Mtume (s.a.w.w.) hakuweza kuhusisha kiini cha imani yake ya Kiyahudi kwa Mtume mwenyewe moja kwa moja. Njia ya kufaa sana kwake ilikuwa ni kuandaa njia ambayo ingezichukua hadithi hizo kwa kutumia majina ya masahaba fulani fulani kama Abu Huraira na wengineo.

Ingawa ile hadithi kutoka kwa Anas imethibitishwa kwamba ni dhaifu, hadithi nyingine kutoka kwa Abu Huraira juu ya suala hilo hilo ilichukuliwa kama ni sahihi, na kwa hiyo ikatoa nguvu kwenye uzushi wa Ka’b. Ilikuwa ni juhudi ya pamoja, za makusudi kabisa au vinginevyo, za wale wanazuoni wa Kikristo na Kiyahudi waliosilimu, na masahaba kadhaa na wale ambao walifuatia zama za masahaba.
Kuenea Kwa Imani Za Kikristo Na Kiyahudi Miongoni Mwa Waislamu Kupitia Kwa Waislamu Wenyewe
Ili kuifanya hoja yetu ieleweke vizuri zaidi, tunatoa mifano miwili ya masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), na vile vile nukuu kutoka kwenye mojawapo ya Tafsiir.
(1) Abu Huraira, Mmoja Wa Masahaba Wa Mtume (S.A.W.W.):
Historia imerekodi majina matatu tofauti ya sahaba huyu mmoja. Hata hivyo, yeye ni maarufu sana kwa Kuniyat yake ya Abu Huraira. Yeye alitokana na kabila la Dus, ambalo lilichipukia kutoka Yemeni.

Abu Huraira aliishi huko kwa miaka thelathini na aliwasili Madina baada ya vita vya Khaibar. Kwa mujibu wa Bukhari, Ibn Sa’d na wengineo, yeye alikuwa pamoja na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika ile miaka mitatu ya mwisho.

Lakini ukichukulia ule ukweli kwamba aliondoka kwenda Bahrain mnamo mwezi 8 Hijiria pamoja na jeshi lililoongozwa na Ala’ Hadhrami, jumla ya siku zake pamoja na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), ni dhahiri kwamba inakuwa ndogo zaidi.

Alikuwa akiishi pamoja na wale Waislamu masikini katika kishubaka cha jiwe kilichojulikana kama Suffah kilichokuwa kimekingama katika Msikiti wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).

Wakati Mu’awiyah alipomtuma yule muuaji muovu sana, Busr, ambaye alihusika na yale mauaji ya halaiki ya Waislamu thelathini elfu wasiokuwa na hatia, baina ya Syria na Yemeni, Abu Huraira aliteuliwa kuwa kama gavana wa Madina kwa baraka zake Busr.3 Halafu aliendelea kubakia na nafasi hiyo hiyo kwa muda fulani katika utawala wa Mu’awiyah.4

Hizi zilikuwa ndio siku za Abu Huraira ambazo alipata muda muafaka haswa wa kuzieneza hadithi zake. Baadhi ya masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) walikuwa kwa kweli wanao ujuzi hasa katika sanaa ya kusoma na kuandika lakini kwa bahati mbaya, Abu Huraira alikuwa sio mmoja wao. Bukhari anamnukuu yeye akisema: Abdullah bin Amru Aas alikuwa anajua kuandika wakati mimi nilikuwa sijui.” Miongoni mwa watu ambao kutoka kwao yeye alipata faida za hali ya juu sana alikuwa ni Ka’b al-Ahbar ambaye alitoa sifa zifuatazo kwa Abu Huraira:

“Kati ya watu ambao hawakuwa wamesoma Taurati na bado wakawa na ujuzi na kuifahamu vizuri sana, Abu Huraira alikuwa ndio mbora wao.”5

Hii ni kusema kwamba, mbali na yule rabi (kiongozi wa dini ya Kiyahudi) ambaye bila shaka alikuwa ameisoma Taurati, Abu Huraira kwa umaarufu aliwapita wengine wote katika ujuzi wa Taurati. Cha kufurahisha vya kutosha, Ibn Kathiir ndani ya Tariikh yake anatoa maoni hivi:

“Abu Huraira alikuwa mdanganyifu, akichanganya kwa ulaghai kile alichokisikia kutoka kwa Ka’b na kile ambacho alikisikia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), bila ya kuyapambanua moja kutokana na jingine.”

Anaendelea zaidi kusema kwamba: “Wafuasi na marafiki zetu wanazitupilia mbali baadhi ya hadithi za Abu Huraira.”

Na vile vile anasema: “Wao hawakuweza kukubali kila hadithi ambayo ilisimuliwa na Abu Huraira.”6

Kipengele kinachouma sana ni kwamba Abu Hurair bila haya na hofu anasimulia hadithi mbili zinazopingana kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).

Bukhari ndani ya Kitab al-Tib anasimulia yafuatayo kutoka kwa Abu Huraira:

“Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: ‘Maradhi hayaambukizi au kuenea.’ Kisha Mwarabu mmoja akasimama kuuliza: ‘Ewe Mtukufu Mtume, tunao ngamia wazuri sana katika jangwa. Lakini pale mmoja wao anapopatwa na ugonjwa wa vidonda, wengine nao vile vile huwa wanaambukizwa.’ Mtume (s.a.w.w.) akauliza: ‘Huyo ngamia wa kwanza aliambukizwa vipi?’”

Baada ya kunukuu hadithi hii, Bukhari anaendelea kusimulia hadithi nyingine:

“Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ameagiza kwamba wale ambao wanaugua na wenye maradhi wasiwatembelee wale wenye afya njema.” Abu Salmah, ambaye ni binamu yake Abu Huraira akauliza: “Ewe Abu Huraira! Hivi wewe hukusimulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) hakuwa akiamini juu ya maambukizo?”

Katika kujibu, Abu Huraira alitoa matamshi fulani katika lugha ya Kihabeshi! Kisha yule binamu yake Abu Huraira akasimama kumtetea Abu Huraira kwa kusema:

“Sijawahi kamwe kumuona Abu Huraira akiwa msahaulifu isipokuwa kati ka tukio hili.”

Ni dhahiri kwamba, Abu Salma alikuwa akijaribu kuhalalisha ule upinganaji katika hadithi za Abu Huraira. Hata hivyo, msemo maarufu unasema hivi: “Pale mtu anapokuwa kama Abu Huraira, huyo huelekea kusahau.”
Abu Huraira Anakiri
Cha kushangaza ajabu ni kule kukubali kwa Abu Huraira mwenyewe kwamba amewahi kusimulia hadithi fulani fulani kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) bila ya kuwa amezisikia kutoka kwake.

Imam Ahmad Hanbal anasimulia tukio fulani ndani ya Musnad yake:

“…….. na Abu Huraira alisimulia hadith na wasikilizaji wake wakauliza: “Hii inatoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) au imetoka mfukoni mwako?” Abu Huraira akasema: “Hii moja makhsusi ni yangu mwenyewe kutoka mfukoni mwangu.”

Bukhari analisimulia tukio hili kama ifuatavyo:

“Abu Huraira aliulizwa: ‘Je hii uliisikia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)?” Naye akajibu: “La hasha, hadithi hii ni yangu mwenyewe.”

Katika hadithi nyingine iliyosimuliwa na Imam Ahmad Hanbal, tunayakuta haya:

“Abu Huraira alisimulia Hadith kana kwamba ameisikia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), lakini mwishowe alikiri kwamba ilikuwa ni yake mwenyewe kutoka mfukoni mwake.”
(2) Abdullah Bin Amru Aas, Mtetezi Wa Hadithi Za Kiyahudi:
Abdullah bin Amru Aas (aliyefariki mnamo mwaka wa 65 Hijiria) anachukuliwa kama mmoja wa masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), na kwa vile alikuwa amerithi hazina kubwa ya dhahabu ya Ki-Misri kutoka kwa baba yake, alijulikana kama mmoja wa matajiri wakubwa miongoni mwa masahaba. Yeye aliijua lugha ya Syria (Suryani), lugha asili ya Taurati.

Katika vita vya Yarmuk, yeye aliongoza jeshi la baba yake kama mshika bendera wake, na aliweza kuzitia mkononi shehena za ngamia wawili za vitabu vya Kiyahudi na Kikristo.7

Dhahabi anasema:

“Abdullah amesimulia kutoka kwa Watu wa Kitabu. Alivisoma vitabu vyao kwa mfululizo, na alionyesha upendeleo maalum juu ya vitabu hivyo.”

Ibn Hajar katika Sharhe yake juu ya Sahih Bukhari anasema:

“Abdullah katika mapambano ya Damascus alipata shehena ya ngamia mmoja ya vitabu vya Kiyahudi na Kikristo kama ngawira ya kivita. Alivisoma kwa uangalifu sana na akazitegemeza hadithi zake juu ya vitabu hivyo. Kwa sababu ya hili, watu maarufu wa kundi la Tabi’in (waliofuata baada ya masahaba) walijizuia kusimulia kutoka kwake.”

Katika Musnad ya Imam Ahmad Hanbal tunayakuta yafuatayo:

“Mtu mmoja alikuja kwa Abdullah na akasema: ‘Hebu niambie kile ulichokisikia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na wala usinisimulie zile hadithi kutoka kwenye Taurati na Injili.”

Katika hadithi nyingine tunasoma haya:

“Abdullah aliambiwa: ‘Hebu niambie yale uliyoyasikia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na wala usinisimulie yale uliyoyapata kutoka kwenye ile shehena ya ngamia wa Yarmuk.”8

Wanazuoni wa Hadith wa Kiislamu wamezitenga Hadith hizo kama ni za kiyahudi (Israiliyyat) – kwa sababu ya asili yao kutoka kwenye Taurati na vyanzo vingine vya Kiyahudi.

Katika lundo la Hadith zilizotwaliwa na wale Waislamu ambao hawatokani na madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s.), tunazikuta Hadith nyingi zinazozungumzia juu ya Mwenyezi Mungu kuwa na mwili. Hizi ni dhahiri kabisa kwamba zinatoka kwenye vyanzo vya Kiyahudi na mara kwa mara tunakuta kwamba zimesimuliwa kutoka kwa Ka’b al-Ahbar au Abu Huraira. Tutakuja kuzijadili hizi kwa kina hapo baadaye.
(3) Maqatil Ibn Sulayman Balkhi:
Yeye huyu alikuja kutoka Balkhi. Aliachiwa huru na kabila la Azd, na akat- waa kuniyat ya Abul Hasan. Katika kuishi kwake mjini Basra na Baghdad, alisimulia hadithi kadhaa kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.), na alikubalika kama mmoja wa wanazuoni maarufu wa elimu za Qur’ani Tukufu na ile madhehebu kinyume na ya Ahlul-Bayt (a.s.).

Miongoni mwa vitabu vilivyotungwa na yeye ni:

Tafsir Kabir – ambacho nakala ya mwandiko wa mkono bado ipo nchini Misri.

Nawadir ya Tafsiri

Al-Ayat al-Mutashabihat

Al-Nasikh wal Mansukh

Al-Qiraat

Al-Ashbah wa al-Nazair fil Qur’an al-Karim

Al-Jawabat fil Qur’an

Ibn Khaldun, katika kitabu chake cha wasifu cha Maqatil, anasimulia kutoka kwa Ibn Habban kwamba:

“Alikuwa akikubali ufafanuzi wa Qur’ani Tukufu kutoka kwa Wayahudi na Wakristo ambao waliitafsiri kwa mujibu wa vitabu vyao wenyewe!”

Na halafu anaendelea tena:

“Maqatil alikuwa miongoni mwa wale waliohusisha sifa za kibinadamu na namna ya kufanana (analojia) kwa Mwenyezi Mungu, na zaidi ya hayo, yeye alikuwa anadanganya wakati alipokuwa akisimulia Hadith.”9

Khatib Baghdadi katika historia yake – Taarikh Baghdad anasema:

“Siku moja, Muhammad bin Said Kalbi (aliyefariki 146 Hijiria) alitokea kupita karibu na Maqatil na akamsikia yeye akisimulia baadhi ya Hadith fulani fulani, akizihusisha kwa Kalbi mwenyewe. Hivyo akasema: ‘Ewe Maqatil! Mimi ndiye Muhammad bin Said Kalbi, na kamwe sijasimulia hadithi hizo ambazo umezitaja hivi punde hapa!”

Maqatil akasema:

“Tunazipamba hadithi zetu kwa majina ya wasimuliaji mashuhuri.”

Maqatil alikuwa na maana kwamba aliambatanisha majina ya wasimuliaji mashuhuri kwenye uzushi wake mwenyewe ili kwamba upate kusadikika!

Muhammad bin Said Kalbi vile vile anasimuliwa kuwahi kusema kwamba:

“Maqatil amezihusisha kwangu kwa uongo hadith ambazo sijawahi kuzitamka, na yeye amezijumuisha katika Tafsir yake.”

Khatib Baghdadi ndani ya maelezo yake juu ya Maqatil anasimulia tukio lililosimuliwa na watu wawili:

“Tuliuliza kutoka kwa Maqatil kuhusu chanzo cha hadithi yake moja mahususi, naye akasema: ‘Mimi niliisikia kutoka kwa Dhahhak.’ Baada ya siku chache tulipomuuliza tena kuhusu hadithi ile ile, yeye akasema: ‘Niliisikia kutoka kwa Ata.’ Katika wakati mwingine aliihusisha kwa Isa.

Baada ya kulisimulia tukio hili, Khatib Baghdad anasema kwamba mtu mmoja alimuuliza Maqatil kama aliwahi kumuona kamwe huyo Dhahhak, ambaye amedai kuwahi kumsikia. ‘Hakika ndiyo!’ Akasema Maqatil. ‘Kulikuwa na mlango uliokuwa umefungwa kati yangu na yeye.’”

Baghdad anaelezea kwamba kwa ile “mlango uliofungwa,” Maqatil alimaanisha lile lango kuu la jiji la Madina, kwa vile Dhahhak aliishi Madina na yeye Maqatil hajawahi kufika huko Madina kamwe.

Ibn Khallikan anasema:

“Dhahhak bin Mazahim, ambaye kutoka kwake Maqatil alisimulia hadith, alifariki miaka minne kabla yeye Maqatil hajazaliwa, na alizikwa ndani ya uwanja wa makaburi huko Madina!”

Zaidi ya hayo, yeye anaongezea:

“Maqatil alisimulia kutoka kwa Mujahid bila hata ya kuwa amewahi kuku- tana naye!”

Khatiib Baghdad ameandika kisa kifupi cha kuvutia sana (kinachomhusu Maqatil). Yeye anasema:

“Mtu mmoja alimuuliza Maqatil: ‘Rafiki yangu alitaka kujua rangi ya yule mbwa wa As’habul-Kahf. Mimi sikuwa na jibu la kumpatia.”

Maqatil mara moja akajitolea kujibu. Yeye akasema:

“Mwambie mbwa huyo alikuwa na madoadoa. Hakuna mtu atakayekanusha hili!”

Anaendelea kusimulia kutoka kwa Mansur na Mahdi, wale wafalme wa ki- Bani Abbas kwamba Maqatil wakati mmoja alijitolea kutunga hadithi chache za uongo katika kumsifu mhenga wao Abbas, kama wao wangependa hivyo. Wote wawili walimkatalia.10

Kwa kupitia vitabu kadhaa ambavyo ndani yake picha ya haraka ya maisha ya Maqatil imeonyeshwa, tunakuta mifano mingi ya uzushi na udanganyifu. Kuhitimisha, yeye alikuwa ni wakili madhubuti wa ile dhana ya kwamba Mwenyezi Mungu alikuwa na umbo la mwanadamu.

Yeye alijifunza tafsiri ya Qur’ani Tukufu kutoka kwa washauri wake wa Kiyahudi na Kikristo na akazinakili imani zao katika kitabu chake juu ya Tafsir. Licha ya haya, inashangaza kweli kweli kuona kwamba wanazuoni kutoka madhehebu kinyume na ile ya Ahlul-Bayt (A.S.) wamemimina sifa nyingi juu ya Tafsir yake.

Ibn Khalidun anasema:

“Katika elimu ya Tafsir, watu wote ni wanyenyekevu kwa Maqatil bin Sulayman …!”
Mifano Ya Hadithi Zilizotengenezwa Na Maqatil, Katika Kuwaunga Mkono Makhalifa:11
Khatib Baghdad, katika kitabu chake kikubwa cha historia, Tarikh Baghdad, anasimulia kupitia nyororo inayoendelea ya wasimuliaji:

Maqatil amesema: “Dhahhak amenisimulia mimi kutoka kwa ibn Abbas kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alishauriwa na masahaba zake kumteua mrithi wa nafasi yake ili aweze kujulikana kwa watu, na kwamba watu watapeleka masuala yao kwake. ‘Hatujui ni nini kitakachotokea baada ya w e we kuondoka.’”

Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akajibu:

“Kama ningeteua mtu ambaye angewaongozeni ninyi katika kumtii Mwenyezi Mungu, nanyi mkaacha kumtii yeye, basi mtakuwa mnapuuza maagizo yangu na yale ya Mwenyezi Mungu. Na kwa upande mwingine, kama mtu kama huyo aliyeteuliwa akawaelekezeni katika kufanya maovu na mkamtii, mtakuwa mmewekwa vyema Siku ya Kiyama kumtaja yeye kama mwenye uwezo wa kisheria. La hasha, mimi sitafanya kamwe jambo kama hilo – ni afadhali mimi nikawaacheni kwenye uangalizi wa Mwenyezi Mungu!”
Tathmini Ya Hadith Hiyo Hapo Juu:
Hadith hii ilibuniwa na Maqatil ili kuwaunga mkono Makhalifa ambao walidai kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) hakuteua mrithi yeyote wa nafasi yake, na kwamba haki ya uteuzi kama huo ilikuwa mikononi mwa umma wa Kiislamu.

Inapendeza kuona kwamba Khatib ameinakili hadith hiyo hapo juu kwenye kitabu chake cha wasifu wa Maqatil kuthibitisha kutoaminika kwake na udanganyifu wake. Anahoji kama Maqatil alikuwa na ujasiri wa kusimulia kutoka kwa Dhahhak bila ya yeye kukutana naye kamwe. Dhahhak aliishi Madina, ambapo Maqatil hakuwahi kusafiri kutoka Khurasan kwenda Madina. Ukweli ni kwamba Dhahhak alifariki miaka minne kabla Maqatil hajazaliwa!

Baada ya mfano huo hapo juu wa upenyezaji wa Kiyahudi na Kikristo katika imani za Kiislamu, tunaona inafaa kunukuu visa viwili vifupi kutoka kwenye Taurati. Hivi vitasaidia sana kwenye tathmini ya imani zinazashikiliwa na madhehebu kinyume na ile ya Ahlul-Bayt (a.s.), hususan kuhusiana na Sifa za Mungu.
1. Kuumbwa Kwa Adam
Katika Kitabu kile cha Mwanzo, Mlango wa Kwanza, mstari wa 27, tunasoma kama ifuatavyo: “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu yeye alimuumba, mwanaume na mwanamke aliwaumba,”

Hadithi hiyo inaendelea kusema kwamba Adam na Hawwa waliwekwa katika Bustani ya Adeni. Halafu Mungu “akawapotosha”:

“Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, usile: kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.11 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akawaambia: ‘Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.’

‘Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala,akam- pa na mumewe, naye akala. Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi.

‘Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu asiwaone. ‘Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, uko wapi?

‘Akasema: Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha. Akasema, Ni nani aliyekwambia ya kuwa u uchi? Je! umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale?’

‘Ndipo Adamu akaeleza yale ambayo yaliyotokea, hivyo Mungu akawaapiza Adamu, Hawwa na yule nyoka na akawalaani wao na vizazi vyao kwenye maisha ya kuhangaika, huzuni na kazi ngumu juu ya ardhi.

‘Bwana Mungu akasema, basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele. ‘….. Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Adeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima.”11
2. Shindano La Mieleka Kati Ya Yakobo (Yaqu- Ub) Na Mungu:
Usiku mmoja, Yakobo alipigana mieleka na Mungu hadi kukacha, lakini Mungu hakufaulu kumshinda Yakobo!

“Yakobo akakaa peke yake; na mtu mmoja akashindana naye mweleka hata alfajiri. Naye alipoona ya kuwa hamshindi….. akasema: ‘Niache, niende maana kumepambazuka.’ Akasema: ‘Sikuachi usiponibariki.’

‘Akasema: Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda… Na Yakobo akapaita mahali pale, Penueli, maana alisema, nimeonana na Mungu uso kwa uso, na nafsi yangu imeokoka.’”12
Maana Ya Visa Hivi Vifupi:
Kwa uwazi kabisa, Mungu wa Wayahudi ni wa kipuuzi na asiye makini. Analala na kama mwanadamu yeyote mbinafsi, anasema uongo na kudanganya!

Alimdanganya Adam pale alipomuonya asile kutoka kwenye ule mti kwa sababu ingeweza kumsababishia kifo; na alikuwa ni yule nyoka ndiye ambaye aliuondoa udanganyifu huo kutoka kwa Adam na akamlaghai yeye kula kutoka kwenye mti huo. Halafu Adam akawa kama mmoja wa miungu, anayeyajua mema na maovu, akijitambua kwamba alikuwa yuko uchi, alijificha mbele ya Mungu! Wote watatu, yule nyoka, Adam na Hawwa walilaaniwa na kuteseka na kazi ngumu juu ya ardhi!

Kwa mujibu wa Taurati, Mungu ana kiwiliwili; anatembea kutoka sehemu moja kwenda nyingine, na anapigana mieleka na hawezi kumuona mtu anayejificha kutoka machoni Kwake!

Hizo ndizo hadithi za dhihaka za Taurati.
Athari Ya Jumla Ya Taurati
Tunaweza tukawagawanya watu walioathiriwa na upuuzi kama huo katika makundi tofauti yafuatayo:

1. Watu ambao walishtushwa kuona kwamba vitabu vilivyodhaniwa kwamba viliteremshwa kwa Mitume wakubwa kama Musa na Isa, amani juu yao wote, vilikuwa na makosa mengi sana na simulizi potovu na zisizo za kimaadili. Na kwa matokeo ya kupoteza imani kwao, walizitelekeza dini zote zilizofunuliwa na wakageuka kuwa wapenda anasa za dunia katika mwelekeo wao.

2. Kuna kundi jingine ambalo ni imara katika njia ya kidini waliyoichagua, licha ya kuangukia kuwa waathiriwa wa dhana hizi zisizo na maana.

Hawa wako katika vikundi vitatu:
A. Wayahudi
Wao wanahusika na upotoshaji na utomaji wa maneno ndani ya Taurati, na upotoshaji huo unaonekana katika mtazamo wao wa maisha na mwelekeo wao wa kitamaduni. Wanawafundisha watoto wao kufuata mbinu zile zile za ulaghai, kusema uongo na udanganyifu. Wanajiona wao wenyewe kuwa ndio wana wa Israeli, yule ambaye alipigana mieleka na Mungu na akashinda. La muhimu zaidi ya yote, wanachukulia wenyewe kama watu wateule, waliopewa kibali cha kufanikisha malengo yao kwa njia yoyote ile, ikiwa ni pamoja na hila na mauji ya halaiki. Zaidi ya hayo, kwa vile wanaamini katika wale mitume waporaji ambao “….waliaangamiza nafsi zote kwa ncha ya upanga, hata walipokuwa wamewaangamiza wote, wala hawakumsaza mmoja mwenye kuvuta pumzi …”13
B. Wakristo
Inaweza kudhaniwa bila wasiwasi kwamba kuhusisha umbile la kibinadamu kwa Mwenyezi Mungu, kama inavyohubiriwa na Taurati, iliwavutia Wakristo kuamini kwamba Mungu ni kama baba ambaye alijitwalia mwana.

Huko Ulaya, ambako wengi wao wameukiri Ukristo na lile Agano la Kale likakubaliwa kama kitabu cha kwanza ndani ya Biblia, kuzaliwa na kuenezwa kwa tamaa ya anasa za dunia kunaweza kuhusishwa na dhana zisizo na mantiki kama hizo, ambazo zilishindwa kuwavutia wasomi.
C. Waislamu
Miongoni mwa Waislamu, kulikuwa na madhehebu mbili. Moja ilikuwa na mwelekeo kwa Ahlul-Bayt (A.S.), ambapo ile nyingine ilikuwa inapingana nao hao moja kwa moja. Hawa wa mwishoni wanaweza wakaitwa madhehebu ya watawala au Makhalifa. Madhehebu haya ya Makhalifa yaliamini katika kuwepo kimwili kwa Mwenyezi Mungu, kitu ambacho chenye kufanana na umbo la mwanadamu. Ni dhahiri, wazo hilo lilikuwa limeazimwa kutoka kwa Wayahudi, kama tutakavyothibitisha katika milango ifuatayo, Inshallah.

Wakati dini ya kweli ya Mwenyezi Mungu inapochafuliwa kwa lugha yenye maneno ya kufuru, tunaziona dalili za athari za uharibifu katika zile imani halisi. Mafundisho ya Qur’ani Tukufu yalikuwa ya maneno machache ya dhahiri, halisi na wazi, lakini kwa vile wanazuoni wa Kiislamu walianza kuwakubali wale wasimulizi wa ngano wa Kiyahudi na Kikristo kama wafasiri wa Qur’ani Tukufu, hata zile itikadi kuu za Tawhiid zilishushwa na kuwa kama mambo ya kukisia tu.

Kabla hatujaendelea na mada yetu kuu, tunadhani kuna umuhimu wa kujadili yale matumiziya maneno halisi na ya kiistiari.
________________________
1. Tazama Tafsiir Ibn Kathiir, Juz. 4, uk. 17

2. Tabari (Toleo la Ulaya), Juz. 1, uk. 62-63.

3. Al-Gharaat, cha Thaqafi na vile vile Sharhe Nahjul Balaghah cha Ibn Abil Hadiid

4. Musnad ya Ahmad Hanbal

5. Tadhkiratul Huffadh cha Dhahabi

6. Tariikh Ibn Kathir, Juz. 8, uk. 109.

7. Usudul-Ghabah, Juz. 3, uk. 234 na Fat'hul-Bari, Juz. 1, uk. 166

8. Musnad Ahmad Hanbal, Juz. 2, uk. 195, 202. 203, na 209.

9. Wafayat al-A'yan

10. Tarikh Baghdad

11. Nukuu kutoka Kitabu cha Mwanzo; 3.

12. Nukuu kutoka Kitabu cha Mwanzo; 32.

13. Yoshua; 11: 14
Katika Kiarabu au Kifursi, kama vile katika lugha nyinginezo tu, pale neno linapoonyesha maana ambayo kwamba lilitungiwa kwa asili, matumizi yake yanaitwa halisi. Wakati tunaposema: “Mikono ya mwizi ilikatwa,” neno “mikono” katika kadhia hii limetumika katika maana yake halisi.

Lakini pale neno linapotumika kama tamathali ya usemi ambamo linahamishiwa kwenye kitu ambacho halitumiki hasa, linaitwa la kitamathali au kiistiari. Kwa mfano, wakati neno “mkono” linapotumika kumaanisha “uwezo” au “mamlaka” na kadhalika.

Wakati mwingine inasemwa: “Kuna mkono juu ya kila mkono.”

Katika suala hili, maana yake ni kwamba kuna uwezo juu ya kila uwezo. Matumizi kama hayo yanapatikana katika kila kazi ya fasihi, na inaongezea uzuri wa mtindo. Qur’ani Tukufu, katika mtindo wake usioigika na bora sana, hutmia matumizi kama hayo katika sehemu nyingi. Kwa mfano:
وَلَا تَجْعَلْ يَدَكَ مَغْلُولَةً إِلَىٰ عُنُقِكَ وَلَا تَبْسُطْهَا {29}
Wala usifanye mkono wako (kama) uliofungwa shingoni mwako, walausiukunjuwemkunjuowakabisa(BaniIsraail;17:29)
Lakini ni dhahiri kabisa kwamba maneno haya katika Ayah hii sio ya kutafsiriwa neno kwa neno. Maana ya Ayah hii ni: “Usiwe bakhili, wala usiwe mkarimu mno au mbadhilifu....”

Mfano mwingine ni wa neno “Siraat” ambalo katika Kiarabu lina maana ya “barabara” au “njia.” Katika Suratul-Fatiha, kama tutachukua maana halisi ya neno Siraat, Ayah hiyo itasomeka hivi:

“Tuonyeshe barabara iliyonyooka. Barabara ya wale ulioshusha neema Zako juu yao, sio ya wale uliowaghadhibikia au waliopotea.” (Al-Fatiha)

Kwa hakika, Ayah hizi hazizungumzii juu ya barabara zozote zile. Ayah zinazunguzia juu ya njia, ile njia ya Mitume, njia inayoongozea kwa Mwenyezi Mungu, ambayo ni sawasawa na Uislamu. Tunaomba tuonyeshwe njia ya wale waliobarikiwa na kuongozwa na sio ya wale ambao Yeye amewaghadhibikia.
Hitimisho
Kila mwanazuoni wa lugha ya Kiarabu atathibitisha kwamba ule “unyooshaji mkono mbele” katika Ayah ya Qur’ani Tukufu hakuelekezi kwenye viungo vya mwanadamu. Kunamaanisha utoaji mwingi wa tunzo au zawadi. Hali kadhalika, neno Siraat halirejelei kwenye zile barabara zenye mavumbi, linaelekeza kwenye njia ya kiroho na adhimu, Uislamu.

Hata wanazuoni wa wafasiri kutoka kwenye madhehebu tofauti na ile ya Ahlul-Bayt (a.s.) wanakubaliana nasi katika tafsiri hii. Hata hivyo, cha kushangaza zaidi, wakati neno linaloashiria sehemu za mwili kama vile “mkono”, “jicho”, au “kifundo cha mguu” linaonekana ndani ya Qur’ani Tukufu kuhusiana na Mwenyezi Mungu, wao wanasisitiza kwamba lazima lichukue maana halisi, na kwamba wao wanalitumia hasa kwenye viungo vya mwili “Wake.” Madhehebu ya Ahlul-Bayt imeyachukulia maneno haya kuwa na maana ya kiistiari.

Kwa hiyo, ni muhimu kabisa kulinganisha na kupima hoja zinazotolewa na kila madhehebu, na kuchunguza ni vipi kila moja imepata kuungwa mkono na Qur’ani Tukufu na hadith. Hii itatuwezesha sisi kuzielewa zile Sifa Tukufu katika Uislamu.
Uchaguzi Wa Kitabu Kimoja Cha Tawhiid Kutoka Kila Madhehebu
Tumechagua kitabu kimoja kutoka kwenye madhehebu ya Makhalifa na kimoja kutoka madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s.). Kila kimoja kinajishughulisha na maudhui ya Upweke wa Allah.

Tawhii kutoka kwa Ibn Khuzaimah ni ya kutoka madhehebu ya Makhalifa, na Tawhiid ya Sheikh Saduuq inawakilisha madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s.). Kabla hatujaendelea na kunukuu kutoka kila kimoja chao, tunadhani ni busara tukiwatambulisha hao waandishi ili kwamba ubora na vyeo vyao viwe vinaeleweka.
Ibn Khuzaimah Kama Anayotazamwa Na Madhehebu Ya Makhalifa
Wanazuoni wamemteua Ibn Khuzaimah kama: Imamul Aimmah (Imam wa Maimamu)

• Al-Hafidh al-Kabiir (mtunzaji mkuu wa elimu za Kiislamu – au mashuhuri miongoni mwa wale walioihifadhi Qur’ani kwa moyo)

• Al-Mujtahid al-Mutlaq (Mwana-Fiqh thabiti)

• Bahrul Uluum (Bahari ya elimu)

• Ra’sul Muhaddithin (kiongozi wa wasimulizi)

• Habr ul-Ulama al-Amiliin (mshauri wa wanazuoni waadilifu)

• Ka’batul Ulama (kitovu cha wasomi)
Muhammad Ibn Ishaq Khuzaimah Nisaburi:
Yeye alizaliwa mnamo mwaka wa 213 Hijiria na alifariki mwaka wa 311 Hijiria. Wanazuoni wengi wamesimulia hadithi kutoka kwake, ikiwa ni pamoja na waandishi wa Bukhari na Muslim. Inasemekana kwamba Ibn Khuzaimah kwa kulipa hisani alizikubali hadithi zilizosimuliwa na hawa wawili wa mwisho hapo juu.

Mbali na tasnifu ndogo ndogo zilizoandikwa katika kujibu maswali fulani, Ibn Khuzaimah ameandika vitabu vikubwa 140, ambavyo vinajumuisha pamoja na ile Sahih maarufu ya Ibn Khuzaimah. Baadhi ya Wanazuoni wanaiona Sahih yake kama ni bora na yenye kuzidi aula kuliko Sahih Bukhari na Sahih Muslim. Alikuwa ni mfuasi wa Shafi’i.

Ndani ya mjala huu mfupi, tumetegemea kwenye kitabu chake kiitwacho Tawhiid, kilichopitiwa kwa makini na Muhammad Khaliil Haras wa al- Azhar, Cairo na kuchapishwa na al-Azhar University Press – (Taasisi ya kupiga chapa ya Chuo Kikuu cha al-Azhar), Cairo, mnamo mwaka 1378 Hijiria.
Sheikh Saduuq Kama Anavyotazamwa Na Madhehebu Ya Ahlul-Bayt (A.S.)
Saduuq ni jina alilopewa Abu Ja’far Muhammad ibn Ali bin Husayn bin Babawayh Qummi. Yeye alifariki mnamo mwaka 381 Hijiria. Ni mwanazuoni mwenye heshima ya juu, asiyehitaji kutambulishwa. Ameandika takriban vitabu 200.

Katika mjadala huu, tumetegemea kwenye kitabu chake cha Tawhiid, kilichochapishwa Tehran mnamo mwaka 1381 Hijiria, kikapitiwa kwa tahaki- ki na Syed Hashim Husayni Tehrani.

Vitabu hivi viwili ndio vyanzo vyetu vikuu. Kwa nyongeza, tunarejea kwenye vitabu vingine maarufu vilevile kama vile Mlango wa Tawhiid ndani ya Sahih Bukhari, Mlango wa Iman kutoka Sahih Muslim. Na kwa upande wa madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s.), tutafanya marejeo kwenye Mlango wa Tawhiid kutoka kitabu Biharul Anwar cha Majlisi (aliyefariki mwaka 1111 Hijiria).
(A) Kutoka Madhehebu Ya Makhalifa
Hebu tuzichunguze hadithi mbili kutoka kwenye madhehebu hii:

1. Ibn Khuzaimah ndani ya Tawhiid, pamoja na Bukhari na Muslim wanasimulia kupitia kwa Abu Huraira kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema:

“Allah amemuumba Adam kwa mfano Wake Mwenyewe, futi sitini kwa urefu. Halafu Akamuamuru yeye kwenda mbele ya kikundi cha Malaika na kuwasalimia. ‘Wasikilize vizuri wakati wanapojibu maamkuzi yako, kwani hayo yatakuwa ndio maakuzi wewe na kizazi chako mtakayotu- mia,’ Allaha akasema.

“Hivyo Adamu akatii na akawaamkia hivi: ‘Assalamu Alaikum’ (Amani iwe juu yenu). Hao Malaika wakamjibu: ‘Assalamu Alaika wa Rahmatullah.’ (Amani iwe juu yako na Rehma za Mwenyezi Mungu), wakiongezea ‘Wa Rahmatullah.’

“Hivyo kila mmoja anayeingia peponi atakuwa katika mfano wa umbile la Adam. Wanadamu walipunguzwa tarat- ibu katika urefu kiasi muda ulivyopita, hadi kufikia kimo walichonacho leo hii.”

2. Abu Huraira anasimulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema:

“Wakati wowote ule mtu anapohusika kwenye ugomvi au mapigano dhidi ndugu yake, mtu anapaswa kujiepusha kumpiga kwenye uso. Hii ni kwa sababu Mwenyezi Mungu alimuumba Adam katika mfano Wake Mwenyewe.”1

Hizi ni hadith kutoka kwa Abu Huraira. Hebu sasa tuzilinganishe na hadithi zilizosimuliwa na Madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s.) ili picha ipate kukamilika.
(B) Ahlul-Bayt (A.S.) Wanauelezea Ukweli Hasa
1. Husayn bin Khalid anasema:

“Nilimuuliza Imam Ridha (a.s.) kuhusu ile hadithi mashuhuri ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwamba Mwenyezi Mungu alimuumba Adam katika mfano Wake Mwenyewe. Yeye akasema: ‘Walaaniwe wale wasimuliaji wadanganyifu ambao wameiacha ile sehhemu ya kwanza ya hadithi hii.’ Kisha akaelezea: Wakati mmoja Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alikuwa anapita pale aliposikia watu wawili wakitukanana wenyewe kwa wenyewe. Alimsikia mmoja wao akisema kwamba: ‘Mwenyezi Mungu auchukize na kuufedhehesha uso wako, na uso ambao unafanana na wako.’

Wakati huo, Mtukufu Mtume akasimama na kuwaonya kwa kusema: ‘Usitamke maneno kama hayo kumwambia ndugu yako. Kwani Mwenyezi Mungu amemuumba Adamu (pia) kwa mfano wake. (Akimaanisha kwamba Adamu vilevile alifanana na huyo ndugu yake).”

2. Katika hadithi nyingine iliyosimuliwa na Abul Ward kwa Thamamah kutoka kwa Amirul Mu’minin Ali ibn Abi Talib (a.s.) tunasoma kama ifuatavyo:

“Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimsikia mtu mmoja anamtukana mwingine akisema kwamba: ‘Mwenyezi Mungu auchukize na kuufedhehesha uso wako, na uso unaofanana na wako.’ Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: ‘Nyamaza kimya! Usisema maneno kama hayo! Kwani Mwenyezi Mungu alimuumba Adamu katika mfano wake.’”

3. Licha ya hadithi hizi mbili, hebu natuchunguze nyingine moja zaidi, ambayo itatupa maoni ya jumla juu ya jinsi Maimamu wa Ahlul-Bayt (a.s.) walivyoziangalia imani za uhusishaji viungo kwa Allah (anthropomorphism).

Saduuq katika kitabu chake cha Tawhiid anasema:

“Imam Musa ibn Ja’far (a.s.) alipokea barua ambayo ndani yake mtu mmoja alikuwa akitafuta ubainisho kuhusu ile imani inayohusu mwili na mfano wa Mwenyezi Mungu. Imam (a.s.) akamjibu: ‘Sifa zote zimwendee Allah swt! Hakuna chochote kile kinachofanana na Yeye – hakuna mwili na wala hakuna mfano.’”
(C) Uchunguzi Na Ulinganishaji
Tunapotafakari juu ya hadithi hizi na kuzilinganisha, tunakuta kwamba Abu Huraira katika hadithi zake mbili ameweka nyongeza mbili na ameacha jambo moja.
1. Lile Ambalo Limeachwa
Wakati Abu Huraira anaposimulia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), yeye analiacha lile tukio ambamo Mtume alikabiliana na watu wawili waliohusika katika lugha chafu na matusi, halafu akamuonya mmoja wao asiizungumzie vibaya sura ya mwanadamu kwa sababu ilifanana na ile ya Adam. Kwa hakika jambo lililoachwa hapa ni muhimu sana, kwa sababu maelezo ya Abu Huraira yanatoa taswira kwamba kile kiwakilishi nomino “yake” kinarejea kwa Mwenyezi Mungu, ambapo kwa kweli kinarejea kwa yule mtu mwenyewe.

Abu Huraira anaweza kuwa ameacha ile sehemu muhimu ya hadithi hiyo kwa sababu:-

(a) Alikuwa akihifadhi hadithi kichwani, kwa vile alivyokuwa hawezi kusoma wala kuandika. Na hata kama angekuwa anaweza, asingeruhusiwa na hao Makhalifa ambao walikuwa wamewakataza Waislamu kutunza kumbukumbu ya maandishi ya hadithi za Mtume, hadi mwisho wa karne ya kwanza ya Hijiria.

(b) Abu Huraira alikuwa ameshawishiwa sana na Ka’b al-Ahbar ambaye alieneza hadithi fupi zilizopotoshwa kutoka kwenye Taurati miongoni mwa Waislamu. Ni dhahiri, athari za kile alichokisimulia Ka’b zilikuwa bado zina nguvu mpya kwenye akili ya Abu Huraira, kwa sababu kimekuja takriban miaka ishirini baada ya kukisikia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).

(c) Huenda kosa lilikuwa upande wa wasimulizi wa siku za baadae ambao walizinakili simulizi za Ka’b zilizohusishwa kwa makosa kwa Abu Huraira. Vyovyote vile hali iwavyo, matokeo yake yanabakia vile vile, bila kubadilika.
2. Nyongeza Mbili
(a) Katika hadithi ya kwanza, Abu Huraira anayahusisha maelezo yafu- atayo kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.):-

“Wakati wowote mtu anaposhiriki katika ugomvi dhidi ya ndugu yake, huyo ajiepushe na kumpiga usoni mwake…..”

Inawezekana hii ni hadithi mbadala iliyobuniwa na Abu Huraira, mahala pa ule uachwaji tulioutaja hapo juu.

(b) Katika hadithi nyingine, Abu Huraira anazungumzia juu ya urefu wa Adam:-

“Mwenyezi Mungu amemuumba Adam katika mfano Wake, kwa urefu wa futi sitini…..”

Ni dhahiri, maelezo kama haya si yenye ukweli, wala hayapatani na uchunguzi wa kielimu.

Mtu anaweza kuona kwa urahisi kwamba hadithi zilizosimuliwa kutoka kwa Abu Huraira zinabeba kufanana kunakoafikiana sana na zile hadithi kutoka kitabu cha Mwanzo ndani ya Agano la Kale.

Kwa kuzichezea zile hadithi za kweli za Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), kuingiza maneno hapa na pale, kukata hapa na pale, Abu Huraira na wanaofanana naye wamefanikiwa kutoa usadikikaji kwenye hadithi za uzushi kutoka kwenye Taurati. Hizi, hivyo basi, ndio hadithi Israiliyyat, ambazo zimefanya uingiliaji wa kuhuzunisha kwenye hadithi na imani za Kiislamu.

Madhehebu za Makhalifa zimezimeza, kuanzia ndoano, kamba yake na chambo chake, kwa sababu majina maarufu kama yale ya akina Abu Huraira yameambatanishwa nazo.

Matokeo yake yamekuwa kwamba mahali popote pale maneno kama “uso” yanapotokea kuhusiana na Mwenyezi Mungu ndani ya Qur’ani Tukufu, wao wamesisitiza juu ya maana halisi. Kwao wao, sifa zote za kibinadamu, kanuni na maumbo vinaweza kutumika kwa Mwenyezi Mungu! Tutalijadili somo hili katika milango inayofuata Inshallah.
________________________
1. Sahih Muslim, uk. 2016, 2017
1. “Uso” Wa Mwenyezi Mungu Kama Unavyoeleweka Kwa Madhehebu Ya Makhalifa:
Ibn Khuzaimah katika kitabu chake kiitwacho Tawhiid anaandika katika ukurasa wake wa kumi. Mlango unaothibitisha uso wa Mwenyezi Mungu, ambao Yeye Mwenyewe ameueleza kama wenye kujaa utukufu na heshima katika Ayah ifuatayo:
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ {27}
“Na itabaki dhati ya Mola Wako, Mwenye utukufu na Heshima.” (Ar- Rahmaan; 55: 27)
Na Amethibitisha vilevile kwamba Uso Wake hautatoweka kamwe:
ۚ كُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ إِلَّا وَجْهَهُ ۚ لَهُ الْحُكْمُ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ {88}
“…….. Kila kitu kitaangamia isipokuwa Uso Wake, hukumu iko Kwake, na kwake Yeye mtarejeshwa.” (Al-Qasas; 28: 88)
Baada ya hapo, Ibn Khuzaimah anatafuta uhakikisho mwingine zaidi kuto- ka kwenye Ayah nyingine za Qur’ani Tukufu, na kisha anasema:

“Kwa hiyo Mwenyezi Mungu amethibitisha kabisa kwamba Yeye anao uso, ameuelezea kama ni Wenye Utukufu na Heshima, na amehukumu kwamba uso huo utadumu milele, bila kutoweka kamwe……”

Katika maelezo yake ya kumalizia, anaongezea kusema:

“Kila kile ambacho Mwenyezi Mungu amejithibitishia yeye Mwenyewe, sisi pia tunakithibitisha. Lakini uso Wake sio kama uso wowote wa kiumbe chochote.”

Katika ukurasa wa kumi na moja wa kitabu hicho hicho, Ibn Khuzaimah anasimulia hadithi 14 kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ambamo neno “uso” limetajwa, na anaegemeza madai yake juu ya hadithi hizo. Kwa mfano, pale Mtume anapoomba du’a kwa kusema:

“Ninaomba hifadhi kwa Uso Wako wenye Rehma.”

Ibn Khuzaimah anaona kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alilitaja neno uso kwa maana yake halisi. Kwa maneno mengine, anasisitiza kwamba “uso” ni sehemu ya mwili wa Mwenyezi Mungu, sawa sawa na ule wa mwanadamu au mnyama mwingine.

Sasa hebu tuangalie kile ambacho Ahlul-Bayt (a.s.) walichokieleza katika hadithi zao:
2. “Uso” – Kama Ulivyoelezewa Na Ahlul-Bayt (A.S.)
Kama dibaji, hebu natushughulike na hadithi kutoka kwa Amirul- Mu’minin, Ali bin Abi Talib (a.s.) ambamo aliweka kanuni kwa ajili ya uelewa wa Ayah za Qur’ani Tukufu, hususan zile zinazohusika na sifa za ki-mungu.

Mtu mmoja alipeleka swali lake kwa Ali bin Abi Talib (a.s.), akinukuu baadhi ya Ayah kutoka kwenye Qur’ani Tukufu, kutoa vipingamizi vyake. Miongoni mwa hizo tunachagua hizi mbili zifuatazo:

Maana hasa ya maneno yenyewe ya Ayah hizi mbili ni:
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا {22}
“(NakatikahiyoSikuyaKiyama)NaakajaMola WakonaMalaika safukwasafu…”
(Al-Fajr;89:22)
هَلْ يَنْظُرُونَ إِلَّا أَنْ تَأْتِيَهُمُ الْمَلَائِكَةُ أَوْ يَأْتِيَ رَبُّكَ أَوْ يَأْتِيَ بَعْضُ آيَاتِ رَبِّكَ {158}
“HawangojiilawawafikieMalaikaauMola Wakoafike,auzifike baadhiyadalilizaMolaWako………” (Al-An’aam;6:158)
Swali lililoletwa ni kama Mwenyezi Mungu Mwenyewe atakuja kutokeza hiyo Siku ya Kiyama, kwa dhahiri kama ilivyowasilishwa na Ayah hizo.
Imam Ali (a.s.) alielezea hivi:
“Chochote kile ambacho Mwenyezi Mungu, Aliye Mkuu, amekidhihirisha ndani ya Ayah, ni kweli kabisa; isipokuwa kwamba kuja kwake sio sawa na kuja kwa viumbe Vyake. Nimekushauri hapo mapema kwamba sehemu fulani za Qur’ani Tukufu lazima zisitafsiriwe kwa maana halisi ya maneno; badala yake unapaswa kuelewa ile maana ya ki- istiari. Neno Allah sio kama neno la kibinadamu, na tendo Lake sio kama tendo la kibinadamu. Ili kuiweka hoja yangu ieleweke vizuri, nitakupa mifano kutoka kwenye Qur’ani Tukufu, ili Inshallah, uelewaji wako wa Qur’ani utakuwa wa hakika na wa sawasawa. Qur’ani inamsimulia Nabii Ibrahim akisema:
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهْدِينِ {99}
“NakwendakwaMola Wangu,yeyendiyeatakayeniongoza.”(As- Saffat;37:99)
Hapa, “kwenda kwa Mola” hakuna maana ya kutembea hadi Kwake kwa msaada wa miguu. Ina maana ya kurejea Kwake, kwa uimara na ukweli, kupitia ibada, na kutafuta ukaribu Naye. Je, unaweza kuona tofauti baina ya maana yake halisi na ile maana yenyewe iliyowasilishwa na istiari? Halafu tena, maana halisi ya Ayah zifuatazo inaweza kuwa:
وَأَنْزَلَ لَكُمْ مِنَ الْأَنْعَامِ ثَمَانِيَةَ أَزْوَاجٍ ۚ {6}
“…na akakushushieni wanyama, (kwa jozi) wanane madume na majike…”(Az-Zumar;39:6)
وَأَنْزَلْنَا الْحَدِيدَ فِيهِ بَأْسٌ شَدِيدٌ {25}
“….Natumekishushachumachenyenguvunyingi…”(Al-Hadiid;57:25)
Sasa kama ungekuwa utegemee kwenye maana halisi, ungeona kwamba zile jozi nane za ng’ombe na kile chuma “vilishushwa” kutoka juu mbinguni. Lakini bila shaka haikumaanishwa hivyo. Maneno hayo hapa yanamaanisha “tuliumba,” au “Aliumba.”1
Ali ibn Abi Talib (a.s.) ametufundisha kanuni mbili muhimu juu ya kuele- wa Sifa na kazi za Mungu. Kwanza, kazi na matendo ya Mwenyezi Mungu haviwezi kulinganishwa na kazi na matendo yetu. Wakati Mwenyezi Mungu ndani ya Qur’ani Tukufu anaposema:
قَدْ سَمِعَ اللَّهُ {1}
“HakikaMwenyeziMunguniMwenyekusikia…”(Al-Mujadilah;58:1),
Haifananishwa na kusikia kwa mwanadamu, mnyama au kiumbe chochote. Sisi tunasikia kwa msaada wa masikio yetu. Kusikia kwa Mwenyezi Mungu hakuashirii kitu kama hicho.
Mwenyezi Mungu anasema:
قَالَ يَا إِبْلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَنْ تَسْجُدَ لِمَا خَلَقْتُ بِيَدَيَّ {75}
“Akasema: Ewe Iblis, ni nini kimekuzuia kumtii yule niliyemuumba kwamikonoyangu?
(As-Swad;38:75)
Mwanadamu anaweza akasema vile vile kwamba ameumba kitu kwa mikono yake. Lakini yote yana maana tofauti. Mwenyezi Mungu hana viungo, wala hahitaji mikono.
Mwenyezi Mungu alimdhihirishia Nabii Musa (a.s.) hivi:
قَالَ لَا تَخَافَا ۖ إِنَّنِي مَعَكُمَا أَسْمَعُ وَأَرَىٰ {46}
“Msiogope, bila shaka mimi niko pamoja nanyi, ninasikia na ninaona.”(At-Twaha;20:46)
Kuwa pamoja na mtu kuna maana tofauti wakati inapotumika kwetu sisi. Wakati Mwenyezi Mungu yuko “pamoja” na mtu, haiashirii kuwa pamoja kimwili au kwa ukaribu.

Pili, Amirul Mu’minin, Ali bin Abu Talib (a.s.) alisema kwamba ilikuwa ni lazima kuyaelewa matumizi halisi na yale ya kiistiari vilevile ya maneno ndani ya Qur’ani Tukufu, kabla mtu hajaanza kutafsiri au kusherehesha. Alitoa mifano miwili kutoka ndani ya Qur’ani ili kuielezea hoja yake.

Kwa kweli, tunapokaa kusoma kazi ya sanaa ya fasihi au maandishi, katika lugha yoyote ile iwayo, tunatakiwa kuwa wenye kufahamu vizuri zile tamathali za semi, matumizi tofauti ya maneno na kadhalika. Kwa kutegemea kanuni hii iliyoenea pote, hebu sasa tuangalie jinsi madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s.) inavyoushughulikia huu mtajo “uso” wa Mwenyezi Mungu.

Abu Hamza alimuuliza Imam Muhammad Baqir (a.s.) kuhusu maana ya Ayah hii:-

“Kila kitu chenye uhai kitatoweka isipokuwa Uso Wake Mwenyewe.”

Imam alimjibu hivi:

“Hivi wao wanadhania kwamba Mwenyezi Mungu anao uso na kwamba kila mtu atakufa na kutoweka bali Uso Wake? Mwenyezi Mungu yuko mbali na kuwa mwenye uso! Maana halisi ya Ayah hii ni kwamba kila kitu kitat

Share this article

Comments 0

Your comment

Comment description

Latest Post

Most Reviews

MOST READ