Rafed English

Je Kufunga Mikono

Je Kufunga Mikono by : Sheikh Jafar Subhani

 

Kitabu kilichoko mikononi mwako, ni tarjuma ya kitabu cha Kiarabu kwa jina la: "Al-Qabdh Baina ‘l-Bid’ah wa‘s-Sunnah" Sisi tumekiita: "Je, Kufunga Mikono Ni Bidaa au Sunna? Kwenye Sala." Kitabu hiki, "Je, Kufunga Mikono Ni Bidaa au Sunna? Kwenye Sala" ni matokea ya utafiti wa kielimu uliofanywa na Mwanachuoni wa Kiislamu, Jafar Subhany. Sheria ya Kiislamu ni ya kipekee kwa kuwa inahusika na kila jambo huku ikiweka utatuzi wa matatizo yote yanayompata mwanadamu katika sekta zote za maisha yake.

Wanachouni wa Kiislamu kama kawaida ya wanadamu wamehitilafiana katika hukumu ndogo ndogo katika matendo ya ibada, lakini kama ilivyo, tofauti ndogo kati ya wanachuo kwa wafuasi inakuwa ni mlima wa tofauti na kusababisha zongo lisilo na maana. Mambo ambayo wanachuo wetu wamehitilafiana si katika asili au misingi ya dini, na isitoshe ni mambo machache sana ukilinganisha na yale tunayokubaliana nayo.

Kufunga mikono kwenye Sala ni suala ambalo wanachuo wetu wamehitalifiana; ndani ya madhehebu moja na kati ya madhehebu. Kwa hiyo hii sio hitilafu ya madhehebu, bali ni hitilafi ya wanachuo wa madhehebu zote wamehitilafiana juu ya suala hili. Lakini bahati mbaya Waislamu wengi hawaitambui hitilafu hii kwa usahihi na hivyo kuongelea katika dhana na kusababisha mizozo isiyokuwa na maana. Kutokana na hali hii Sheikh wetu, Jafar Subhani amelifanyia utafiti wa kina suala hili na kuweka wazi asaili ya hitilafu hii, kisha akamuachia msomaji mwenyewe kutoa uamuzi.

Kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote. Kutokana na ukweli huu, Taasisi yetu ya 'Al-Itrah Foundation' imeona ikitoe kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili, kwa madhumuni yake yale yale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili, ili kuongeza ujuzi wao katika masuala ya dini na ya kijamii.

Tunamshukuru ndugu yetu, Hemedi Lubumba Selemani (Lipumba) kwa kukubali jukumu hili la kukifanyia tarjuma kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwa kitabu hiki.
Mchapishaji:
Al-Itrah Foundation
S. L. P. 19701, Dar-es-Salaam,
Tanzania.
Kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu mlezi wa ulimwen- gu. Rehma na Amani zimfikie mbora wa viumbe na hitimisho la mitume Wake, pia kizazi chake kitakatifu ambacho ndio kasha la elimu yake na hazina ya mafunzo yake. Hakika Uislamu ni imani na sheria. Imani ni kuamini Mwenyezi Mungu, mitume Wake na Siku ya Mwisho. Na sheria ni huku- mu za Mwenyezi Mungu ambazo zina jukumu la kumpa mwanadamu maisha bora na kumuhakikishia wema wa dunia na akhera.

Sheria ya Kiislamu ni ya kipekee kwa kuwa inahusika na kila jambo huku ikiweka utatuzi wa matatizo yote yanayompata mwanadamu katika sekta zote za maisha yake, hivyo Mwenyezi Mungu akasema:

الْيَوْمَ يَئِسَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ دِينِكُمْ فَلَا تَخْشَوْهُمْ وَاخْشَوْنِ ۚ الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ{3}
“Leo nimewakamilishieni dini yenu na kuwatimizieni neema Yangu na nimewapendeleeni Uislamu uwe dini yenu.” ( 5:3 ).

Isipokuwa kuna masuala madogo madogo ambayo wanazuoni wa sheria wamehitilafiana kwa sababu ya kutofautiana kwao kuhusu riwaya ambazo zimenasibishwa kwa Mtume. Jambo ambalo limepelekea kutofautiana kuhusu masuala madodo madogo ya sheria.

Kwa kuwa ukweli hutokana na utafiti basi hakika katika mtiririko wa masomo haya tumejaribu kuliweka sala hili juu ya meza ya utafiti, kwani huenda ikawa ndio njia ya kuunganisha mtazamo na kusogeza hatua katika uwanja huu. Kwani tofauti iliyopo si katika asili na misingi ya dini hata ipelekee kuwa na uadui na chuki bali tofauti iliyopo ni kuhusu riwaya zilizonasi- bishwa na Mtume, nalo ni jambo dogo ukilinganisha na mambo mengi ambayo tunaafikiana kati ya madhehebu za Kiislamu. Na muongozo wetu katika njia hii ni kauli ya Mwenyezi Mungu:

وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا ۚ وَاذْكُرُوا نِعْمَتَ اللَّهِ عَلَيْكُمْ إِذْ كُنْتُمْ أَعْدَاءً فَأَلَّفَ بَيْنَ قُلُوبِكُمْ فَأَصْبَحْتُمْ بِنِعْمَتِهِ إِخْوَانًا{103}

“Na shikamaneni katika kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msifarakiane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu, mlipokuwa maadui na akaziungan- isha nyoyo zenu, hivyo kwa neema Zake mkawa ndugu.” (3:103)
Sheikh Jafar Subhani
Tasisi ya Imam Sadiq (a.s.)
Qum
Hakika kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ni jambo mashuhuri lililohimizwa na wanafiqihi wa kisunni.

Wafuasi wa Hanafiy wamesema: “Hakika kufunga mikono ni Sunna na wala si wajibu, na lililo bora kwa mwanaume ni aweke tumbo la kiganja chake cha kulia juu ya mgongo wa kiganja chake cha kushoto chini ya kitovu chake, na kwa mwanamke aweke mikono yake juu ya kifua chake.”

Wafuasi wa Shafiy wamesema: “Ni Sunna kwa mwanamume na mwanamke. Na lililo bora kwa mwanaume ni kuweka tumbo la kiganja chake cha kulia juu ya mgongo wa kiganja chake cha kushoto chini ya kifua na juu ya kitovu upande wa kushoto.” Wafuasi wa Hambal wamesema: “Hakika ni Sunna, na bora ni aweke kiganja cha kulia juu ya mgongo wa kiganja cha kushoto, aweke chini ya kitovu.”

Wafuasi wa Malik wamekwenda kinyume na hao, hivyo wakasema: “Ni Sunna kuachia mikono ndani ya Sala ya faradhi.”

Na kuna kundi lililosema hivyo kabla yao, kati yao ni Abdullah bin Zubeiri, Saidi bin Al-Musayyabu, Saidi bin Jubairi, Atau, Ibnu Jariji, An-Nakhaiy, Hasani Al-Basriy, Ibnu Sirini na kundi la wanafiqihi. Na ndio msimamo wa Alay-thu bin Saad, isipokuwa yeye kasema: “Isipokuwa atakaporefusha kisimamo na akawa amechoka basi itambidi kufunga mikono.”

Na kauli iliyonukuliwa toka kwa Imam Al-Awzaiy ni hiyari kati ya kufunga mikono au kuachia.1

Mufti wa madhehebu ya Malik huko Ad-Dayaru Al-Hijaziya, Muhammad Abidu ameona kuwa kuachia mikono na kufunga ni Sunna toka kwa Mtume na kuwa muumini anaporefusha kisimamo ilihali kaachia mikono na akachoka basi anafunga mikono. Akasema kuwa kuachia mikono ni asili na kufunga ni tawi. 2

Ama Shia Imamiyah mashuhuri kwao ni kuwa ni haramu na hubatilisha Sala, na ni wachache sana wamesema ni makuruhu, kama vile Al-Halbiy ndani ya Al-Kafiy 3
Kufunga Mikono Ni Bidaa Iliyozushwa
Hakika kufunga mikono ni bidaa iliyozushwa iliyodhihiri baada ya kufariki Mtume mtukufu. Na tegemezi letu katika kuthibitisha hilo ni Hadithi mbili sahihi:

Moja kati ya hizo imepokewa kwa njia za Masunni, na nyingine imepokewa kwa njia ya Shia Imamiyah. Hadithi hizo mbili ni dalili yakinifu zinazothibitisha kuwa mwenendo wa Mtume na kizazi chake kitakasifu ulikuwa ni kuachia mikono ndani ya Sala, na kuwa kufunga mikono ni bidaa iliyoanzishwa baada ya kifo cha Mtume.
A: Hadithi Ya Abu Humeidi As-Saidiyu
Wanahadithi wengi zaidi ya mmoja wamepokea Hadithi ya Abu Humeidi As-Saidiyu, hapa tutaitaja kwa mujibu wa maele- zo ya Al-Bayhaqi.

Amesema: Ametupa habari Abu Abdillah Al- Hafidhu: Akasema Abu Humeidi As-Saidiyu: “Mimi ni mjuzi zaidi wa Sala ya Mtume wa Mwenyezi Mungu.”

Wakasema: “Kwa nini? Ilihali haukumfuata mara nyingi zaidi yetu wala hukutangulia kuwa nae kabla yetu?” Akasema:

“Ndio.” Wakasema: “Tuelezee.”

Akasema: “Mtume alipokuwa akisimama kuswali alikuwa akiinua mikono yake mpaka iwe sawa na mabega yake, kisha anatoa takbira mpaka kila kiungo kitulie sehemu yake huku akiwa amenyooka. Kisha anasoma, kisha anatoa takbira na kuinua mikono yake mpaka iwe sawa na mabega.

Kisha anarukuu na kuweka viganja vyake juu ya magoti yake, kisha ananyooka bila kunyanyua kichwa chake wala kukilaza. Kisha anainua kichwa chake na kusema: (Mwenyezi Mungu amemsikia anaemuhimidi). Kisha anainua mikono yake mpaka iwe sawa na mabega yake mpaka kila kiungo kirudi sehemu yake akiwa amenyooka. Kisha anasema: Allahu Akbar.

Kisha anaporomoka ardhini anaweka mikono yake pembeni mwake. Kisha anainua kichwa chake anakunja mguu wake wa kushoto na kuukalia. Na anaposujudu hufungua vidole vya miguu yake. Kisha anarudi kusujudu, kisha anainua kichwa na kusema: Allahu Akbar. Kisha anakunja mguu wake na kuukalia akiwa amenyooka mpaka kila mfupa urudi au utulie sehemu yake.

Kisha anafanya hivyo hivyo katika rakaa nyingine. Kisha anaposimama toka kwenye rakaa mbili hutoa takbira na kuinua mikono yake mpaka iwe sawa na mabega yake kama alivyofanya na kutoa takbira mwanzo wa Sala yake.

Kisha anafanya hivyo hivyo katika Sala yake yote mpaka anapofika katika sijida ya kutoa Salamu hapo huchelewesha mguu wake wa kushoto na kukaa mkao wa Tawaruku upande wake wa kushoto.”

Hapo wote wakasema: “Amesema kweli, hivyo ndivyo alivyokuwa akiswali Mtume wa Mwenyezi Mungu.”4

Na kinachoweka wazi usahihi wa kutegemea Hadithi hii ni mambo yafuatayo:

Kitendo cha maswahaba wakubwa kumsadikisha Abu Humeidi5 kinaonyesha nguvu ya Hadithi, na kufaa kuitanguliza kabla ya dalili nyingine.

Hakika yeye katoa wasifu wa Sala kuanzia faradhi zake hadi Sunna zake wala hakutaja kufunga mikono, na wala maswahaba hawakumkosoa au kutaja kitu kinyume na alivyosema, ili- hali walikuwa na hamu ya kufanya hivyo kwa sababu mwanzo hawakukubali kuwa yeye ni mjuzi wa Sala ya Mtume kuliko wao. Lakini pamoja na hali hiyo wote walisema:

Umesema kweli hivyo ndivyo alivyokuwa akiswali Mtume. Na iko mbali sana dhana ya kuwa wao wote walisahau ilihali walikuwa makumi na wako katika mazingira ya kukumbuka.

Asili katika kuweka mikono ni kunyoosha, kwa sababu ndio maumbile, na Hadithi imeonyesha hilo.

Huwezi kudai kuwa Hadithi hii imekuja bila sharti lakini kuna Hadithi nyingine zimekuja kuiwekea sharti. Haiwezekani hivyo kwa sababu katoa wasifu na kuorodhesha faradhi zote za Sala na Sunna zake na vyote vinavyokamilisha umbile la Sala, ilihali akiwa katika kuonyesha na kubainisha mafunzo, hivyo kutotoa baadhi ya sifa ni kufanya khiyana. Na jambo hilo la khiyana liko mbali na yeye bali na wao.

Baadhi ya maswahaba waliokuwepo kati ya wale waliopokea Hadithi za kukunja mikono hawajapinga (Maelezo yake). Hivyo ikaonyesha kuwa kukunja mikono ni sheria iliyoisha muda wake, au kwa uchache inaruhusiwa kwa yule aliyerefusha kisimamo ndani ya Sala yake, na si miongoni mwa Sunna za Sala kama ilivyo kwa madhehebu ya Alaythu bin Saad na Al-Awzaiy na Malik6

Ibnu Rushdi amesema: “Na sababu ya kutofautiana kwao ni kuwa zimekuja riwaya thabiti zilizonukuu wasifu wa Sala ya Mtume lakini haijanukuliwa kuwa alikuwa akiweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto.”7

Hapa limebakia swali moja nalo ni kuwa ni mashuhuri kuwa wafuasi wa Malik hawafungi mikono na Imam wao alikataa jambo hilo.

Akasema ndani ya Al-Mudawanati: “Malik amekataa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala na akasema:

Silijui jambo hilo ndani ya faradhi, ilihali yeye mwenyewe ndani ya kitabu chake Al-Muwata amepokea Hadithi ya kukunja mikono, kwani amepokea toka kwa Sahl bin Saad kama alivyopokea kwa kuvushwa toka kwa Abdul- Karimu ibnu Abu Al-Makhariqu Al-Basriy kuwa alisema: “Miongoni mwa maneno ya unabii ni: Kama hauna haya tenda lolote unalotaka, na kuweka mikono, mmoja juu ya mwingine ndani ya Sala, kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto, na kuharakisha kufuturu na kuchelewesha kula daku.”8

Nasema: Hakika kitabu Al-Muwata ni kitabu cha riwaya, hivyo Imam anaweza kuipokea na wala asitoe fat’wa kufata riwaya hiyo. Ndio maana utaona ndani ya Al-Mudawanat kuna fat’wa zinazopingana na riwaya alizozipokea ndani ya Al-Muwatau.

Na atakayefuatilia fiqhi yake ataona kuwa kuna tofauti kubwa kati ya riwaya zake zilizomo ndani ya Al-Muwatau na fat’wa zake zilizoandikwa.

Dr. Abdul-Hamidi ndani ya ujumbe wake mfupi alioandika kuhusu kuachia mikono ameashiria sehemu hizo za tofauti.9

Vyovyote vile ni kuwa kauli yake (Silijui jambo hilo ndani ya faradhi) ni dalili ya wazi kuwa matendo ya watu wa mji wake ni tofauti na kitendo hicho, kwani kauli (Silijui jambo hilo ndani ya faradhi) maana yake silijui jambo hilo kutoka kwenye matendo ya Maimam ambao ndio waliyokuja baada ya maswahaba na wakachukua elimu toka kwa maswahaba.

Hii ndio Hadithi ambayo imesimama kubainisha namna ya Sala ya Mtume, nayo imepokewa kwa njia ya Masunni, na tayari umeshajua hoja zake. Na sasa ni riwaya iliyopokewa na Shia Imamiyah.
B: Hadithi Ya Hammadi Bin Isa
Hammadi bin Isa amepokea toka kwa Imam Sadiqi (a.s.) kuwa alisema: “Ni jambo baya sana mtu kutimiza miaka sitini au sabini ilihali hajawahi kuswali hata Sala moja kwa ukamilifu. Hammadi akasema: Ukanifikia udhalili ndani ya nafsi yangu, nikasema: Niko chini yako, nifundishe Sala.”

Akasimama Abu Abdillah akiwa kaelekea kibla ilihali kany- ooka, akanyoosha mikono yake yote juu ya mapaja yake ilihali kabana vidole vyake na kasogeza nyayo zake mpaka kiwango cha uwazi wa vidole vitatu.

Akaelekeza kibla vidole vya miguu yake kwa unyenyekevu, na wala hakuvitoa kwenye kibla. Akasema: Allahu Akbar, kisha akasoma Al-Hamdu na Qul-huwa llahu ahadu. Kisha akasubiri kidogo kwa kiwango cha kuvuta pumzi ilihali akiwa kasimama.

Kisha akasema: Allahu Akbar akiwa amesimama, kisha akarukuu na kujaza viganja vyake kwenye magoti yaliyoachana na akarudisha magoti yake nyuma mpaka mgongo wake ukanyooka kiasi kwamba hata kama tone la maji au mafuta lingedondoka juu ya mgongo wake basi lingekaa. Akaendelea kunyoosha mgongo ilihali magoti yake kayarudisha nyuma, akanyoosha mbele shingo yake huku kafumba macho yake.

Kisha akamsabihi Mwenyezi Mungu akasema: Ametakasika Mola Wangu Mtukufu na kila sifa njema ni Zake. Kisha akasimama akiwa kanyooka na alipotulia akasema: Mwenyezi Mungu kamsikia aliyemuhimidi.

Kisha akatoa takbira ilihali kasimama. Akainua mikono yake mkabala na uso wake na kusujudu, akaweka mikono yake aridhini kabla ya magoti yake na kusema mara tatu:

Ametakasika Mola Wangu Mtukufu na kila sifa njema ni zake.

Wala hakuweka sehemu ya mwili wake juu ya sehemu nyingine ya mwili wake. Akasujudu kutumia viungo nane: Bapa la uso, viganja viwili, macho ya magoti yake, vichwa vya vidole gumba vyake na pua. Hivi viungo saba ni lazima na pua ni Sunna, nayo ni kwa ajili ya kujidhalilisha.

Kisha akainua kichwa chake toka sijida, na alipokaa sawa akasema: Allahu akbar kisha akakaa kwa kulalia upande wake wa kushoto, akawa ameweka mgongo wa nyayo yake ya kulia juu ya nyayo yake ya kushoto. Akasema: Namuomba Mola wangu magh’fira na ninatubu kwake.

Kisha akatoa takbira ilihali kakaa. Akasujudu sijida ya pili, akasema kama alivyosema katika sijida ya kwanza. Wala hakutumia sehemu ya mwili wake kuusaidia mwili wake katika sijida yake na rukuu yake. Wala hakuweka dhiraa zake juu ya ardhi.

Hivyo akaswali rakaa mbili kwa namna hii. Kisha akasema:

Ewe Hammadi, hivi ndivyo uswali wala usigeuke wala usicheze kwa mikono yako na miguu yako wala usiteme mate kushotoni mwako au kuliani au mbele yako.”10

Unaona kuwa riwaya hizi mbili zinabainisha namna ya Sala waliyofaradhishiwa watu, na ndani ya maelezo hayo hamna ishara yoyote inayogusia kufunga mikono kwa vigawanyo vyake tofauti.

Laiti ingekuwa ni Sunna basi Imam asingeacha kubainisha kwa sababu kwa kitendo chake anatujengea hali halisi ya Sala ya Mtume kwa sababu kachukua toka kwa baba yake Imam Al- Baqir na yeye kachukua toka kwa baba zake toka kwa kiongozi wa waumini Imam Ali toka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).

Hivyo kufunga mikono ndani ya Sala ni bidaa, kwa sababu ni kupandikiza jambo ndani ya sheria ilihali lenyewe si katika sheria.
Dalili Zinazosema Kuwa Kufunga Mikono Ndani Ya Sala Ni Lazima
Kisha hakika anayeruhusu kufunga mikono ana dalili, nasi tutazichambua.

Hakika dalili zote zinazosihi kutolewa kuthibitisha kuwa kufunga mikono ndani ya Sala ni Sunna hazizidi riwaya tatu:11

1. Hadithi ya Sahl bin Saad. Kaipokea Bukhari.

2. Hadithi ya Wailu bin Hajar kaipokea Muslim na kainukuu Al- Bayhaqiy kwa njia tatu.

3. Hadithi ya Abdallah bin Mas’ud kaipokea Al-Bayhaqiy ndani ya Sunan yake na vitabu vingine.

Ufuatao ni uchambuzi wa kila Hadithi: Hadithi ya Sahl bin Saad.

Bukhari amepokea toka kwa Abu Hazimu toka kwa Sahl bin Saad amesema: Watu walikuwa wakiamrisha mtu aweke mkono wa kulia juu ya dhiraa yake ya kushoto ndani ya Sala. Abu Hazimu akasema: Silijui jambo hili, labda kama hilo litanasibishwa na Mtume.12 Ismail13 amesema: “Hilo litanasibishwa, hajasema atanasibisha.”

Riwaya imebeba jukumu la kubainisha namna ya kufunga mikono, isipokuwa baada ya njia yake ya upokezi kukubalika tatizo linabakia kwenye hoja yake.

Wala riwaya haionyeshi Sunna ya kufunga mikono. Hilo ni kwa vigezo viwili:

Kwanza: Laiti kama Mtukufu Mtume angekuwa ndio muamrishaji wa kufunga mikono basi ni nini maana ya kauli “Watu walikuwa wakiamrisha” Hivi haikuwa ni sahihi kusema Mtume alikuwa akiamrisha? Hivi huoni kuwa hii ni dalili kuwa hukumu ya kufunga mikono ilianza baada ya kufariki Mtukufu Mtume kiasi kwamba makhalifa na magavana wao walikuwa wakiwaamrisha watu kufunga mikono kwa kudhania kuwa hali hiyo ndio iliyo karibu sana na unyenyekevu?

Na kwa ajili hiyo baada ya riwaya hiyo Bukhari akaweka mlango maalum kwa jina la mlango wa unyenyekevu.

Ibnu Hajar amesema: “Hekima ya muundo huu (kufunga mikono) ni kuwa ni sifa ya muombaji dhalili, nalo ni jambo linalomzuwia mtu kuchezacheza na liko karibu sana na unyenyekevu, Bukhari alizingatia hekima hii hivyo baada yake akaleta mlango wa unyenyekevu.

Kwa ibara nyingine ni kuwa: Kuamrisha kufunga mikono ni dalili ya kuwa watu katika zama za Mtume na muda mfupi baada ya zama zake walikuwa wanaswali kwa kuachia mikono, kisha baadaye ikazushwa fikira hii na hivyo wakawaamrisha watu kufunga mikono.

Pili: Hakika mwishoni mwa njia ya upokezi kuna kitu kina- chounga mkono kuwa kufunga mikono ilikuwa ni kitendo cha waamrishaji wala si kitendo cha mwenyewe Mtukufu Mtume, kwani amesema:

Ismaili amesema: “Silijui jambo hili, labda kama hilo litanasibishwa kwa Mtume.” Hiyo ni kama tutasoma kwa tamko la kutomtaja mtendaji. Maana yake itakuwa yeye hajuwi kuwa jambo hilo ni Sunna ndani ya Sala isipokuwa linanasibishwa tu na Mtume, hivyo riwaya aliyoipokea Sahl bin Saad itakuwa imevushwa (Yaani mlolongo mzima wa wapokezi hadi kumfikia yeye haujatajwa).

Ibnu Hajar amesema: Na katika istilahi za fani ya Hadithi ni kuwa mpokezi atakaposema; inanasibishwa, Maana yake ni kuwa imevushwa toka kwa Mtume.14

(Yaani mlolongo mzima wa wapokezi hadi kumfikia yeye haujatajwa)

Haya yote ni iwapo tutasoma kwa tamko la kutomtaja mtendaji. Ama tukisoma kwa tamko la kumtaja mtendaji, maana yake ni kuwa Sahl ananasibisha hilo kwa Mtume.

Hivyo iwapo ikisihi kusoma kwa tamko la kumtaja mtendaji na Hadithi ikawa si ya kuvushwa basi kauli: “Silijui jambo hili, labda kama….”Iinaonyesha udhaifu wa unasibishaji, na ni kuwa alilisikia toka kwa mtu mwingine na hajamtaja jina.

Ibnu Hajar ndani ya Fat’hul-Bari amesema: Ad-Daniyu amezungumzia kuhusu kuvushwa kwa Hadithi hii akasema: Hii ina ila, kwa sababu ni dhana toka kwa Abu Hazimu, na imesemekana kuwa laiti ingekuwa imevushwa basi asingehitajia kusema: “Silijui jambo hili”15
 
Hadithi Ya Wailu Bin Hajar
Imepokewa kwa sura tofauti:
Sura Ya Kwanza Ya Hadithi:
Muslim amepokea toka kwa Wailu bin Hajar: Kuwa alimuona Mtume kainua mikono yake na kutoa takbira pindi alipoingia kwenye Sala, kisha akajifunika kwa nguo yake, kisha akaweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto.

Alipotaka kurukuu akatoa mikono yake ndani ya nguo kisha akaiinua na kutoa takbira kisha akarukuu…..16

Kutumia hoja ya Hadithi hii ni kutumia hoja ya kitendo na kitendo si hoja isipokuwa mpaka ijulikane kwa nini katenda hivyo, na hilo ni jambo lisilojulikana. Kwa sababu dhahiri ya Hadithi inaonyesha kuwa Mtume alikusanya pande za nguo yake akafunikia kifua chake na akaweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto.

Je alifanya hivyo kwa kuwa ni jambo la Sunna au alifanya hivyo ili nguo yake isifunuke bali nguo igusane na mwili na kujikinga baridi kwa nguo hiyo?

Anuani ya kitendo haijulikani hivyo kitendo hakiwi hoja mpaka itakapojulikana kuwa alifanya hivyo kwa kuwa ni Sunna ndani ya Sala kufanya hivyo.

Na kuna uwezekano mwingine nao ni kuwa kitendo cha Mtume ilikuwa ni kuzuwia nguo isifunuke ndani ya Sala.

At-Tirmidhiy ametoa toka kwa Abu Huraira kuwa amesema: “Mtume alikataza kufunua nguo ndani ya Sala. Akasema: Kufunua ni mtu kuachia nguo bila kufumba pande za nguo yake mbele yake, hivyo iwapo akiifumba hatokuwa ameifunua, na imepokewa toka kwa Mtume kuwa ni karaha kufunua nguo ndani ya Sala.”17

Hakika Mtume aliswali pamoja na Muhajirina na Answari zaidi ya miaka kumi, hivyo laiti kama ingethibiti kufunga mikono toka kwa Mtume basi suala hilo lingenukuliwa kwa wingi na kuenea, na wala asingepokea Wailu peke yake huku katika kunukuu kwake kuna uwezekano wa aina mbili.
Sura Ya Pili Ya Hadithi:
An-Nasai na Al-Bayhaqi wametoa ndani ya vitabu vyao kwa njia mbili tofauti toka kwa Wailu bin Hajar amesema: “Nilimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu anapokuwa kasimama ndani ya Sala hufunga mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto.”18

Katika tamko la Al-Bayhaqi ni: “Anaposimama kwenye Sala hufunga mkono wake wa kushoto kwa mkono wake wa kulia, na nilimuona Al-Qamah anafanya hivyo.”19

Kutumia Hadithii kama dalili kunategemea usahihi wa njia ya upokezi na kutimia kwa hoja.

Ama upande wa njia ya upokezi ni kuwa japokuwa mashekhe wawili (Bukhari na Muslim) wameinukuu kwa njia mbili tofauti lakini zote zimeshirikiana kwa kuwepo Abdallah ndani ya njia zote mbili.

Ndani ya Sunan An-Nasai: “Alitupa habari Abdullah”. Ndani ya Sunan Al-Bayhaqi: “Alitupa habari Abdullah bin Jafar” na mkusudiwa ni Abdullahi bin Jafar bin Najihi Al-Saady.

Inatosha kuthibitisha udhaifu wake kwa aliyonukuu Abdallah Ibnu Imam Ahmad toka kwa baba yake: “Wailu alipokuwa aki- fika kwenye Hadithi yake humtia dosari.”

Sehemu nyingine akasema amenukuu toka kwa baba yake toka kwa mashekhe wake kuwa alisema: “Sikuwa naandika chochote katika Hadithi yake baada ya kunibainikia jambo lake.”

Ad-Dauriyu amesema toka kwa Ibnu Muini kuwa: Si chochote.

Abu Hatim amesema: Yazid ibnu Haruna aliuliza kuhusu yeye, akasema:

“Msiulize kuhusu mambo.”

Amr bin Ali amesema: “Ni dhaifu.”

Abu Hatimu amesema: Hadithi zake hukanushwa sana, anasimulia toka kwa waaminifu mambo yasiyokubalika. Mpaka akasema: An-Nasai amesema: ‘Hadithi zake huachwa.’ Mara nyingine akasema: “Si mwaminifu.”20

Ama hoja ya Hadithi: Kwa sababu huenda Hadithi hii ni picha nyingine ya Hadithi ya kwanza, na tofauti ni kuwa Hadithi ya kwanza ina nyongeza isiyokuwepo kwenye Hadithi hii, kwani katika sura ya kwanza imesemwa kuwa alijifunika nguo yake kisha akaweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto.

Tayari imeshapita kuwa dhahiri ya Hadithi ni kuwa Mtume alikusanya pande za nguo zake akajifunikia kifua chake na akaweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto ili nguo yake isifunuke bali ibakie imegusana na mwili na ajikingie mwili wake dhidi ya baridi.

Hivyo kwa kuwa anuani ya kitendo haijulikani Hadithi hii haiwi hoja kwani haijulikani ni kwa nini alifanya hivyo.

Pamoja na hayo ni kuwa ndani ya Hadithi hii kuna ushahidi unaothibitisha kuwa kitendo cha kufunga mikono hakikuwa kinajulikana kipindi cha mwanzo, kwa sababu ndani ya Hadithi imekuja kauli: “Nilimuona Al-Qamah akifanya hivyo.”

Hivyo laiti kufunga mikono ingekuwa ni jambo lililoenea kati ya maswahaba na waliokuja baada ya maswahaba basi kusingekuwepo na kigezo cha kunasibisha kitendo hiki kilichoenea kwa Al-Qamah mpokezi wa Hadithi toka kwa Wailu.

Na hii inaonyesha kuwa kufunga mkono ilikuwa ni jambo lisiloenea na ndio maana Al-Qamah akalinukuu.
Sura Ya Tatu Ya Hadithi
An-Nasai ametoa kwa njia yake toka kwa Wailu bin Hajar kuwa alisema: Nikasema: Hapana….. Kwenye Sala ya Mtume wa Mwenyezi Mungu jinsi anavyoswali na nikamtazama. Akasimama akatoa takbira na akainua mikono yake mpaka ikalingana na masikio yake, kisha akaweka mkono wake wa kulia juu ya kiganja chake cha kushoto na fundo lake na muundi. 21

Al-Bayhaqi naye ametoa ndani ya kitabu chake kwa tamko hilo hilo.22

Kutumia riwaya hii kama hoja kunategemea usahihi wa njia ya upokezi na hoja yake. Ama kuhusu njia ya upokezi wa An-Nasai, ni kuwa njia hiyo imemjumuisha Aswimu bin Kulaybu Al-Kufiy.

Ibnu Hajar ametaja kuwa alimuuliza Ibnu Shahabu kuhusu dhehebu la Kulaybu je alikuwa Mur’jia. Akasema: Sijui, lakini Shariku bin Abdallah An-Nakhaiy amesema kuwa alikuwa Mur’jia.

Ibnu Al-Madainiy amesema: Hawi hoja akipokea peke yake.23

Ama njia ya Al-Bayhaqi yenyewe imemjumuisha Abdallah bin Rajau. Ibnu Hajar amenukuu toka kwa Ibnu Muini kuwa alisema: Alikuwa mwingi wa kukosea maneno, hana ubaya.

Amr bin Adiyu amesema: Ni mkweli, mwingi wa kuchanganya maneno na kukosea, yeye si hoja, amefariki mwaka 219 au 220 Hijiria. Na mkusudiwa hapa si Abdallah bin Rajau Al-Makiyu ambaye hupokea toka kwa Imam Jafar Al-Sadiq (a.s.) na wengine.

Na hata kama tukijaalia mkusudiwa ni Abdallah bin Rajau Al-Makiyu bado hata yeye hajasalimika na dosari. Ibnu Hajar amenukuu toka kwa As-Sajiy kuwa alisema ana Hadithi zisi- zokubalika.

Ahmad na Yahya wametofautiana kuhusu yeye. Ahmad amesema:

Wamedai kuwa vitabu vyake vilitoweka hivyo akawa anaandika yale aliyoyahifadhi kichwani, na ana riwaya zisizokubalika, na wala sikusikia toka kwake isipokuwa Hadithi mbili tu. Na maelezo kama haya kaeleza Al-Uqay’liyu toka kwa Ahmad.24

Ama hoja ya Hadithi ni kuwa hoja yake iko wazi kuliko Hadithi mbili za mwanzo, na huenda vile vile ikawa Hadithi hii ndio ile ile Hadithi ya mwanzo isipokuwa imenukuliwa kwa namna tofauti na hiyo tofauti inatoka kwa wapokezi.

Hivyo kwa kuwa huenda ikawa ndio ile ile Hadithi ya sura ya kwanza basi umeshajua kuwa kitendo cha Mtume kinategeme- wa vigezo viwili (Ima kuzuwia nguo isifunuke au Sunna), na kwa ajili hiyo haiwi hoja.

Mpaka hapa umetimia uchambuzi kuhusu Hadithi mbili:

1. Hadithi ya Sahl As-Saidiyu.

2. Hadithi ya Wailu bin Hajar kwa sura tatu.

Umeona upungufu wa hoja zake huku kukiwa na udhaifu kati- ka njia za upokezi wa Hadithi ya Wailu. Imebaki Hadithi ya tatu wanayotumia kama dalili ya kufunga mikono kwenye Sala.
Hadithi Ya Abdallah Bin Mas’ud
An-Nasai ametoa toka kwa Al-Hujaju bin Abu Zainabu amese- ma: “Nilimsikia Abu Uthman akisimulia toka kwa Ibnu Mas’ud alisema: Mtume aliniona nikiwa nimeweka mkono wa kushoto juu ya mkono wa kulia ndani ya Sala, basi akachukua mkono wangu wa kulia akauweka juu ya mkono wa kushoto.”25

Al-Bayhaqi naye kaitoa kwa tamko hili hili isipokuwa kwa njia nyingine.

Kutumia Hadithi hii kama dalili kunategemea usahihi wa njia ya upokezi na hoja yake.

Ama kuhusu njia ya upokezi ni kuwa njia zote mbili zimemju- muisha Al-Hajaju bin Abu Zainabu As-Salmiy ambaye Ahmad bin Hambal amemzungumzia kwa kusema: Nahofia asiwe ni yule mwenye Hadithi dhaifu.

Ibnu Muinu amesema: Hana ubaya.

Hasani bin Shajau Al-Bal-khiy amesema toka kwa Ali bin Al- Madayniyu:

Shekhe toka watu wa Wasitu ni dhaifu

An-Nasai amesema: Dhaifu.

Ibnu Ali amesema: Natarajia hana ubaya katika yale anayoyapokea. Kisha akasema: Amesema Ad-Daruqutniy: “Ni dhaifu na wala si mwenye kuhifadhi.”26 Na mengine mengi.

Ama kuhusu hoja yake ni kuwa: Hebu angalia Abdallah bin Mas’ud alikuwa miongoni mwa watu waliotangulia kuingia ndani ya Uislamu, alisilimu mwanzoni mwanzoni mwa utume, kwa ajili ya kumuamini kwake Mtume na Uislamu yakampata yaliyompata toka kwa Maquraishi.

Hivi inawezekana mtu kama huyu asijue namna ya kufunga mikono (ikiwa kama ni Sunna) hata aweke mkono wa kushoto juu ya mkono wa kulia.
Hadithi Dhaifu Zisizokuwa Hoja
Hadithi tulizozitaja ndio tegemezi katika kutoa dalili ya kuthibitisha kufunga mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto. Tayari umeshajua hali zake na jinsi zisivyoweza kusimama kuthibitisha mada husika.

Kuna Hadithi nyingine na riwaya zilizopokewa ndani ya vitabu, nazo kazikusanya Al-Bayhaqi ndani ya Sunan yake. Wala hakuna hata moja inayosihi kuwa dalili kutokana na udhaifu wa njia ya upokezi na hoja yake.

Hivyo ili tukamilishe vipengele vya uchambuzi tutazitoa hizo Hadithi na kuzichambua upande wa njia ya upokezi na hoja zake ili msomaji aweze kujua sehemu zenye dosari.
1. Hadithi Ya Hulbu
Tirmidhiy ametoa toka kwa Qutayba toka kwa Abul-ah’wasu toka kwa Sammaku bin Harbu toka kwa Qubaysatu bin Hulbu toka kwa baba yake amesema: “Mtume alikuwa akituswalisha hivyo anachukua mkono wake wa kushoto kwa mkono wake wa kulia.”27

Al-Bayhaqi ameipokea kwa tamko lingine, nalo ni: “Nilimuona Mtume akiwa kaweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala.”28

Anajibiwa kuwa: Njia ya upokezi ni dhaifu kama ilivyo hoja yake. Ama kuhusu njia ya upokezi angalia wasifu wa wapokezi wawili tu wa Hadithi hii:
Qubaysatu Bin Hulbu
Ad-Dhahabi amesema: Al-Ajaliyu amesema: Ni mwaminifu, na Ibnu Hibana amemtaja katika orodha ya waaminifu.

Ibnu Al-Madainiyu amesema: “Hajulikani.”29

Ibnu Hajar amesema: “Hajulikani, hakuna aliyepokea toka kwake isipokuwa Sammaku peke yake.”

An-Nasai amesema: “Hajulikani.”30
Sammaku Bin Harbu
Ad-Dhahabi amesema: Ni mkweli mno, mwema. Ibnu Mubarak amepokea toka kwa Sufiani kuwa ni dhaifu.

Jarir Ad-Dhabiyu amesema: “Nilikuja kwa Sammaku nikamuona akikojoa wima, hivyo nikarejea na wala sikumuuliza, nikasema: Ameharibikiwa akili.”

Ahmad bin Abu Mariam amepokea toka kwa Yahya: Sammaku ni mwaminifu, Shaabatu alikuwa akimdhoofisha.

Ahmad amesema: “Sammaku ana Hadithi zenye dosari.”

Abu Hatimu amesema: “Ni mwaminifu, mkweli mno.”

Swaleh amesema: Amedhoofika.

An-Nasai amesema: “Akipokea peke yake hawi hoja, kwa sababu alikuwa akisemezwa na anasema, na mengine zaidi ya hayo miongoni mwa maneno ya kudhoofisha.”31

Ahmad amemzungumzia: “Ana Hadithi zenye dosari.”

Ibnu Abu Khaythamu amesema: “Nilimsikia Ibnu Muini akiulizwa kuhusu yeye, ni kitu gani kilichomtia dosari?”

Akasema: “Ameegemeza Hadithi ambazo hajaziegemeza mwingine.”

Ibnu Ammara amesema: “Wanasema kuwa alikuwa akichanganya na wanatofautiana kuhusu Hadithi yake.”

At-Thauriyu alikuwa ikomdhoofisha katika baadhi ya dosari. Yaqub bin Shayba amesema: “Nilimwambia Ibnu Al-Madainiyu: Vipi riwaya ya Sammaku toka kwa Akrimatu?

Akasema: “Ina dosari”

Zakariya bin Ali amesema toka kwa Ibnu Mubarak: “Sammaku ni dhaifu katika Hadithi.” Yaaqubu amesema: “Riwaya yake aliyohusika yeye peke yake toka kwa Akrima ina dosari.”32

Ama kuhusu hoja ya riwaya ni kuwa ndani ya riwaya hiyo haijatamkwa wazi kuwa ameweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wake wa kushoto katika hali ya kisomo tu, bali dhahiri inayoonekana ni kuwa ameweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wake wa kushoto katika hali zake zote za Sala yake. Na hakuna aliyeshikamana na suala hilo.
2. Hadithi Ya Muhammad Bin Abana Al-Answariy
Al-Bayhaqi ametoa kwa njia yake toka kwa Muhammad bin Abana Al-Answari toka kwa Aisha alisema: “Matatu ni kati ya mambo ya unabii: Kuharakisha kufuturu, kuchelewesha daku na kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala.”33

Aliyoyataja Bukhari ndani ya kitabu chake At-Tarikhul-Kabiru yanatosha kuonyesha udhaifu wa Hadithi hii. Baada ya kunukuu Hadithi hii akasema: “Wala hatujui kusikia kwa Muhamad toka kwa Aisha.”

Katika nakala nyingine: “Wala haijulikani kusikia kwa Muhammad.”34

Mtafiti wa kitabu At-Tarikhul-Kabiru cha Bukhari amenukuu kuhusu kauli za baadhi ya wanazuoni wa fani ya elimu ya wapokezi kuhusu yeye, kisha akatoa matokeo kamili yafuatayo:

Hakika yeye ni Ansariyu mtu wa Madaniyu, kisha akawa mtu wa Al-Yamama, na yeye alivusha Hadithi toka kwa Aisha.35
3. Hadithi Ya Aqabatu Bin Sahbani
Al-Bayhaqi amepokea kwa njia yake toka kwa Hammadi bin Sal-matu toka kwa Asimu Al-Jahdariyu toka kwa Aqabatu bin Sahbani toka kwa Ali (a.s.) “Basi Swali kwa ajili ya Mola wako, na uchinje”.

Akasema: “Ni kuweka mkono wako wa kulia juu ya mkono wako wa kushoto ndani ya Sala.”36

Anajibiwa kuhusu dalili hii kuwa: Kwanza: Asimu Al- Jahdariyu hajathibitishwa kuwa ni mwaminifu. Ad-Dhahabi amesema: Asimu bin Al-Ujaji Al-Jahdariyu Al-Basriyu amesoma kwa Yahya bin Yaamuru na Nasru bin Asimu.

Salamu bin Abu Al-Mundhiru na baadhi ya watu wamechukua toka kwake kisomo kilichokwenda kinyume chenye mambo yasiyo kubalika.37

Bukhari amemtaja ndani ya Historia yake akasema: Asimu Al- Jahdariyu anawekwa miongoni mwa watu wa Basra, toka kwa Aqabatu bin Dhabiyanu na wala hajamthibitisha kuwa ni mwaminifu38

Kisha kulingana na nukuu ya Al-Bayhaqi ni kuwa Hadithi inakomea kwa Aqabatu bin Sahbani. Al-Bayhaqi amesema: Na ameipokea Bukhari ndani ya At-Tarikhu katika kutoa wasifu wa Aqabatu bin Dhabayani toka kwa Musa bin Ismaili toka kwa Hammadi bin Salmatu:

Alimsikia Asimu Al-Jahdariyu toka kwa baba yake toka kwa kwa Aqabatu bin Dhabayani toka kwa Ali “Basi swali kwa ajili ya Mola na uchinje” akainua mkono wake wa kulia akauweka katikati ya muundi wake juu ya kifua chake.

Kwa mujibu wa riwaya aliyoinukuu Al-Bayhaqi toka kwa Bukhari ndani ya historia yake inatofautiana na ile aliyoipokea Al-Bayhaqi yeye mwenyewe moja kwa moja, hiyo ni kwa vigezo viwili:

Kwanza: Kwa riwaya ya Al-Bayhaqi njia ya upokezi wa Hadithi hiyo inakomea kwa Aqabatu bin Sahbani, na kwa nukuu ya Bukhari inakomea kwa Aqabatu bin Dhabayani.

Pili: Hakika kwa mujibu wa nukuu ya Al-Bayhaqi ni kuwa.

Asimu Al-Jahdariyu amepokea toka kwa Aqabatu bin Sahbani, na kwa mujibu wa nukuu ya historia ya Bukhari ni kuwa Asimu kanukuu toka kwa baba yake toka kwa Aqabatu bin Dhabayani.

Na bahati mbaya sana ni kuwa ndani ya vitabu vya fani ya wapokezi hamna anuani ya Abu Aujaju. Hivyo Hadithi kama hii abadani haiwi hoja.
Hadithi Ya Ghazuwani Bin Jarir
Al-Bayhaqi amepokea toka kwa Ghazuwani bin Jarir toka kwa baba yake amesema: Ali (a.s.) alikuwa akisimama kwenye Sala na akatoa takbira huweka mkono wake wa kulia kwenye fundo la mkono wake wa kushoto, hubakia katika chali hiyo mpaka anaporukuu, isipokuwa labda akune ngozi au aweke vizuri nguo yake.39

Jarir mzazi wa Ghazawani hajulikani. Hiyo inatosha kud- hoofisha riwaya hii.

Ad-Dhahabi amesema: “Huyu Jariru Ad-Dhabiyu aliyepokea toka kwa Ali na mwanae Ghazawani akapokea toka kwake hajulikani.”40
Hadithi Mbili Za Kuvushwa Za Ghadhifu Na Shadadu
Al-Bayhaqi amepokea akasema: “Tumepokea toka kwa Al- Harithu bin Ghadhifu Al-Kindi na Shadadu bin Shar’habilu Al- Ansari kuwa kila mmoja kati yao alimuona Mtume amefanya hivyo: “Ameweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wake wa kushoto.”41

Haya ndio aliyoyapokea Al-Bayhaqi na Tirmidhi akaandika kwa namna ifuatayo:

Ghatifu bin Al-Harithu.42

Kwa mujibu wa nukuu ya Al-Bayhaqi ni kuwa mpokezi ni Al- Harithu bin Ghadhifu Al-Kindi, ilihali kwa mujibu wa nukuu ya Tirmidhiy mpokezi ni Ghadhifu bin Al-Harithu, hivyo baba akafananishwa na mtoto na hawajajulikana.

Kwa mujibu wa yale aliyonukuu Ibnu Hajar inaonekana kuwa alimdiriki Mtume akiwa mtoto. Ibnu Hajar amenukuu toka kwake akasema: “Nilikuwa mtoto nikipopoa mitende ya Ansari, wakanileta kwa Mtume, akapangusa kichwa changu na kusema: ‘Kula zile zilizodondoka na wala usipopowe mitende yao.”

Bali inaonekana toka kwa baadhi yao kuwa alikuwa miongoni mwa waliokuja baada ya maswahaba na wala hajamdiriki Mtume (s.a.w.w.).

Amesema: “Baadhi ya watu wamemtaja katika watu waliokuja baada ya maswahaba.”43

Hivyo kutokana na waliyoyataja tunapata muhtasari kuwa Hadithi hii haiwi hoja, kwa sababu zifuatazo:

1. Ni Hadithi ya kuvushwa (Yaani mlolongo mzima wa wapokezi haujatajwa), watu wa fani ya Hadithi hawana njia inayoelekea kwa hao wawili.

2. Alimdiriki Mtume akiwa bado mtoto, kwa ajili hiyo ndio maana unaona wanamtambulisha kwa kusema: “Ana uswahi- ba” Yaani uswahiba mchache.

3. Haijathibitika kuwa alikuwa ni swahaba, na kuna kundi limemuhesabu kuwa ni aliyekuja baada ya maswahaba.

Vyovyote vile ni kuwa hii ndio hali halisi ya Hadithi: Kwanza jina lake limechanganywa. Pili imechanganywa kati ya baba na mtoto.

Tatu kama ameishi na Mtume basi ni muda mchache utotoni mwake. Nne haijathibitika kuwa aliishi na Mtume, bali ni miongoni mwa waliokuja baada ya Mtume. Haiwi hoja.
4. Hadithi Ya Nafiu Toka Kwa Ibnu Umar
Al-Bayhaqi ametoa kwa njia yake toka kwa Abdul-Majidi bin Abdul-Azizi bin Abu Rawadu toka kwa baba yake toka kwa Nafiu toka kwa Ibnu Umar kuwa Mtume (s.a.w.w.) alisema: Sisi kundi la manabii tumeamrishwa mambo matatu: Kuharakisha kufuturu, kuchelewesha kula daku, na kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto.

Hii ndio ile ile Hadithi aliyoipokea Muhammad bin Abana Al-Ansari toka kwa Aisha. Angalia namba mbili.

Al-Bayhaqi amesema: Abdul-Majid ameipokea peke yake, na anajulikana kwa jina la Talha bin Amr na yeye ni dhaifu.44

Ad-Dhahabi amemtambulisha kuwa ni mkweli mno na ni Mur’jiu kama baba yake.

Ibnu Muini amethibitisha uaminifu wake. Abu Daud amesema: Ni mwaminifu mwenye kulingania imani ya Ir’jai.

Ibnu Hibana amesema: “Anastahiki kuachwa, ana Hadithi zisizokubalika sana, hubadili habari na ananukuu toka kwa wasimulizi mashuhuri riwaya zisizo kubalika.”

Abu Hatimu amesema: “Ni dhaifu, Hadithi yake huandikwa.”

Ad-Daru Qutniy amesema: “Hawi hoja na (wasimulizi) huwa naye makini. Ahmad bin Abu Mariam amesema toka kwa Ibnu Muini kuwa: “Ni mkweli anapokea toka kwa watu madhaifu.”

Bukhari amesema: “Al-Humaidiyu alikuwa akimzungumzia, na pia akasema ndani ya Hadithi yake kuna baadhi ya tofauti, wala hazijulikani hata Hadithi tano sahihi toka kwake.”45
5. Hadithi Ya Ibnu Jarir Adhabiy
Abu Daud ametoa toka kwa Jarir Dhabiyu toka kwa baba yake amesema: “Nilimuona Ali (a.s.) ameshika mkono wake wa kushoto kwa kutumia mkono wake wa kulia kwenye fundo la mkono juu ya kitovu.”

Abu Daud amesema: “Imepokewa toka kwa Saidi bin Jubairu “Juu ya kitovu.” Abu Maj-lazu amesema: “Chini ya kitovu” na imepokewa toka kwa Abu Huraira kuwa ni dhaifu.46

Anajibiwa kuwa: Hakika Ibnu Jarir Dhabiyu ndio yule yule Ghazawani ibnu Jarir. Na tayari maneno yake kuhusu mzazi wake yameshatangulia, angalia namba nne.

Na huenda Hadithi hii ndio ile ile Hadithi iliyotangulia na wala si Hadithi nyingine.

Ama Hadithi aliyopokea toka kwa Tausi amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa akiweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wake wa kushoto, kisha anaikaza kifuani kwake ilihali akiwa ndani ya Sala.47

Yenyewe ni Hadithi ya kuvushwa kwa sababu Tausi ni miongoni mwa watu waliokuja baada ya maswahaba.

Na kuna riwaya nyingine zimenasibishwa na Ibnu Zubeiri ya kuwa alisema: Kuweka sawa nyayo mbili na kuweka mkono juu ya mkono ni miongoni mwa Sunna.48

Kama alivyosema Abu Huraira: Alichukua kiganja akakiweka juu ya kiganja ndani ya Sala chini ya kitovu.49

Maalum ni kuwa kauli ya sahaba si hoja iwapo haijatokana na Mtume (s.a.w.w.).
Hivi Sasa Haki Imedhihirika
Kutokana na uchambuzi wa mada hii yamebainika mambo yafuatayo:

Kwanza: Abu Humaidu As-Saidiyu ni kati ya walionukuu Sala ya Mtume kwa vipengele vyake na wala hajataja chochote kuhusu kufunga mikono, na alinukuu namna ya Sala ya Mtume mbele ya makumi ya maswahaba, na akapata usadikisho toka kwao.

Na wala kufunga mikono si jambo dogo mpaka mpokezi aghafilike nalo au maswahaba waliokuwepo waghafilike nalo. Hivyo laiti kama Sala ya Mtume ingekuwa ilikuwa na kitendo cha kufunga mikono basi wangemkosoa na kumlaumu kwa kuacha kukitaja.

Pili: Hadithi walizotoa kama dalili ya kuthibitisha kuwa kufunga mikono ndani ya Sala ni Sunna, Hadithi hizo nyingine hoja yake ni dhaifu na nyingine njia ya upokezi wake ni dhaifu au ni dhaifu vyote viwili.

Tatu: Laiti kufunga mikono ingekuwa ni Sunna basi Maimam wa Ahlul-Bayt wote wasingeipinga na kuihesabu kuwa ni mwenendo wa Majusi, hiyo ni kama utakavyoona ndani ya riwaya zao.

Nne: Jambo hili linazunguka kati ya bidaa na Sunna, na kwa kanuni ya tahadhari ni kuacha kufunga mikono, kwa sababu kutenda suala hilo huenda ikawa ni haramu na ni kutenda bidaa. Kinyume na kuacha, kwani katika kuacha hutokua umefanya chochote bali utakuwa umeacha jambo la Sunna tu, na wala haijakatazwa kuacha Sunna.

Tano: Wanachostaajabisha wanazuoni wa fiq’hi wa Kisunni ni kuwa wamegonga milango yote (Katika kutaka kujua ukweli wa jambo hili) isipokuwa mlango wa Ahlul-Bait!
Hadithi Za Ahlul-Bayt
Hakika Maimam wa Ahlul-Bayt walikuwa wakijizuia kufunga mikono huku wakiona kuwa kitendo hicho ni kitendo cha waabudu moto wa Irani ya zamani mbele ya mfalme wao.

Muhammad bin Muslim amepokea toka kwa As-Sadiq au Al- Baqir (a.s.) amesema: “Nikamwambia: Vipi mtu anayeweka mkono wake ndani ya Sala – na imeelezwamkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto?”

Akasema: “Kufanya hivyo ni kuwatukuza wafalme wa kifarisayo, (haifanywi ndani ya Uislamu).50

Zararatu amepokea toka kwa Abu Jafar (a.s.) kuwa alisema: “Ni wajibu juu yako kuielekea Sala yako na wala usitukuze wafalme wa kifarisayo, hakika hilo hufanywa na majusi.”51

As-Suduq amepokea kwa njia yake toka kwa Ali (a.s.) kuwa alisema: “Ni wajibu juu yako kuielekea Sala yako na wala usitukuze wafalme wa kifarisayo, hakika hilo hufanywa na majusi.”

As-Suduq amepokea kwa njia yake toka kwa Ali (a.s.) kuwa alisema: “Muislamu hakusanyi mikono yake ndani ya Sala yake ilihali yeye kasimama mbele ya Allah Mtukufu akijifanananisha na watukuza wafalmeyaani majusi.”52

Na mwisho hebu tugeuze mtazamo wa msomaji kwa kuangalia maneno yaliyotoka kwa Dr. Ali As-Salusi. Yeye baada ya kunukuu mtazamo wa wanazuoni wa fiq’hi wa makundi yote mawili, aliwasifia wanaosema kuwa ni batili na haramu akasema:

“Na hao waliona kuwa ni haramu na batili au haramu tu, hao wanaonyesha chuki ya kimadhehebu na kupenda tofauti kwa ajili ya kuwafarakisha Waisilamu.”53

Ni ipi dhambi ya Shia iwapo juhudi za kielimu na utafiti wa Kitabu na Sunnah umewaongoza kujua kuwa kufunga mikono ni jambo lililozushwa baada ya Mtukufu Mtume, na watu walikuwa wakiamrishwa kufanya hivyo zama za makhalifa.

Atakayedai kuwa ni sehemu ya Sala kwa kuwa ni faradhi au Sunna atakuwa amepandikiza ndani ya dini jambo lisilokuwe- mo. Je hivi malipo ya aliyetumia juhudi za kielimu ni kushutu- miwa kuwa ana chuki za kimadhehebu na kupenda mfarakano?!

Na kama hilo ni sahihi, hivi inasihi kumnasibisha Imam Malik na sifa hiyo? Kwa sababu yeye alikuwa akichukia kufunga mikono kwa namna yoyote ile. Hata tukijaalia kuwa ni sahihi je, inasihi kumshutumu Imam wa Madina kuwa yeye alikuwa akipenda mfarakano?!

Naam, enyi viumbe kwa nini kutokunyoosha mikono na kuifunga hakuwi ni kuonyesha chuki ya kimadhehebu na kupenda mfarakano kati ya Waisilamu?!

Imetafsiriwa na:

Hemedi Lubumba Selemeni.
________________________
1. Muhammad Jawad Al-Mughuniyya: Al-Fiqihi ala Madh-habul- khamsa: 110

2. Angalia ujumbe mfupi kuhusu kuachia mikono wa Dr. Abdul-Hamidi bin Mubarak

3. An-Najafiy: Jawahirul-Kalamu: 11/ 15- 16

4. Al-Bayhaqi: As-Sunan: 2/ 72, 73, 101, 102, . Abu Daud: As-Sunan:1/194, mlango wa kuanza Sala. Hadithi ya 730-736. Al-Tir’midhiy: As-Sunan: 2/ 98, mlango wa wasifu wa Sala. Musnad Ahmad: 5/ 424. Ibnu Khuzayma ndani ya Sahih yake, mlango wa itidali ndani ya rukuu, namba 587

5. Miongoni mwao ni Abu Huraira, Sahl As-Saidiyu, Abu Usaydu As- Saidiyu, Abu Qatadatu Al-Harithu bin Rabiiyu na Muhammad bin Maslamati.

6. Dr. Abdul-Hamidi bin Mubarak: Ujumbe mfupi kuhusu kuachia mikono: 11

7. Bidayatul-Muj’tahid

8. Al-Muwatau:1/158 mlango wa kuweka mkono juu ya mwingine ndani ya Sala, Hadithi ya 46, 47

9. Ujumbe mfupi kuhusu kuachia mikono: 6 - 7

10. Al-huru Al-amiliy: Al-wasailu:4 mlango 1 mlango wa vitendo vya sala. Hadithiu ya 1. Na angalia mlango wa 17 Hadithi ya 1,2.

11. Kuna dalili nyingine zisizo sahihi zinazozungumzia kufunga mikono. Hayo ni kama inavyofahamika toka kwenye maneno ya Al- naswawiy ndani ya Shar’hu yake ya Sahih Muslim:4/358. Tutakuletea maneno yake.

12. Ibnu Hajar: Fat’hul-Bari fi Shar’hi Sahih Bukhari: 2/224. mlan- go wa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto. Sahih Muslim: 2/13, mlango wa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto.
Al-Bayhaqi kaipokea ndani ya As-Sunanl-Kubra: 2/28, Hadithi ya 3, mlango wa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala.

13. Mlengwa ni Ismail bin Abu Awyasi, shekhe wa Bukhari. Hayo ni kama alivyohakikisha Al-Humaidiyu. Angalia Fat’hul-Bari: 5/325

14. Ibnu Hajari mwenyewe: hamishi namba 1

15. Fat’hul-Bari: 4/126

16. Muslim: Sahih:1/13 mlango wa 5 kitabu cha Sala, mlango wa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto. Na katika njia ya Hadithi yumo Hamamu. Na kama anaekusudiwa ni Hamamu bin Yahya basi ni kuwa Ibnu Ammari kamzungumzia kwa kusema: Yahya bin Al-Qatani alikuwa hamjali Hamamu. Umar bin Shaybatu amesema: Alitusimulia Affani akasema: Yahya bin Saidi alikuwa akimtia dosari Hamamu katika Hadithi zake nyingi. Abu Hatimu akasema: Mwaminifu katika kuhifadhi. Angalia Huda Sariy:1/449.

17. Sunanut -Tirmidhiy: 2/217 Hadithi ya 378.

18. Sunanun-Nasaiy: 2/97 mlango wa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala.

19. Sunan-Bayhaqiy: 1/28 mlango wa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala.

20. Tahdhibul-Tahdhibu: 5/174, namba 298.

21. Sunanun-Nasaiy :2/97, mlango wa kuweka mkono wa kulia kwenye mkono wa kushoto ndani ya Sala.

22. Al-Bayhaqi: 2/ 28, mlango wa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala.

23. Tahdhibut-Tahdhibu:5/56 namba 89.

24. Tah’dhibut-Tah’dhibu: 5/211 namba 364

25. Sunanun-Nasaiy: 2/97 mlango wa imamu atakapomuona mtu kaweka mkono wa kushoto juu ya mkono wa kulia

26. Tah’dhibut-Tah’dhibu: 2/201 namba 372

27. Sunanut-Tir-midhiy:2/23, namba 252

28. Sunanul-Bayhaqiy: 2/29

29. Mizanul-Itidali: 3/384 namba 6863

30. Tah’dhibut-Tah’dhibu: 8/350 namba 633

31. Mizanul-Itidali: 2/233 namba 3548.

32. Tah’dhibut-Tah’dhibu: 8/350 namba 633

33. Sunanul-Bayhaqiy: 2/29

34. At-Tarikhul-Kabiru: 11/32 namba 47. Mizanul-Itidali: 3/454 namba 7129.

35. At-Tarikhul-Kabiru: 11/34

36. Sunanul-Bayhaqiy: 2/29

37. Mizanul-Itidali: 2/354, namba 4057.

38. At-Tarikhul-Kabiru: 6/486, namba 3061

39. Sunanul-Bayhaqiy: 2/29

40. Mizanul-Itidali: 1/397 namba 1474

41. Sunanul-Bayhaqiy: 2/29

42. Sunanut Tirmidhiy: 2/32, Hadithi ya 252

43. Al-Isabatu: 3/186, namba 6912

44. Sunanul-Bayhaqiy: 2/29

45. Mizanul-Itidali: 2/648, namba 5183

46. Sunan Abu Daud: 1/201, mlango wa kuweka mono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala, namba 757 na 759

47. Sunan Abu Daud: 1/201, mlango wa kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto ndani ya Sala, namba 757 na 759

48. Sunan Abu Daud: 1/200-221 namba 754 na 758

49. Sunan Abu Daud: 1/200-221, namba 754 na 758.

50. Al-Wassailu: 4 mlango wa 15 Hadithi ya 1 mlango wa vikatiza Sala

51. Al-Wassailu: 4 mlango wa 15 Hadithi ya 2 na 3 na 7 mlango wa vikatiza Sala.

52. Al-Wassailu: 4 mlango wa 15 Hadithi ya 2 na 3 na 7 mlan- go wa vikatiza Sala.

53. Fiqhi Shiatu Imamiyatu sehemu ya tofauti kati yake na Madhehebu manne:183
1. Qur'an Al-Kariim - Tafsir Al-Kashif Juzuu ya kwanza mpaka kumi na sita

2. Uharamisho wa Riba

3. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya kwanza

4. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya pili

5. Hekaya za Bahlul

6. Muhanga wa Imamu Husein (A.S.)

7. Mikingamo iliyomzunguka Imamu Ali (A.S.)

8. Hijab vazi Bora

9. Ukweli wa Shia Ithnaashari

10. Madhambi Makuu

11. Mbingu imenikirimu

12. Abdallah Ibn Saba

13. Khadijatul Kubra

14. Utumwa

15. Umakini katika Sala

16. Misingi ya Maarifa

17. Kanuni za Ndoa na maadili ya Familia

18. Bilal wa Afrika

19. Abudharr

20. Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

21. Salman Farsi

22. Ammar Yasir

23. Qur'an na Hadithi

24. Elimu ya Nafsi

25. Yajue Madhehebu ya Shia

26. Ukusanyaji na Uhifadhi wa Qur'an Tukufu

27. Al-Wahda

28. Ponyo kutoka katika Qur'an.

29. Uislamu mfumo kamili wa maisha ya kijamii

30. Mashukio ya Akhera

31. Al Amali

32. Dua kwa mujibu wa Ahlul Bayt

33. Udhuu kwa mtazamo wa Qur’an na Sunna.

34. Haki za wanawake katika Uislamu

35. Mwenyeezi Mungu na sifa zake

36. Amateka

37. Nafasi za Ahlul Bayt (a.s)

38. Adhana.

39 Upendo katika Ukristo na Uislamu

40. Nyuma yaho naje kuyoboka

41. Amavu n’amavuko by’ubushiya

42. Je, Kufunga Mikono Ni Bidaa au Sunna? Kwa Mtazamo wa Qur’ani na Sunna

43. Kupaka juu ya khofu

Share this article

Comments 0

Your comment

Comment description

Latest Post

Most Reviews

MOST READ