Rafed English

Tawasali

Tawasali by : Seyyid Abdul Rahim Al-Musawi

 

Kitabu kilichoko mikononi mwako ni tarjuma ya kitabu cha Kiarabu kwa jina la, at-Tawassul. Sisi tumekiita, Tawasali.

Kitabu hiki, Tawasali, ni matokea ya kazi ya kielimu iliyofanywa na mwanachuoni wa Kiislamu, Sayyid Abdul Rahim al-Musawi.

Kumekuwepo na zogo kubwa katika miji yetu ya Kiislamu kuhusu usahihi wa tawasali. Baadhi wanasema, ni sahihi kutawasali, na wengine wanasema, ni bidaa - yaani jambo lililozushwa na kuingizwa katika dini. Baadhi ya masheikh wamekwenda mbali zaidi hadi kufikia kuwaita Waislamu wenzao kuwa ni mushirikina au makafiri.

Sheikh Muhammad bin Abdul Wahhab, amewaita mushirikina wale Waislamu wanaotawasali akisema: “Iwapo baadhi ya mushirikina [yaani Waislamu wasiokuwa Mawahabi] wakikwambieni: Sikilizeni! Hakika vipenzi vya Mwenyezi Mungu hawana khofu wala hawahuzuniki; au shufaa ni haki, au Manabii wana jaha kwa Mwenyezi Mungu, au akatoa maneno ya Nabii ambayo kwayo anafanya ni dalili juu ya batili yake, na ikawa wewe hufahamu [yaani huna uwezo wa kumjibu], basi jibu lake ni kumwambia:

‘Hakika Mwenyezi Mungu ndani ya Kitabu Chake ametaja kuwa - ambao ndani ya nyoyo zao mna upotovu huacha aya zilizo waziwazi na hufuata yaliyofichikana.’

Sheikh Abdul Aziz bin Baaz, anasema: “Atakayemwomba Nabii na kumwomba shufaa, basi ametengua Uislamu wake.”

Haya ndiyo maoni ya masheikh hawa wawili wa Kiwahabi kuhusu kutawasali na wale ambao wanaitekeleza. Lakini je, tawasali haina asili katika dini? Ukweli ni kwamba ni ibada maalumu na ina asili katika dini kama utakavyoona katika kitabu hiki.

Kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote. Kutokana na ukweli huu, Taasisi yetu ya Al-Itrah Foundation imeona bora ikichapishe kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili, kwa madhumuni yake yaleyale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili, ili kuongeza ujuzi wao katika masuala ya dini na ya kijamii.

Tunamshukuru ndugu yetu, Hemedi Lubumba Selemani kwa kukubali jukumu hili la kukitarjumi kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwake. Mchapishaji: Al-Itrah Foundation S. L. P. 19701 Dar-es-Salaam, Tanzania.

Neno La Jumuiya

Hakika mirathi ya Ahlul-Bait ambayo imehifadhiwa na Kambi yao na wafuasi wao dhidi ya upotovu inaonyesha ni kambi iliyokusanya aina mbalimbali za taaluma za kiisilamu.

Kambi hii imeweza kulea nafsi mbalimbali zilizo tayari kunywa kutoka kwenye chemchemu hiyo, na kuupa umma wa kiislamu wanachuoni wakubwa wenye kufuata nyayo za Ujumbe wa Ahlul-Bait.

Wanachuoni waliokusanya vidodosa na maswali mbalimbali ya madhehebu na mitazamo tofauti ya kifikira kuanzia ndani ya desturi ya kiislamu hadi nje ya desturi hiyo, huku wao wakitoa majibu na utatuzi makini juu ya maswali hayo ndani ya karne zote.

Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bait imefanya hima kutetea tukufu za Ujumbe wa Uislamu na ukweli wake ambao umechafuliwa na makundi, madhehebu na wanaharakati mbalimbali wenye chuki na Uislamu.

Jumuiya imefuata nyayo za Ahlul-Bait na za wafuasi wa Kambi yao njema ambayo imefanya hima kujibu madai yenye kuendelea na daima ikajaribu kubaki ndani ya msitari wa mapambano kwa kiwango kinachohitajika ndani ya kila zama.

Hakika uzoefu ambao umehifadhiwa ndani ya vitabu vya wanachuoni wa Kambi ya Ahlul-Bait katika dhamira hii ni vya aina ya pekee, kwa sababu una nguzo ya kielimu inayotegemea akili na hoja, huku ukijiepusha na matamanio na uzalendo uliyokatazwa.

Unazungumza na wasomi na wanaharakati wenye fani maalumu, mazungumzo ambayo yanaituliza akili na yanapokewa na maumbile salama.

Jaribio hili la Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Baiti limekuja kuwapa watafuta ukweli hatua mpya ya uzoefu wa thamani katika ulingo wa mazungumzo na maswali na kujibu hoja za utata zilizotolewa zama zilizo- pita au zinazotolewa leo kwa njia ya Tovuti, na hasa kwa kupewa nguvu na baadhi ya nchi zenye chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu.

Jumuia imejiepusha na udadisi uliokatazwa na ni yenye kuhangaikia kuzi- dadisi akili zenye kufikiria na nafsi zenye kutafuta haki ili ziweze kufikia kwenye haki ambayo inatolewa na Kambi ya Ahlul-Bait ulimwengu mzima, ndani ya zama ambazo akili inaerevuka na nafsi na roho zinaboreka kwa kasi ya pekee.

Ni lazima tugusie kuwa mfululizo huu wa tafiti hizi umeandaliwa na Kamati Maalumu toka jopo la wanachuoni watukufu, hivyo tunatoa shukurani njema kwa hawa wote na kwa wasomi na wahakiki kwa kila mmoja miongoni mwao kupitia sehemu ya tafiti hizi na kutoa mchango wao wa thamani kuhusu tafiti hizi.

Tunategemea na kutaraji kuwa tutakuwa tumetoa kile tunachokiweza kati- ka juhudi za kutekeleza baadhi ya wajibu tulioanao mbele ya ujumbe wa Mtukufu Mola Wetu Mlezi ambaye alimtuma Mtume Wake na uongofu na dini ya haki ili aidhihirishe juu kuliko dini zote. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi. JUMUIYA YA KIMATAIFA YA AHLUL-BAITI KITENGO CHA UTAMADUNI

Hakika Tawassul uhalisi wake umeelezwa na Qura’ni tukufu pindi Mwenyezi Mungu alipowaambia waumini:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَابْتَغُوا إِلَيْهِ الْوَسِيلَةَ وَجَاهِدُوا فِي سَبِيلِهِ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ {35}

 

“Enyi mlioamini mcheni Mwenyezi Mungu na tafuteni njia ya kum- fikia.Napiganenikwaajiliyadiniyakeilimpatekufaulu.”Al-Maida: 35.

 

Hakika Aya hii tukufu imehesabu Uchamungu na Jihadi kuwa ni miongo- ni mwa njia za kisheria ambazo mwanadamu anaweza kuzifanya sababu ya kumfikia Mwenyezi Mungu Mtukufu.

 

Na je, kuna njia nyingine ambazo zimehimizwa na Sheria? Au jambo hili ameachiwa mwanadamu na kwa uwezo wake agundue njia nyingine za kumkurubisha kwa Mwenyezi Mungu?

 

Ni wazi kuwa njia ambazo mja anaweza kujikurubisha kwazo kwa Mwenyezi Mungu hazitokani na Juhudi za kielimu, kwani kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu na njia za kupatikana ukuruba huo zinahitaji mwongozo wa Mwenyezi Mungu.

 

Na hapo ndipo Sheria ilipochukua jukumu la kuzibainisha, ikazitolea maelezo na kuziwekea mipaka ndani ya Kitabu na Sunna tukufu. Kila njia isiyokuwa ile iliyoelezwa na Sheria kwa namna ya pekee au ya mjumuisho, basi yenyewe ni aina moja ya bidaa na upotovu.

 

Imam Ali bin Abu Twalib amegusia njia ambazo kwazo mja atajikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, akasema: “Hakika njia bora ya kupita wenye kwendakwaMwenyeziMunguni:KumwaminiYeyenaMtumewake naJihadi katika njia yake, hakika yenyewe ndio heshima ya Uislamu.

 

Na Tamko la dhati, hakika lenyewe ndio silika. Na kusimamisha Swala, haki- ka yenyewe ndio dini. Na kutoa Zaka, hakika yenyewe ni faradhi.

 

Na Funga ya Ramadhani, hakika yenyewe ni ngome dhidi ya adhabu. Na Kuhiji Nyumba tukufu na kufanyia Umra, hakika hivyo viwili vinaondoa ufakiri na kuondoa dhambi. Na kuunga undugu wa damu, hakika kwenyewe ni ongezeko la utajiri katika mali.

 

Na Sadaka ya wazi, hakika yenyewe inaepusha kifo kibaya. Na kutenda wema, hakika wenyewe unazuia kushindwa kwa udhalili.”1

 

Qur’an tukufu imeelekeza mwenendo wa kusifika unaohitajika kwa waislamu, Mwenyezi Mungu akasema:

 

وَلَوْ أَنَّهُمْ إِذْ ظَلَمُوا أَنْفُسَهُمْ جَاءُوكَ فَاسْتَغْفَرُوا اللَّهَ وَاسْتَغْفَرَ لَهُمُ الرَّسُولُ لَوَجَدُوا اللَّهَ تَوَّابًا رَحِيمًا {64}

 

“Nalauwangelikujiawalipojidhulumunafsizaowakaombamsamaha kwa Mwenyezi Mungu na Mtume akawaombea msamaha, bila shaka wangemkutaMwenyeziMunguMwenyekupokeatoba,Mwenyekure- hemu.” An-Nisai:64.

 

Kwa waislamu utaratibu huu uliosifiwa haukomei kipindi cha uhai wa Mtukufu Mtume tu, hilo ni baada ya Mwenyezi Mungu kusema:

 

وَلَا تَحْسَبَنَّ الَّذِينَ قُتِلُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ أَمْوَاتًا ۚ بَلْ أَحْيَاءٌ عِنْدَ رَبِّهِمْ يُرْزَقُونَ {169}

 

Wala usidhani wale waliouliwa katika njia ya Mwenyezi Mungu kuwa ni wafu, bali wako hai wanaruzukiwa kwa Mola wao Mlezi.”Al-Imrani:169.

Hivyo yenyewe ni Ibada endelevu inayofanywa hata baada ya kifo cha Mtukufu Mtume, na waislamu waliifahamu ruhusa hiyo na wakaitenda baada ya kifo chake kama walivyosema baadhi ya wafasiri.2

Hivyo hakuna kizuizi cha mahusiano na Mwenyezi Mungu na kuomba msamaha kutoka kwake au kuomba kupata haja za kiakhera na kidunia kwa njia ya kupitia njia ya Mtukufu Mtume ili awaombee kwa kuzingatia ukuruba wake kwa Mwenyezi Mungu na nafasi yake maalumu kwake. Njia hii imehimizwa na Sheria na kuainishwa na Qur’ani tukufu. Kwa ufafanuzi zaidi tutafuatilia utafiti katika nukta zifuatazo:

Kwanza: Maana ya Tawassuli kilugha na kiistilahi.

Pili: Rai mbalimbali kuhusu hukumu ya Tawassuli.

Tatu: Ruhusa ya Tawassuli ndani ya Qur’ani.

Nne: Tawassuli ndani ya Hadithi za Mtume.

Tano: Mwenendo wa Waislamu katika Tawassuli. Sita: Tawassuli kwa mujibu wa Ahlul-Baiti.

Saba: Mjadala dhidi ya wanaokanusha ruhusa ya kisheria juu ya Tawassuli
________________________
1. Nahjul-Balagha, uhakiki wa Subhiyu Asw-Saleh: Hotuba ya 110/ 163.

2. Tafsiri Ibnu Kathir 1:532.

Ndani ya kamusi ya Lisanul-Arabi imeelezwa kuwa: Al-Wasilatu Indal- Malaki: Al-Wasilatu ni: Ngazi na ukuruba. (Husemwa): fulani ametumia Wasila kwa Mwenyezi Mungu: Pindi anapotenda amali itakayomkurubisha Kwake.

Al-wasilu: Mwenye raghba na Mwenyezi Mungu. Labidu amesema: “Nawaona watu hawajui thamani ya jambo lao. Ndio; kila mwenye rai ana raghba ya kuelekea kwa Mwenyezi Mungu.”

Ametawasali Kwake kwa Wasila: Pindi anapojikurubisha Kwake kwa amali fulani.

Na ametawasali Kwake kwa kadha: Amejikurubisha Kwake kwa utukufu wenye huruma utakaomhurumia.

Na Al-Wasilatu ni: Fungamano na ukuruba, na wingi wake ni Al-Wasailu. Mwenyezi Mungu amesema: “Hao wanaowaomba, wao wenyewe wanatafuta njia (Al-Wasilatu) iliyo karibu sana miongoni mwao ya kwenda kwa Mola Wao Mlezi” (17: 57) 1

Na kamusi nyingine za lugha ya kiarabu zimetoa baadhi ya mifano halisi ya neno Al-Wasilatu, kwa sababu maana yake ni miongoni mwa ufahamu wa wazi na uhalisi wake si zaidi ya kukifanya kitu njia ya kufikia jambo jingine ambalo ndilo makusudio na shabaha. Na njia hiyo hutofautiana kulingana na tofauti za makusudio.

Yule anayetafuta radhi za Mwenyezi Mungu njia yake ya kupitia huwa ni matendo mema ambayo kwayo hupata ridhaa zake, na anayetaka kuizuru Nyumba tukufu ya Mwenyezi Mungu hutumia kile kitakachomfikisha huko.2

Ibnu Kathir amesema kuhusu Tawassuli kuwa: “Ni mwanadamu afanye kiungo kati yake na Mwenyezi Mungu ili akidhiwe haja yake kwa sababu ya kiungo hicho.”3
________________________
1. Lisanul-Arabi cha Ibnu Mandhuri, Juzuu ya 11, kitomeo: Wasala.

2. At-Tawassul fi Ash-Shariati Al-Islamiya, Jafar Subhani: 17.

3. Tafsir ya Ibnu Kathir 1: 532.

Kabla hatujaingia kwenye dalili za Tawassuli na uhalisi wake kisheria na kisha kuzijadili, hatuna budi kwanza tunukuu muhtasari wa rai mbalimbali ambazo zimepatikana kuhusu kuruhusiwa na kukatazwa kwa Tawassuli.

Rai Ya Kwanza: Kukatazwa Tawassuli:

Al-Baniyu ndani ya kitabu chake ametoa rai hiyo na kuona kuwa ni upotovu. Na katika utangulizi wa Kitabu Sharhu At-Twahawiyatti1 amesema: “Hakika suala la Tawassuli si miongoni mwa maswala ya kiimani.”

Na miongoni mwa wanaokataza Tawassuli ni Muhammad bin Abdul- Wahabi, anasema: “Iwapo baadhi ya Mushirikina (Yaani Waisilamu wasiyokuwa Mawahabi) wakikwambia: Sikilizeni; “Hakika vipenzi vya Mwenyezi Mungu havina khofu wala havihuzuniki.”2

Au shufaa ni haki au Manabii wana jaha kwa Mwenyezi Mungu au akatoa maneno ya Nabii ambayo kwayo anafanya ni dalili juu ya batili yake, na ikawa wewe hufahamu (Yaani huna uwezo wa kumjibu), basi jibu lake ni kumwambia: Hakika Mwenyezi Mungu ndani ya Kitabu chake ametaja kuwa ambao ndani ya nyoyo zao mna upotovu huacha Aya zilizo waziwazi na hufuata yaliyofichikana.”3

Na miongoni mwa wanaozuia ni Abdul-Aziz bin Bazi, kwani anasema: “Atakayemwomba Nabii na kumwomba shufaa, basi ametengua Uislamu wake.”4

Rai Ya Pili: Kauli Ya Kuruhusu:

As-Shawkani Az-Zaydiyu ameona hivyo ndani ya kitabu chake (Tuhfatudh-Dhakirina) kwa kusema: “Na anatawasali kwa Mwenyezi Mungu kupitia Manabii wake na watu wema.”5

As-Samuhudiyu Ash-Shafiiyyu ameruhusu kwa kusema: “Kutawasali kupitia Mtume inawezekana kukawa kwa kuomba jambo hilo kutoka kwake, ikimaanisha kuwa (s.a.w.w.) ana uwezo wa kusababisha jambo hilo kwa yeye (s.a.w.w.) kuomba na kukuombea kwa Mola wake Mlezi, hivyo inarudi kwenye kumwomba dua yake; japokuwa ibara zinatofautiana.

Na miongoni mwa Tawassuli ni mtu kumwambia: Nakuomba kuingia pamoja na wewe Peponi Hakuna kinachokusudiwa hapa ila ni Mtume (s.a.w.w.) kuwa sababu na mwombezi”6

Ibnu At-Taymiyya ndani ya kitabu (Mansakul-Marawiziyu) amenukuu kutoka kwa Ahmad bin Hanbali kuwa Mtume (s.a.w.w.) ana Tawassuli na Dua. Pia amenukuu hilo kutoka kwa Ibnu Abid-Duniya na Al-Bayhaqi na At-Tabarani kwa njia mbalimbali akithibitisha usahihi wake.7

Na miongoni mwa wanaosema kuwa inaruhusiwa ni Imam Shafi, amesema: “Mimi hutafuta baraka kupitia Abu Hanifa na huja kwenye kaburi lake kila siku, na ninapopatwa na haja huswali rakaa mbili kisha huja kwenye kaburi lake na kumwomba Mwenyezi Mungu haja kwake na huwa haichelewi kukidhiwa.”8

Na miongoni mwa wanaosema kuwa inaruhusiwa ni Abu Ali Al-Khalali Sheikh wa kihambali kwani anasema: “Sikuhuzunishwa na jambo lolote kisha nikaja kwenye kaburi la Musa bin Jafar na kutawasali kupitia kwake ila Mwenyezi Mungu alinirahisishia lile nilipendalo.”9

Ama Shia Imamiya wao wamesema: “Katika kukidhiwa haja na kuondolewa matatizo inaruhusiwa kutawasali kupitia Nabii na Maimamu baada ya kifo chao, kama inavyoruhusiwa katika hali ya uhai wao, kwakuwa kufanya hivyo; kwanza si kumsemeza asiyekuwepo, na pili si shirki.”10

Rai Ya Tatu: Kutenganisha Kati Ya Aina Za Tawassuli:

Rai hii ni ya Ibnu At-Taymiyya, lakini tunamkuta katika suala la Tawassuli anatapatapa kirai, mara anakanusha na mara nyingine anaruhusu, na tatu anatenganisha. Na alipoonyesha vigawanyo vyake vya sura za Tawassuli, aliruhusu viwili na kuharamisha cha tatu, amesema: “Neno Tawassuli, linakusudiwa maana tatu: Mojawapo ni: Kutawasali kwa kumtii Mtume na kumwamini, na hili ndio asili ya Imani na Uislamu, na atakayelikanusha basi ukafiri wake ni dhahiri kwa watu maalumu na wa kawaida.

Pili: Kutawasali kwa dua yake na shufaa yake - Yaani Mtume hapa ndiye anayeomba na kumwombea moja kwa moja - hili lilifanyika zama za uhai wake na litafanyika siku ya Kiyama, watatawasali kupitia shufaa yake. Na atakayekanusha hili basi yeye ni kafiri murtadi anayetakiwa kutubu, basi akitubu sawa na kama sivyo huuwawa akiwa murtadi.

Tatu: Kutawasali kupitia shufaa yake baada ya kifo chake na kuapa kwa Mwenyezi Mungu kupitia dhati yake, hili ni miongoni mwa Bidaa iliyozushwa.”11
________________________
1. Al-Bisharatu Wal-Ittihafi cha As-Saqafi: 52. Amenukuu toka kwenye Sharhu At-Twahawiya: 60.

2. Yunus: 62.

3. Kashfu -Shubuhati cha Muhammad bin Abdul-Wahabi: 60.12 Mukhalafatul-Wahabiyati Lil-Qur’ani Was-Sunnati cha Umar Abdus-Salami:

4. Amenukuu toka kwenye Al-Aqidatus-Swahihatu Wanawakidhul-Islami cha Abdul-Aziz bin Abdullah bin Bazi.

5. Tuhfatudh-Dhakirina cha Ash-Shawkani: 37.

6. Wafaul-Wafa Biakhbari Daril-Mustwafa cha As-Samuhudiyu 2: 1374.

7. At-Tawassulu Wal-Wasilatu cha Ibnu At-Taymiyya: 144-145, chapa ya Darul- Afaki mwaka 1399 A.H. Na itakujia rai yake yeye mwenyewe.

8. Tarikhu Baghdadi 1: 123, mlango wa yaliyoelezwa kuhusu makaburi ya Baghdadi.

9. Tarikhu Baghdadi 1: 120, mlango wa yaliyoelezwa kuhusu makaburi ya Baghdadi.

10. Al-Barahinu Al-Jaliyatu fi Daf ’i Tashikikatil-Wahabiyya, cha As-Sayyidu Muhammad Hasani Al-Kazawiniyu Al-Hairiyu: 30.

11. Tazama: At-Tawassulu Wal-Wasila: 13, 20, 50.

Manabii na waja wema wamethibitisha ukweli wa Tawassuli kama Ibada ya kisheria isiyo na vumbi lolote. Na Qur’ani imetunukulia maeneo mengi ambayo watu walitawasali kupitia Manabii na Mawalii kwa lengo la kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, na baada ya dua zao yalikuwa yanatimia na kujibiwa maombi yao.

Miongoni mwa maeneo yaliyoelezwa na Qur’ani tukufu ni:

a) Mwenyezi Mungu amesema:

وَأُبْرِئُ الْأَكْمَهَ وَالْأَبْرَصَ وَأُحْيِي الْمَوْتَىٰ بِإِذْنِ اللَّهِ ۖ {49}

 

“Na niwapoze vipofu na wenye mbalanga, niwafufue wafu kwa idhini yaMwenyeziMungu.”
Al-Imrani:49.

 

Hapa tunakuta watu wametawasali kupitia Isa (a.s.), lakini kutawasali huku hakukutokana na imani kuwa Isa (a.s.) ana uwezo usiyokuwa wa Mwenyezi Mungu, bali kulitokana na imani yao kuwa Isa (a.s.) ana uwezo unaomwezesha kuponya magonjwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu kwa kuwa yeye (a.s.) ni mwenye jaha mbele ya Mwenyezi Mungu. Na hili halihesabiwi shirki; kwani shirki ni kuamini Isa ana uwezo wa kujitegemea usiotokana na uwezo wa Mwenyezi Mungu. Na hakuna mwislamu yeyote anayesema hilo.

 

b) Mwenyezi Mungu amesema:

 

قَالُوا يَا أَبَانَا اسْتَغْفِرْ لَنَا ذُنُوبَنَا إِنَّا كُنَّا خَاطِئِينَ {97}

 

Wakasema: Ewe baba yetu tuombee msamaha kwa dhambi zetu, hakikasisitulikuwaniwenyemakosa.”Yusuf:97.
Hakika wana wa Yakub hawajaomba msamaha kutoka kwa Yakub kwa kumweka kando na uwezo wa Mwenyezi Mungu, bali walimfanyaYakub (a.s.) kiungo katika kuomba maghufira kwa kuwa yeye (a.s.) ni mtu wa karibu na mwenye jaha kwa Mwenyezi Mungu. Hili liko wazi kupitia jibu la Yakub kwa wanawe:

 

قَالَ سَوْفَ أَسْتَغْفِرُ لَكُمْ رَبِّي ۖ إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ {98}

 

“Akasema:NitakuombeenimsamahakwaMola WanguMlezi,kwani yeyendiyeMwingiwakusameheMwenyekurehemu.”Yusuf:98.

 

c) Mwenyezi Mungu amesema:

 

وَلَوْ أَنَّهُمْ إِذْ ظَلَمُوا أَنْفُسَهُمْ جَاءُوكَ فَاسْتَغْفَرُوا اللَّهَ وَاسْتَغْفَرَ لَهُمُ الرَّسُولُ لَوَجَدُوا اللَّهَ تَوَّابًا رَحِيمًا {64}

 

“Nalauwangelikujiawalipojidhulumunafsizaowakaombamsamaha kwa Mwenyezi Mungu na Mtume akawaombea msamaha, bila shaka wangemkuta Mwenyezi Mungu Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu.” An-Nisa:64.

“Na lau wangelikujia walipojidhulumu nafsi zao wakaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu na Mtume akawaombea msamaha, bila shaka wangemkuta Mwenyezi Mungu Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu.” An-Nisa: 64.

Aya inaashiria kukubaliwa kwa maghufira anayowaombea Mtume waisla- mu wenye kutubu, kwa sababu ana jaha kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu. Na wakati huohuo inatilia mkazo umuhimu wa waislamu kuja kwa Mtukufu Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa lengo la Mtume kuwaombea maghufira.1

Ndiyo, hayo yote ni zama za uhai wake.

Aina Za Tawassuli Kama Zinavyoonyeshwa Na Quran Tukufu18

Mwenyezi Mungu ndani ya Qur’ani tukufu amewahimiza waja wake waumini kutawasali na akaruhusu Tawassuli za aina mbalimbali, na hapa kwa ufupi tunakuletea aina mbalimbali za Tawassuli zilizoruhusiwa kisheria ndani ya Qur’ani tukufu.

A) Kutawasali Kupitia Majina Ya Mwenyezi Mungu:

Amesema:

وَلِلَّهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ سَيُجْزَوْنَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ {180}

 

“Na Mwenyezi Mungu ana majina mazuri basi mwombeni kwayo, na waacheniwalewanaoharibuutakatifuwamajinayakewatalipwayale waliyokuwawakiyatenda.”Al-Aaraf:180.

Aya inatoa wasifu wa majina ya Mwenyezi Mungu kuwa yote ni mazuri bila kubagua, kisha inaamuru maombi kupitia kwayo, hivyo mja anapotaja majina yake ambayo yamebeba kila heri na uzuri, rehema, maghufira na utukufu, kisha mja akaenda mbele ya Mwenyezi Mungu kuomba maghufira dhidi ya madhambi na akaomba kukidhiwa haja, basi Mwenyezi Mungu atajibu dua ya mwenye kutawasali kupitia majina yake.

B) Kutawasali Kupitia Matendo Mema:

Kwa hakika matendo mema huhesabiwa kuwa ni njia za kisheria ambazo kupitia kwazo mja hujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Tawassuli maana yake ni kutanguliza kitu fulani kwenye uwanja wa Mola Mlezi kwa lengo la kupata ridhaa yake, basi hamna shaka kuwa matendo mema ni miongoni mwa njia bora ambazo anashikamana nazo mja kwa lengo la kutimiza haja zake. Mwenyezi Mungu amesema:

وَإِذْ يَرْفَعُ إِبْرَاهِيمُ الْقَوَاعِدَ مِنَ الْبَيْتِ وَإِسْمَاعِيلُ رَبَّنَا تَقَبَّلْ مِنَّا ۖ إِنَّكَ أَنْتَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ {127}

 

رَبَّنَا وَاجْعَلْنَا مُسْلِمَيْنِ لَكَ وَمِنْ ذُرِّيَّتِنَا أُمَّةً مُسْلِمَةً لَكَ وَأَرِنَا مَنَاسِكَنَا وَتُبْ عَلَيْنَا ۖ إِنَّكَ أَنْتَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ {128}

 

“NaIbrahimnaIsmailwalipoinuamisingiyaNyumba.EeeMolawetu Mleziutukubalie,hakika WewendiyeMwenyekusikia,Mwenye kujua.EeeMola WetuMlezi,utufanyetuwewenyekunyenyekea Kwakonautuonyesheibadazetunautupokelee,bilashaka Wewe ndiyeMwenyekupokea,Mwenyekurehemu.” Baqara:127-128.

 

Hapa Aya inahimiza mafungamano ya matendo mema, nayo ni kujenga Nyumba na dua ambayo Nabii Ibrahim alikuwa akitamani itimie, nayo ni kukubaliwa kwa matendo mema. Na kutokana na kizazi chake upatikane umma wenye kunyenyekea kama inavyosisitiza kauli ya Mwenyezi Mungu:

 

الَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا إِنَّنَا آمَنَّا فَاغْفِرْ لَنَا ذُنُوبَنَا وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ {16}

 

“Ambao husema: Mola wetu Mlezi, hakika sisi tumeamini basi tusamehe madhambi yetu, na utuepushe na adhabu ya moto.”Al- Imrani:16

Utaona kaunga kitendo cha kuomba maghufira kwenye kauli yake: “Eee Mola wetu Mlezi, hakika sisi tumeamini.” Hivyo Al-Fau hapo inaonyesha fungamano kati ya imani na kuomba maghufira.

C) Kutawasali Kupitia Dua Ya Mtukufu Mtume:

Qur’ani tukufu imeashiria nafasi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), utukufu wake na hadhi yake mbele ya Mwenyezi Mungu na tofauti kati yake na watu wengine, akasema:

لَا تَجْعَلُوا دُعَاءَ الرَّسُولِ بَيْنَكُمْ كَدُعَاءِ بَعْضِكُمْ بَعْضًا ۚ {63}

 

“Msifanye wito wa Mtume baina yenu kama wito wa nyinyi kwa nyinyi.”An-Nur:63.

 

Pia Qur’ani tukufu ikaashiria kuwa Mtukufu Mtume ndiye mmoja wa amani mbili ardhini, akasema:

 

وَمَا كَانَ اللَّهُ لِيُعَذِّبَهُمْ وَأَنْتَ فِيهِمْ ۚ وَمَا كَانَ اللَّهُ مُعَذِّبَهُمْ وَهُمْ يَسْتَغْفِرُونَ {33}

 

“Na Mwenyezi Mungu hakuwa wa kuwaadhibu maadamu wewe umo pamoja nao, wala Mwenyezi Mungu hakuwa wa kuwaadhibu hali wanaombamsamaha.”Al-Anfal:33.

 

Kisha tunaikuta Qur’ani tukufu sehemu zaidi ya moja inakutanisha Jina la Mwenyezi Mungu na Jina la Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na kuyanasibisha na kitendo kimoja, anasema:

 

وَسَيَرَى اللَّهُ عَمَلَكُمْ وَرَسُولُهُ ثُمَّ تُرَدُّونَ إِلَىٰ عَالِمِ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ {94}

 

“Na Mwenyezi Mungu ataviona vitendo vyenu na Mtume wake, kisha mtarudishwakwaMjuziwasirinadhahiri.”At-Tawbah:94.

 

Na anasema:

 

وَمَا نَقَمُوا إِلَّا أَنْ أَغْنَاهُمُ اللَّهُ وَرَسُولُهُ مِنْ فَضْلِهِ ۚ {74}

 

“Na hawakuona kosa ila ya kuwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake amewatajirishakwafadhilaZake.”At-Tawbah:74.

 

Na Aya nyingine ambazo ndani yake kuna jina la Mtukufu Mtume limekutanishwa na jina la Mwenyezi Mungu, hivyo ikawa hii ndio nafasi ya Mtume kwa Mwenyezi Mungu, basi dua yake haikataliwi na hujibiwa ombi lake, na anayeshikamana na dua yake anakuwa kashikamana na nguzo imara.

 

Kwa ajili hiyo tunamkuta Mwenyezi Mungu anawaamuru wenye dhambi miongoni mwa waislamu washikamane na dua yake na wamwombe maghufira Mwenyezi Mungu kwenye kikao chake na wamwombe Mtume awaombee maghufira ili kitendo cha Mtume kuwaombea maghufira kiwe sababu ya kuteremka rehema zake na kukubaliwa toba yao. Mwenyezi Mungu amesema:

 

وَمَا أَرْسَلْنَا مِنْ رَسُولٍ إِلَّا لِيُطَاعَ بِإِذْنِ اللَّهِ ۚ وَلَوْ أَنَّهُمْ إِذْ ظَلَمُوا أَنْفُسَهُمْ جَاءُوكَ فَاسْتَغْفَرُوا اللَّهَ وَاسْتَغْفَرَ لَهُمُ الرَّسُولُ لَوَجَدُوا اللَّهَ تَوَّابًا رَحِيمًا {64}

 

“Na hatukumpeleka Mtume yeyote ila apate kutiiwa kwa amri ya Mwenyezi Mungu. Na lau wangelikujia walipojidhulumu nafsi zao wakaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu na Mtume akawaombea msamaha, bila shaka wangemkuta Mwenyezi Mungu ni Mwenye kupokeatoba,Mwenyekurehemu.”An-Nisa:64.

 

Na kuhusu maana hii ni kauli ya Mwenyezi Mungu:

 

وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا يَسْتَغْفِرْ لَكُمْ رَسُولُ اللَّهِ لَوَّوْا رُءُوسَهُمْ وَرَأَيْتَهُمْ يَصُدُّونَ وَهُمْ مُسْتَكْبِرُونَ {5}

 

“Na wanaambiwa: Njooni Mtume wa Mwenyezi Mungu atakuombeeni msamaha huvigeuza vichwa vyao, na unawaona wana- jizuianawakijionaniwakubwa.”Al-Munafiquna:5.

 

D) Kutawasali Kupitia Dua Ya Ndugu Muumini:

Mwenyezi Mungu amesema:

وَالَّذِينَ جَاءُوا مِنْ بَعْدِهِمْ يَقُولُونَ رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ وَلَا تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا لِلَّذِينَ آمَنُوا رَبَّنَا إِنَّكَ رَءُوفٌ رَحِيمٌ {10}

 

“Na waliokuja baada yao wanasema: Mola wetu Mlezi tusamehe sisi na ndugu zetu waliotangulia katika imani, wala usiweke mfundo kwa walioamini, Mola wetu Mlezi, hakika wewe ni Mpole sana, Mwenye kurehemu.”Al-Hashr:10.

Aya tukufu inaonyesha kuwa waumini waliofuatia wanawatakia maghufira ndugu zao waliotangulia, na hii inaonyesha kuwa dua ya ndugu kwa ndugu yake ni jambo la kupendeza na hujibiwa.

E) Kutawasali Kupitia Manabii Na Watu Wema Wao Wenyewe:

Fungu hili si fungu lililotangulia ambalo ni kutawasali kupitia dua ya Mtukufu Mtume, bali lenyewe ni kutawasali kupitia Manabii wenyewe na watu wema na kuwafanya njia ya kujibiwa dua na kuelezea kwa sauti ya juu cheo na hadhi waliyonayo mbele ya Mwenyezi Mungu.

Ikiwa tumetawasali kwa Mwenyezi Mungu kupitia dua ya Mtume kama njia ya kufika kwake, basi katika fungu hili tunamfanya Mtume mwenyewe na heshima yake njia ya kufika kwa Mtukufu Mola Mlezi. Inajulikana kuwa Al-Wasila ni dua itokanayo na ule utu ambao Mwenyezi Mungu ameutukuza na kuukuza na kunyanyua hadhi yake kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ {4}

 

“Natukakutukuziasifazako.”Al-Inshirah:4.

 

Na akawaamuru waumini kumheshimu na kumtukuza, akasema:

 

فَالَّذِينَ آمَنُوا بِهِ وَعَزَّرُوهُ وَنَصَرُوهُ وَاتَّبَعُوا النُّورَ الَّذِي أُنْزِلَ مَعَهُ ۙ أُولَٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ {157}

“Basiwalewaliomwaminiyeyenakumtukuzanakumsaidianawakai- fuatanuruiliyoteremshwapamojanaye,haondiowenyekufaulu.”Al- Aaraf:157.

Ikiwa nguzo ya kujibiwa dua ni utu wake wa pekee wa juu na nafasi yake kwa Mwenyezi Mungu basi ni bora mwanadamu atawasali kupitia utu huo kama anavyotawasali kupitia dua yake. Hivyo atakayekiri kuruhusiwa aina ya mwanzo na akakataza ya pili basi atakuwa ametenganisha kati ya mambo mawili yasiyoachana.

Aina hii ya Tawassuli inaungwa mkono na Sunna ya Mtukufu Mtume iliyopokewa kwa njia sahihi ambayo vigogo wote wa Hadithi wameikubali.2

F) Kutawasali Kupitia Haki Ya Waja Wema, Heshima Yao Na Vyeo Vyao:

Hakika anayefuatilia sera ya waislamu ataikuta imejaa aina hii ya Tawassuli, yaani wao wanatawasali kupitia vyeo vya waja wema na heshi- ma zao mbele ya Mwenyezi Mungu na haki yao juu Yake, na hili ndilo ambalo ufafanuzi wake unakuja kama ifuatavyo:
________________________
1. Tazama: Mukhalafatul-Wahabiyati Lil-Qurani Was-Sunnati: 22.

2. Rejea At-Tirmidhi, kitabu cha maombi, mlango wa 119, namba 3578, 5: 531. Na Sunanu Ibnu Majah 1: 441 namba 1385. Na Musnad ya Ahmad 4: 138, Hadithi ya 16789.

Zimepokewa Hadithi mbalimbali zikionyesha ruhusa ya kutawasali kupitia Nabii au Mawalii Wema.

(I) Toka kwa Uthman bin Hunaif amesema: “Mtu mmoja kipofu alikwen- da kwa Mtume akasema: ‘Niombee kwa Mwenyezi Mungu aniponye.’ Mtume akamwambia: ‘Ukipenda nitaomba na ukipenda vumilia na ndiyo bora.’ Yule mtu akamwambia Mtume: ‘Muombe Mwenyezi Mungu.’ Basi Mtume akamwamuru atawadhe vizuri na aswali rakaa mbili na aombe kwa kutumia dua hii: “Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi nakuomba na ninaelekea kwako kupitia kwa Mtume wako, Mtume wa Rehema. Ewe Muhammad, hakika mimi naelekea kwa Mola Wangu Mlezi kupitia kwako katika haja yangu ili ikubaliwe. Ewe Mwenyezi Mungu mfanye Muhammad kuwa mwombezi wangu.”1

Hadithi hii haina dosari katika usahihi wake mpaka Ibnu At-Taymiyya ameiona kuwa ni sahihi na akasema: “Abu Jafar anayekusudiwa aliyomo ndani ya njia ya upokezi wa Hadithi hii ni Abu Jafar Al-Khatwamiyu, na yeye ni mwaminifu.”

Ama Ar-Rifai yeye amesema: “Hamna shaka kwamba Hadithi hii ni sahihi na ni mashuhuri. Na imethibiti bila wasiwasi wala mashaka kuwa macho ya kipofu yule yalirudia kuona kwa sababu ya dua ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.).”2

Hadithi hii wameileta An-Nasaiy, Al-Bayhaqiy, At-Tabaraniy, At-Tirmidhiy na Al-Hakim ndani ya Al-Mustadrak yake.3

Kwa Hadithi hii inazidi kuthibiti Sheria ya Tawassuli, kiasi tunamkuta Mtume wa Mwenyezi Mungu amemfunza kipofu namna ya kutawasali kwa Mwenyezi Mungu kupitia Nabii Wake, Nabii wa Rehema, na kum- wombea ili kukidhi haja yake. Na makusudio ya Nabii ni Nabii mwenyewe si dua yake. Na kuelekea kwa Mwenyezi Mungu kupitia jaha ya Mtume na njia yake.

(II) Atwiyatu Al-Awfi amepokea kutoka kwa Abu Said Al-Khidri kwam- ba Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Yeyote atakayetoka nyumbani kwake kwenda kuswali akasema:

“Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba kwa haki ya wanaokuomba na ninakuomba kwa haki ya mwendo wangu huu, kwani mimi sikutoka kwa maringo na majivuno, wala kujionyesha wala kutaka kusifiwa, nimetoka kwa kuogopa ghadhabu zako na kutafuta radhi zako; basi ninakuomba uniepushe na moto na unisamehe madhambi yangu, kwani hakuna anayesamehe madhambi isipokuwa Wewe.”

Basi Mwenyezi Mungu atamwelekea mtu huyo kwa dhati yake na watam- takia msamaha Malaika elfu sabini.”4

Hakika Hadithi hii inaonyesha ruhusa ya kutawasali kwa Mwenyezi Mungu kupitia heshima ya mawalii wema na daraja zao na cheo chao walichonacho mbele ya Mwenyezi Mungu, basi mtu huwafanya hao ndio viun- go na waombezi ili haja zao zikubaliwe na dua zao zipokelewe.

(III) Anas bin Malik amesema: “Alipofariki Fatima binti Asad, Mtume aliingia mahala alipofia akakaa upande wa kichwa chake akasema: “Mwenyezi Mungu akurehemu ewe mama yangu mpendwa baada ya mama yangu mpendwa.” Akataja sifa zake juu yake na kumvisha sanda kwa joho lake, kisha Mtume akamwita Usama bin Zaydi, Abu Ayubu Al-Ansari, Umar bin Al-Khattab na kijana fulani mweusi ili wakachimbe kaburi.

Wakalichimba kaburi lake na walipofikia kuchimba mwanandani Mtume akaichimba hiyo yeye mwenyewe kwa mkono wake na kuutoa mchanga kwa mkono wake. Alipomaliza akaingia kwenye mwanandani kisha akalala ndani yake na akasema:

“Mwenyezi Mungu ndiye anayehuisha na kufisha, na Yeye yu hai wala hatokufa. Ewe Mwenyezi Mungu, msamehe mama yangu mpendwa Fatima binti Asad na uyapanue makazi yake kwa haki ya Mtume Wako na Manabii ambao wamepita kabla yangu.”5

Imepokewa kuwa As-Sawadi bin Qaribi alimsomea Mtume utenzi wake ambao ndani yake alitawasali kupitia Mtume (s.a.w.w.), akasema:

Nashuhudia kwamba hapana Mola isipokuwa Allah. Na kwamba wewe ndiye mwenye kuaminiwa kuhusu mambo ya kila asiyekuwepo.

Nawe ndiye uliye karibu mno kama njia kwa Mwenyezi Mungu kuliko Mitume wengine, ewe mwana wa watukufu walio wema.

Tuamrishe yale yanayokufikia ewe mbora wa Mitume, japo yatakuwa mazito.

Na uwe mwombezi wangu siku ambayo mwombezi yeyote hatomnufaisha As-Sawadi bin Qaribi japo kwa sehemu ndogo.6
________________________
1. Sunanu Ibnu Majah 1: 441, Hadithi ya 1385. Musnad Ahmad 4: 138 Hadithi ya 16789. Mustadrak Asw-Swahahain cha Al-Hakim An-Naisaburi 1: 313. Al- Jamius-Swaghir cha As-Suyutwi: 59. Minihajul-Jamiu 1:286.

2. At-Tawassuli cha Subhani: 69. Amenukuu kutoka kwenye At-Tawassulu ila Haqiqatu At-Tawassul cha Ar-Rifai: 158.

3. Sunanut-Tirmidhi: 5/ 531 Hadithi ya 3578. As-Sunanu Al-Kubra cha An-Nasai: 6, 169, Hadithi ya 10495.

4. Sunanu Ibnu Majah 1: 256 Hadithi ya 778, mlango wa kwenda kwenye Sala

5. Kashful-Irtiyabi: 312, amenukuu toka kwenye Wafaul-Wafai na Ad-Duraru As-Saniyatu: 8..

6. Ad-Duraru As-Saniyatu: 27. At-Tawassulu ila Haqiqatu At-Tawassuli: 300. Fat'hul-Bari 7: 137

Sera ya waislamu zama za uhai wa Mtume (s.a.w.w.) na baada ya kufa kwake ni kutawasali kupitia Mtume (s.a.w.w.) na Mawalii wa Mwenyezi Mungu na kuomba shufaa kupitia vyeo vyao na heshima zao mbele ya Mwenyezi Mungu. Ifatayo ni mifano ya sera hiyo ya waislamu:

a) Baada ya kufariki Mtume wa Mwenyezi Mungu Abu Bakr alisema: “Ewe Muhammad tutaje mbele ya Mola wako Mlezi na tuwe ndani ya kumbukumbu yako.”1

b) Al-Hafidh Abu Abdullah Muhammad bin Musa An-Nu’mani ndani ya kitabu chake Misbahu Adh-Dhulami amesema: “Hakika Al-Hafidh Abu Said As-Samuani ameeleza tuliyopokea kutoka kwake kutoka kwa Ali bin Abu Twalib kuwa (a.s.) alisema: “Baada ya siku tatu tangu tulipomzika Mtume wa Mwenyezi Mungu alitujia bedui akajitupa juu ya kaburi la Mtume (s.a.w.w.) na kumwagia sehemu ya udongo wake juu ya kichwa chake na kusema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu ulisema tukasikia kauli yako. Ukatuelimisha kuhusu Mwenyezi Mungu na tukaelimika kuhusu wewe, na miongoni mwa yaliyoteremshwa ilikuwa ni: “Lau wangelikujia walipojidhulumu nafsi zao wakaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu...” Na nimeshaidhulumu nafsi yangu na nimekujia uniombee msamaha.” Basi akaitwa toka kaburuni: Hakika Yeye (Mwenyezi Mungu) ameshakusamehe.”2

c) Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa keshamfunza mtu fulani namna ya kuomba awe anamwomba Mwenyezi Mungu, kisha awe anamse- meza Mtume na awe anatawasali kupitia yeye (s.a.w.w.), kisha amwombe Mwenyezi Mungu akubali shufaa yake, aseme:

“Hakika mimi nakuomba na natawasali kwako kupitia Nabii wako Nabii wa Rehma. Ewe Muhammad; ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu; hakika mimi ninatawasali kupitia wewe kwa Mola Wangu Mlezi katika haja yangu ili nikidhiwe. Ewe Mwenyezi Mungu mfanye awe mwombezi wangu.”3

d) Ndani ya Sahih Bukhari imekuja kuwa: Umar bin Al-Khattab alikuwa kila wanapopatwa na ukame huomba mvua kupitia Abbas bin Abdul-Mutwalibi (r.a.) na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu tulikuwa tuk- itawasali kwako kupitia Mtume wetu na ukitupa mvua, basi sasa tunatawasali kwako kupitia ami ya Mtume wetu basi tupe mvua.” Bukhari amesema: “Basi hupewa mvua.”4

e) Al-Mansur Al-Abasiyu alimuuliza Malik bin Anas –Imam wa madhehebu ya Maliki - kuhusu namna ya kumzuru Mtume (s.a.w.w.) na namna ya kutawasali kupitia yeye…. Akamwambia Malik: Ewe Abu Abdullah, nielekee Kibla niombe au nimwelekee Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Malik akajibu: Kwa nini unampa kisogo Mtume wakati yeye ndiyo njia yako na njia ya baba yako Adamu Siku ya Kiyama? Bali mwelekee na umwombe akuombee na Mwenyezi Mungu atakubali maombi yako, kwani Mwenyezi Mungu anasema: “Na lau walipozidhulumu nafsi zao….”5

f) Shafi’i amesoma beti hizi mbili za shairi lake akitawasali kupitia Kizazi cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.):

“Kizazi cha Mtume, wao ni njia yangu na wao ni wasila wangu kwa Mwenyezi Mungu. Kwao wao kesho nataraji kupewa kitabu changu kwa mkono wa kulia.”6

Baada ya maelezo yote yaliyotangulia miongoni mwa dalili, hoja na ushahidi wa kihistoria inawezekana kusema kwamba: Manabii na watu wema miongoni mwa waja Wake wanahesabiwa kuwa ndio njia za kishe- ria ambazo alizikusudia Mwenyezi Mungu kwenye kauli yake: “Enyi mlioamini mcheni Mwenyezi Mungu na tafuteni njia ya kumfikia.”7

Na hapa njia inajumuisha mambo ya Sunna na wala haikomei kwenye kutekeleza mambo ya faradhi na kujiepusha na mambo ya haramu pekee.
________________________
1. Ad-Durarus-Saniyatu fi Radi A'lal-Wahabiyya: 36.

2. Wafaul-Wafai cha As-Samuhudiyu 2: 1361.

3. Majumuatu Ar-Rasaili Wal-Masaili cha Ibnu At-Taymiyya 1: 18.

4. Sahih Bukhari: Mlango was ala na kuomba mvua 2: 32, Hadithi ya 947.

5. Kutoka kwenye Wafaul-Wafai cha As-Samuhudiyu 2: 1376.

6. As-sawaaiqul-Muhriqa: 274.

7. Al-Maida: 35.

Maimamu wa Ahlul-Baiti wamehimiza sana kutawasali kupitia Qur’ani tukufu, Mawalii wa Mwenyezi Mungu na mengineyo. Atakayerejea kwenye vitabu vya Shia Imamiya, vitabu vyao vya Hadithi na vitabu vyao vya dua atalikuta ni jambo la wazi kabisa kiasi kwamba haiwezekani kulishakia. Ifatayo ni baadhi ya mifano:

a) Al-Harith bin Al-Mughira amepokea, amesema: “Nilimsikia Abu Abdullah akisema:

“Iwapo mmoja wenu anataka kumwomba Mola Wake Mlezi kitu kati ya haja za kidunia, basi asianze mpaka aanze kumhimidi na kumsifu Mwenyezi Mungu Mtukufu na kumtakia rehema Mtume (s.a.w.w.) kisha amwombe Mwenyezi Mungu haja zake.”1

b) Kutoka kwa Abu Jafar (a.s.) amesema: Jabir Al-Answari amesema: “Nilimwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): Unasemaje kuhusu Ali bin Abu Twalib? Akasema: “Yeye ni nafsi yangu.”

Nikasema: Unasemaje kuhusu Hasani na Huseini? Akasema: Wenyewe wawili ni roho yangu na Fatuma mama yao ni binti yangu, kinanichukiza kile kinachomchukiza na kinanifurahisha kile kinachomfurahisha. Nashuhudia kwa Mwenyezi Mungu kuwa hakika mimi ninapigana na wanaopigana nao na nina amani na wale wanaokaa nao kwa amani. Ewe Jabir, ukitaka kumwomba Mwenyezi Mungu na akujibu ombi lako mwombe kupitia majina yao, hakika yenyewe ni majina vipenzi kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.”

c) Kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.): “Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi naelekea kwako kupitia Muhammad na Kizazi cha Muhammad na naku- rubia kwako kupitia wao na ninawatanguliza huku nikiwa na haja.”2

d) Imam Ali Kiongozi wa waumini (a.s.) ndani ya dua yake alikuwa akisema: “……..kwa haki ya Muhammad na Kizazi cha Muhammad iliyo juu yako, na haki Yako tukufu juu yao wapelekee Rehema kama unavyostahiki na unipe kilicho bora mno kuliko vile ulivyowapa waombaji miongoni mwa waja wako waumini waliotangulia na kilicho bora mno kuliko vile utakavyowapa waja wako waliosalia miongoni mwa waumini.” 3

e) Imam Abu Abdullah Husein (a.s.) katika dua yake ya Arafa amesema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu hakika sisi tunaelekea kwako - jioni hii ambayo umeifaradhisha na kuitukuzakupitia Muhammad Nabii wako na Mteule wako miongoni mwa viumbe vyako.4

f) Imam Zainul-Abidin amesema ndani ya dua yake ya munasaba wa kuingia Mfungo wa Ramadhani: …..Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi nakuomba kupitia haki ya Mfungo huu na haki ya atakayejibidisha humu kwa Ibada, mwanzo wake hadi mwisho wake; kuanzia Malaika uliyemkurubisha au Nabii uliyemtuma au mja mwema uliyempenda…..” 5
________________________
1. Biharul-Anwar: juzuu 93, kitabu cha utajo na dua, mlango wa 17, Hadithi ya 19 kutoka kwenye Iddatu Ad-Dai: 97.

2. Biharul-Anwar, Juz 94, mlango wa 28, Hadithi ya 19. Kutoka kwenye Da’awatul-Qutubi Ar-Rawandiyu.

3. As-Swahifatul-Alawiyya cha As-Samahijiyu: 51.

4. Iqbalul-Amali cha Ibnu Twawusi 2: 85.

5. As-Swahifatus-Sajadiyya: Dua namba 44.

Imesemekana haiwezekani kutawasali kupitia mfu, na kitendo hiki ni kibaya kiakili kwa sababu maiti haina uwezo wa kujibu, na kuwa kutawasali kupitia yeye ni kusemesha kisichokuwepo. 1

Dai hili linapingwa na linapingana na Qur’ani tukufu. Ifuatayo ni mifano halisi kutoka ndani ya Aya za Qur’ani tukufu ambazo zinakanusha dai la kuwa maiti ni kisichokuwepo:

i) “Na humo watapata riziki zao asubuhi na jioni.”2

Kundi hili la Aya liliteremka kuzungumzia haki ya waumini, kwani lin- abainisha aina ya umuhimu watakaofanyiwa duniani na Akhera.

Na nyingine ikaweka wazi:

النَّارُ يُعْرَضُونَ عَلَيْهَا غُدُوًّا وَعَشِيًّا ۖ وَيَوْمَ تَقُومُ السَّاعَةُ أَدْخِلُوا آلَ فِرْعَوْنَ أَشَدَّ الْعَذَابِ {46}

“Ni moto wanawekewa asubuhi na jioni. Na siku kitakapotokea Kiyama waingizeni watu wa Firauni katika adhabu kali zaidi.”Ghafiru:46.

Mwenyezi Mungu anabainisha adhabu watakayoipata wenye kuasi na makafiri katika maisha ya Barzakhi, jambo linalojulisha kuwa wao ni hai baada ya kifo na kabla ya Kiyama, kwani kusimama Kiyama kumetajwa baada ya kuwekewa moto Asubuhi na Jioni. Hivyo ikithibiti kuwa kifo si kutoweka bali ni uhai mpya, basi je, inawezekana kuwasiliana na mfu au haiwezekani? Kwa madai kuwa uhai wa Barzakhi unazuia kuwasiliana naye?

Jibu ni: Kuna Aya nyingi ndani ya Qur’ani tukufu - ukiongezea na Sunna tukufu - zinazoonyesha uwezekano wa mwanadamu aliyomo duniani kuwasiliana na mwanadamu hai aliyomo ndani ya ulimwengu wa Barzakhi. Miongoni mwa Aya hizo ni hizi zifuatazo:

Wito wa Nabii Saleh kwa kaumu yake akitaka wamwabudu Mwenyezi Mungu na akaiamuru isiudhuru muujiza wake, na baada ya kumchinja ngamia jike na kuasi amri ya Mola wao Mlezi, Mwenyezi Mungu anasema:

فَأَخَذَتْهُمُ الرَّجْفَةُ فَأَصْبَحُوا فِي دَارِهِمْ جَاثِمِينَ {78}

فَتَوَلَّىٰ عَنْهُمْ وَقَالَ يَا قَوْمِ لَقَدْ أَبْلَغْتُكُمْ رِسَالَةَ رَبِّي وَنَصَحْتُ لَكُمْ وَلَٰكِنْ لَا تُحِبُّونَ النَّاصِحِينَ {79}

“Na tetemeko likawanyakua na wakawa majumbani mwao kifudifudi wamekwishakufa.*Basiakawaachanaakasema:“Enyikaumuyangu, bilashakanimekufikishieniujumbewaMola WanguMlezina nimekunasihini lakini nyinyi hamuwapendi wenye kunasihi.”
Al- ‘Aaraf: 78-79.

Tazama jinsi Mwenyezi Mungu anavyotoa habari kwa uhakika na uyakini kuwa tetemeko liliangamiza umma wa Saleh (a.s.) na wakawa majumbani mwao kifudifudi wamekufa. Baada ya hapo anatoa habari kuwa Nabii Saleh (a.s.) aliwaacha kisha akawaambia kwa kusema:

لَقَدْ أَبْلَغْتُكُمْ رِسَالَاتِ رَبِّي وَنَصَحْتُ لَكُمْ ۖ {93}

“Bila shaka nimekufikishieni ujumbe wa Mola wangu Mlezi na nimekunasihini lakini nyinyi hamuwapendi wenye kunasihi.”Al- Aaraf:93.

Maelezo yaliyotoka kwa Saleh (a.s.) kuiambia kaumu yake yalikuwa ni baada ya kuangamia kwao na kifo chao, kwa ushahidi wa kauli: “Na akawaacha” iliyoanza kwa (Al-Fau) yenye kuhisisha kuwa maelezo yalitoka baada tu ya kaumu kuangamia.

Nabii Shuaybu (a.s.) aliwasemeza watu wake baada ya kuangamia kwao kwa kauli ya Mwenyezi Mungu:

فَتَوَلَّىٰ عَنْهُمْ وَقَالَ يَا قَوْمِ لَقَدْ أَبْلَغْتُكُمْ رِسَالَاتِ رَبِّي وَنَصَحْتُ لَكُمْ ۖ فَكَيْفَ آسَىٰ عَلَىٰ قَوْمٍ كَافِرِينَ {93}

“Basi akawaachilia mbali na akasema: “Enyi kaumu yangu, bila shakanimekufikishieniujumbewaMolaWanguMlezinanimekupeni nasaha,basivipinihuzunikejuuyamakafiri.” -Al-Aaraf:93.

Usemi wa Shuaybu kuwaambia kaumu yake umetoka baada ya kuangamia kwao. Hili linahimiza uwezekano wa kuwasiliana nao, kwani laiti walioangamia kwa tetemeko wangelikuwa hawasikii usemi wa Shuaybu (a.s.) na Saleh (a.s.) basi nini maana ya wao wawili kuwasemeza?

Wala haisihi kufasiri kuwa ni maelezo ya kuhuzunika kwa sababu tafsiri hiyo ni kinyume na maana inayojulikana moja kwa moja, na si sahihi kwa mujibu wa misingi ya kitafsiri.

Ama baadhi ya hadithi tukufu ambazo zinaashiria uwezekano wa kuwa na mawasiliano na roho za wafu ni kama zifuatazo:

Imepokewa kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kuwa alisimama kwenye Kisima cha Badri na kuwasemeza mushirikina ambao walikuwa wameuawa na miili yao ikiwa imetupwa kwenye Kisima. Kutoka kwa Anas bin Malik amesema: Sahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu walimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu usiku akisema: “Enyi watu wa kisimani, ewe Ut’batu bin Rabia, ewe Umayya bin Khalaf, ewe Abu Jahl bin Hisham...”
Akataja orodha ya waliyokuwemo kisimani. “Je, mmekuta ni kweli aliyowaahidini Mola wenu Mlezi? Kwani mimi nimekuta ni kweli aliyoniahidi Mola Wangu Mlezi.”

Waislamu wakasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hivi unawaita watu ambao wameshakufa?” Akasema: “Nyinyi hamsikii niyasemayo kuliko wao, lakini wao hawawezi kunijibu.”3

Hakika waislamu bila kujali madhehebu yao humtolea salamu Mtume wa Mwenyezi Mungu ndani ya sala na mwishoni mwake wakisema: “Amani iwe juu yako ewe Nabii na Rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake.” Na hakika Sunna hiyo ya Mtukufu Mtume imethibiti kwa ajili yake zama za uhai wake na baada ya kifo chake, hivyo mawasiliano yetu na uhusiano wetu na Nabii (s.a.w.w.) havikatiki. Salamu hii haijulishi uwezekano wa kuwasiliana na roho yake (s.a.w.w.) tu, bali zaidi ya hapo inathibitisha kwa yakini kuwa mawasiliano yapo.

Imepokewa kutoka kwake kuwa: “Atakayenizuru baada ya kifo changu na akanitolea salamu nitamrudishia salamu mara kumi na watamzuru Malaika kumi wakimtolea salamu. Na hapana yeyote atakayenisalimia ndani ya nyumba yoyote ile isipokuwa Mwenyezi Mungu hunirudishia roho yangu mpaka nami nimrudishie salamu.4

Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: “Mwenye kunizuru baada ya kufa kwangu ni kama amenizuru wakati wa uhai wangu….5

Ikithibiti kuwa inawezekana kuwasiliana na mtu aliyomo kwenye maisha ya Barzakhi, je inaruhusiwa kumwomba na kutawasali kupitia kwake ili kukidhiwa haja, au kufanya hilo ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu kwa ushahidi wa kauli yake (s.w.t.): “Hakika mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu?”6

Jibu: Hakika mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu na kwa utashi Wake na kwa ridhaa Yake hutokea mambo, isipokuwa hilo halizuii kuthibiti shufaa ya Manabii na Mawalii duniani na Akhera baada ya idhini kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kama linavyoonekana hilo pale ilipothibiti kwa Isa (a.s.) kuumba na kuhuisha wafu na kuponya wagonjwa baada ya idhini kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Na kwa kuwa mambo huenda kwa kufuata Kanuni ya ‘Sababu na Kisababishwa’ ndio maana tunamkuta Musa (a.s.) akisema:

قَالَ هِيَ عَصَايَ أَتَوَكَّأُ عَلَيْهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِي وَلِيَ فِيهَا مَآرِبُ أُخْرَىٰ {18}

“Akasema: Hii ni fimbo yangu ninaegemea na ninaangushia majani kwa ajili wanyama wangu; tena ninaitumia kwa matumizi mengine.” Twaha:18.

Hivyo Manabii pamoja na Utakaso wao lakini wametaka msaada kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, mpaka Mtume wa Mwenyezi Mungu akateremshiwa:

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ حَسْبُكَ اللَّهُ وَمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ {64}

“Ewe Nabii Mwenyezi Mungu anakutosha wewe na yule aliyekufuata katikawaumini.”
Al-Anfali:64

Maana inayojulikana kutoka kwenye Aya ni Mtume kutaka msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kutoka kwa waumini kama Isa (a.s.) alivyotaka kusaidiwa na wanafunzi wake, akasema:

مَنْ أَنْصَارِي إِلَى اللَّهِ ۖ {52}

“NaniatakuwamsaidiziwangukwaMwenyeziMungu?”Al-Imrani: 52
Na kama Musa (a.s.) alivyotaka kusaidiwa na ndugu yake Haruna (a.s.) na Mwenyezi Mungu akamjibu: “Karibuni tutautia nguvu mkono wako kwanduguyako.”7na8 Kisha tunamkuta Mwenyezi Mungu ameomba msaada kutoka kwa waja wake akasema:

إِنْ تَنْصُرُوا اللَّهَ يَنْصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ {7}

“MkimsaidiaMwenyeziMunguatawasaidia.”Muhammad:7.

Na akasema:

وَالَّذِينَ آمَنُوا وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَالَّذِينَ آوَوْا وَنَصَرُوا أُولَٰئِكَ هُمُ الْمُؤْمِنُونَ حَقًّا ۚ {74}

“Na wale waliowapa mahala pa kukaa na wakainusuru hao ndio wau- miniwakweli.”
Al-Anfali:74.

Hivyo tukikiri kuwa kuomba msaada na kutawasali kupitia asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni jambo linaloruhusiwa kwa sababu ni kwa idhini Yake na utashi Wake, na si kwa kujitegemea; basi ni ipi dalili ya kuomba msaa- da kupitia maiti? Ilihali kilichothibiti ni kuomba msaada zama za uhai wake kupitia Mtume (s.a.w.w.) au Walii na si wakati wa ufu wake.

Hakika Sahaba hawajakanusha kutawasali kupitia Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) zama za uhai wake na baada ya kifo chake.

Kutawassali Kupitia Manabii Na Mawalii Baada Ya Vifo Vyao

Miongoni mwa sera za waislamu ni kutawasali kupitia Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) baada ya kifo chake:

Ndani ya Musnad ya Ahmad mna: “Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba kwa haki ya wanaokuomba na ninakuomba kwa haki ya mwendo wangu huu, kwani mimi sikutoka kwa maringo na majivuno wala kujionyesha wala kutaka kusifiwa, nimetoka kwa kuogopa ghad- habu zako na kutafuta radhi zako. Basi ninakuomba uniepushe na moto na unisamehe madhambi yangu kwani hapana anayesamehe madhambi isipokuwa Wewe.”9

Hadithi hii iko wazi mno katika maana yake na inajulisha ruhusa ya kutawasali kupitia Mawalii wao wenyewe na wala si kupitia dua zao. Na ni tamko jumuisho linalojumuisha waombaji wote kutoka kwa Adam mpaka siku ya mwombaji, bali linajumuisha Malaika pia na waumini miongoni mwa Majini. Na wala haiwezekani kuihusisha na waombaji wa siku ya leo tu, au walio hai tu, kwani hakuna dalili inayoelekeza Hadithi kwenye maana hiyo na wala haina kihisishi mahususi kutoka nje.10

ii) Ndani ya An-Nasai na At-Tirmidhi imepokewa: “Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba na kutawasali Kwako kupitia Mtume wako Mtume wa Rehema, ewe Muhammad, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu hakika mimi natawasali kwa Mola Wangu Mlezi katika haja yangu kupitia kwako ili ikubaliwe, ewe Mwenyezi Mungu mfanye Muhammad kuwa mwombezi wangu.”

Hizi ni miongoni mwa dua ambazo waislamu wanatawasali kwazo kupitia Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) baada ya kifo chake.

Mdahalo Dhidi Ya Ibnu Taymiyya Kuhusu Mwelekeo Wake Katika Dua Hii

Kumetokea tofauti kati ya Ibnu Taymiyya na wafasi wake kuanzia As- Salafiya mpaka Mawahabi juu ya suala la kutawasali kupitia Manabii na Mawalii baada ya vifo vyao. Yeye anaona kuwa hairuhusiwi kutawasali kupitia wafu, na yafuatayo ni maneno yake kisha mdahalo:

“Katika Tawassuli hakuna kuomba kupitia viumbe wala kutaka msaada kupitia kiumbe bali ni kuomba na kutaka msaada kupitia Mwenyezi Mungu. Lakini kuna kuomba kupitia jaha yake kama ilivyo ndani ya Sunan Ibnu Majah kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kuwa alisema katika dua ya mtu aliyetoka kuswali aseme: “Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba kupitia haki ya waombaji Kwako……. Hadithi.”

Hivyo ndani ya Hadithi hii aliomba kupitia haki ya waombaji kwa Mwenyezi Mungu…. Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ameweka juu ya nafsi yake haki…. (mpaka akasema): Na kuna kundi limesema: Katika dua hii hakuna ruhusa ya kutawasali kupitia yeye (s.a.w.w.) baada ya kifo chake na kipindi cha kutokuwepo kwake, bali kuna kutawasali zama za uhai wake na kipindi cha kuwepo kwake……”

Kisha akaanza kutetea rai hii ya mwisho, akasema: “Na hiyo Tawassuli ya kupitia yeye (s.a.w.w.) ni kuwa wao walikuwa wakimwomba awaombee na yeye anawaombea na wanaomba pamoja naye na wanatawasali kupitia shufaa yake na dua yake.”

Akafananisha hilo na Hadithi ya bedui: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu mali zimeangamia na njia zimekatika, tuombee Mwenyezi Mungu azizuie dhidi yetu.”

Akasema: “Huku ndiko kulikuwa kutawasali kwao kupitia yeye (s.a.w.w.) katika kuomba mvua na mfano wake, na Mtume alipofariki walitawasali kupitia Abasi, na pia Muawiya bin Abu Sufiyan aliomba mvua kupitia Yazid bin Al-Aswad Al-Jarashi akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu hakika sisi tunaleta maombi kwako kupitia wabora wetu, ewe Yazid inua mikono yako kwa Mwenyezi Mungu……”

Kisha akamalizia kwa kusema: “Hakuna mwanachuoni yeyote aliyesema kuwa inaruhusiwa kisheria kutawasali na kuomba mvua kupitia Mtume na Walii baada ya kifo chake wala kipindi cha kutokuwepo kwake. Na wala hawakulifanya hilo kuwa ni Sunna katika kuomba mvua wala katika kuom- ba msaada wala katika dua za aina nyingine, ilihali dua ndio ubongo wa ibada.”11

Ndani ya maneno haya kuna mgongano na mchanganyo na upotoshi wa maneno waziwazi zaidi ya sehemu moja. Tutaanza kuufichua kabla ya kutoa dalili juu ya maudhui.

1. Amechanganya kati ya kutawasali kupitia Mtume (s.a.w.w.) na kutawasali kupitia jaha. Kuna tofauti kubwa kati ya kauli yake: “Ewe Muhammad, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hakika mimi naelekea kwa Mwenyezi Mungu kupitia kwako.” Na kati ya kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu kupitia haki ya waombaji kwako.” Au “Ewe Mwenyezi Mungu kupitia haki ya Muhammad (s.a.w.w.).”

Wa mwanzo ameelekea na kutawasali kupitia yeye (s.a.w.w.) na wa pili kaelekea na kutawasali kupitia haki yake na jaha na cheo chake, hivyo aina mbili hizi za kutawasali za kupitia Manabii na Mawalii zinaingia chini ya kifungu hiki. Na Ibnu Taymiyya amemfasiri wa mwanzo kuwa ni sawa na wa pili, nayo ni tafsiri isiyo sahihi.

2. Hapa amechanganya kama alivyochanganya kabla, kati ya kuelekea kupitia Mtume (s.a.w.w.) na kati ya kuomba akuombee. Kitofautishi kiko wazi na wala haifichiki kuwa amefanya hili ili kupotosha maana na wala si jingine. Na ndio maana utamwona alipotoa dalili kutumia Hadithi ya bedui alileta kipande tu na akaacha kauli yake tuliyoitaja mwanzo “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hakika sisi tunakufanya mwombezi kwa Mwenyezi Mungu.” Ambayo Mtume (s.a.w.w.) aliithibitisha.

3. Amejipinga mwenyewe katika kunukuu kutoka kwa wanachuoni, kisha akakimbilia kwenye kifungu cha dua ya kuomba mvua na kitu kingine ili kupotosha bongo na si jingine, kwa sababu alirudi na kukusanya aina zote za dua “Na wala hawakulifanya hilo kuwa ni Sunna katika kuomba mvua wala katika kuomba msaada wala katika dua aina nyingine.”

Mwanzo amenukuu kutoka kwa wanachuoni kauli yao ikiruhusu kutawasali kupitia Mtume (s.a.w.w.) zama za uhai wake na baada ya kifo chake, kisha akarudi akasema: “Hakuna mwanachuoni yeyote aliyesema inaruhusiwa kisheria kutawasali na kuomba mvua kupitia Mtume na Walii baada ya kifo chake.” Na hapa tunakuja kwenye yale yanayopingana na haya madai yake kupitia dalili ambazo yeye mwenyewe baadhi yake amekiri kuwa ni sahihi. Tumethibitisha na tunasisitiza kuwa Ibnu Taymiyya hajapata maelezo (ya Qur’ani na Hadithi) yanayoonyesha kukatazwa kutawasali kupitia Mtume (s.a.w.w.), hivyo akakimbilia kutafsiri baadhi ya maelezo kwa maana isiyotafsirika.

Na hapa tutamwona jinsi gani anazungusha mgongo wake dhidi ya maele- zo ambayo yamethibiti kwake kuwa ni sahihi kwa namna isiyo na shaka: Ananukuu kwa njia anazojua kuwa ni sahih kutoka kwa Sahaba Mheshimiwa Uthman bin Hunayf kuwa anawafunza watu kutawasali kupi- tia Mtume (s.a.w.w.) zama za Uthman bin Affan, kisha anamfanya mwombezi kupitia habari zilizowakilishwa kutoka kwa wanachuoni waliotangulia.

Anasema: Al-Bayhaqiyu amepokea kuwa kuna mtu alikuwa akienda mara kwa mara kwa Uthman bin Affan kumwomba haja na Uthman alikuwa hamjali na wala hamtekelezei haja yake, basi mtu huyo akakutana na Uthman bin Hunayf na kumlala

Share this article

Comments 0

Your comment

Comment description

Latest Post

Most Reviews

MOST READ